Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Tufanye tu kwa vitendo!

>> Thursday, January 18, 2007

Kuna mambo mengi sisi binadamu
tuyaongeleayo,
tuyalaamikiayo,
tuyapendayo ,
tuyachukiayo,
tuyatamaniyo,
tuyaombeayo,
tuyaviziayo,
tuyasengenyayo,
tuyachombezayo,
tuyakanayo .......... tutakayo kuyaacha.................nk

Kuna mambo mengi tujuayo kabisa kuwa ndio jibu la maswali
tujiulizayo,
ndio jawabu ya matatizo tuliyonayo,
ndio tuyatakayo,
ndio ukweli, ndio busara,..............

Cha ajabu pamoja nakujua yote hayo , haya mambo hata sikumoja hatuchukui hatua kuyafanya , kwa vitendo, hatuyatekelezi kutokana na ukweli hatuanzi kupiga ile hatua ambayo ni ya utekeleza tu.

Inasemekana asilimia kubwa ya watu kabla hawajafa hujutia yale ambayo walikuwa nauwezo wa
kuyatenda,
kuyafurahia,
kuyajaribu..........
halafu hawakuchukua hatua walizojua kuwa zitatimiza matakwa hayo, kwa kifupi hawakuyatenda.
Asilimia kubwa yetu tunaogopa kufanya makosa, hivyo tunajichunga kuchukua hatua kwa kuogopa tusije tukajuta. Chakufurahisha ni kwamba kutokana na kujichunga na kutochukua hatua ni ukweli hatufanyi makosa , hatukosei lakini pia hakuna litendekalo, hivyo hatupati tuyatakayo.

Swali:
Hivi sisi kama binadamu, tunaweza kweli kukwepa kukosea?
Hivi ni busara kutotimiza matakwa yetu kwa sababu ,labda tutachekwa,au kwa kuhisi tu haiwezekani?

Basi kama nikutafuta shule , tuzitafute
kama ni kazi , tuende kuzitafuta
Kama ni kuandika kitabu, siri ni kuanza kuandika tu.

Kama ni kumueleza Zubeda kuwa unampenda basi tufanye hivyo
Tuanze kufanya na........,tutekeleze..........., tuombe msamaha kwa......., na tu..........

Au ngojea niseme...


Ukweli ni kwamba bila kuchukua hatua mpaka milele hakuna kitakacho fanyika!
Sijui unanielewa?

Tukumbushane kuchukua hatua na kutekeleza.Tuamue na tutekeleze.

Mimi naamini inawezekana.Tujaribu ,halafu tujaribu tena na tena na tena.......
Kama ni kweli ndicho,ndilo,....tutakalo, takacho....tutafurahia matokeo, tutajua utamu wake, tutaendelea.

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP