Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Nakuheshimu -SHIKAMOO!Hivi hii ni Salamu?

>> Monday, January 15, 2007




Ni rahisi kusema Watanzania tumelelewa katika maadili yatufanyayo tuheshimu wakubwa zetu. Wengine watasema tunawaheshimu sana ndio maana hata katika salamu tunasema -SHIKAMOOO!Tukitarajia Wakubwa wajibu MARAHABA!

Swali:
Lakini ni kweli kuwa tunawaheshimu tuwapao Shikamoo?

Au tunawaogopa?

Nakumbuka tulikuwa tunatoa shikamoo kwa walimu tuliowadharau!
Nakumbuka tulitoa shikamoo kwa ndugu na jamaa ambao kisirisiri hatuwaheshimu lakini hatuwezi kusema.
Wengine hutoa shikamoo hata kwa wazazi kwa sababu usipoitoa utapigwa bakora.

Shikamoo= nikochini ya miguu yako.Hivi ni kweli hiyo?
Acha kunizingua!

Dondoo:
Unakumbuka ulivyotoa shikamoo kwa mtu halafu ukastukia ni mdogo kwako?

Hivi Shikamoo yako ni heshima , uoga au umekosa chakusema?
Haya bwana nakukubalia , labda ni salamu!

Lakini kama ni salamu, salamu maana yake ni nini?
Kama salamu ni kujuliana hali, sasa unapata kujua hali ya mtu kwa kumpa shikamoo?

Hivi shikamoo ni nini?

Simon: SHIKAMOO!
Wewe jibu lako:.........

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP