Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Wakati tunaendelea KUKATAZA wanawake WASITAHIRIWE au KU-ze-KUKEKETWA!

>> Sunday, March 01, 2009

Nashauri,...
..... tuendelee kupinga mkeketo wa NANIHII kutokana na madhara ya KIAFYA, Kisaikolojia na hata ya KIKUJINOMA.

Tukumbuke tu!
......Ukichomoa uwe na CHA kuingiza kama hutaki kishimo kibakie kitupu.

Kumbuka,...
...hata kama unataka kuacha POMBE, jiandae kuwa na KITU kingine kitakacho CHUCHUMAA pale ULEVI ulipokuwa unachuchumaa , la sivyo utarudia POMBE a.k.a KILAJI tu, kama umeacha tu na KIU ipo tu na haina tiba tofauti ijaziayo palipoachwa na KILAJI.

Kumbuka pia moja ya kiwafanyacho watu waende KISIMANI ni kwa sababu za kuishi katika mazingira yenye KISIMA la sivyo kama katika mazingira kungekua hakuna KISIMA , labda tungeweza kwenda NAO kuvizia mademu bombani.
Swali:

  • AU?
Kwa hiyo wakati unaacha au kuachisha, jiandae au ANDAA vilevile MAZINGIRA yasaidiayo ari mpya na nguvu mpya ya MUACHO . Na kama nia yako ni KUOKOKA na KUACHA POMBE , labda kwepa walevi na jichanganye na WALOKOLE, ingawa labda kama unajiamini , unaweza kuwa Mlokole wa Kikristu ujichanganyaye na waislamu na kuzawadiwa KUJUA zaidi ulokole na UISLAMU.
Swali:

  • AU?
  • Si sehemu watumiayo kisima , watu wanaweza kuridhika na bomba la maji kama tatizo ni MAJI?
Kuna waliofanikiwa kuondoa JANDO na UNYAGO bila kuwa na elimu nyingine imfunzayo KIGOLI shughuli na KIDUME aliye balehe KUSHUGHULIKA , matokeo yake SHUGHULI NA NDOA zinashindikana na tunalaumu TV na MAISHA MAGUMU , ingawa pia siku hizi KUNA wajanja wanafikiri somo litolewalo na SOMO linatosha kufunzwa kwa siku moja kwenye KICHENI PATI .

Somo lililohitaji MKUFUNZI ahakikishe MWANAWANI anapitia UCHUNGU na UTAMU, siku hizi lina WAKUFUNZI wasisitiziao UTAMU TU na ni kwa siku moja, kwa kuandaa LIMTU kwenye maisha yenye MACHUNGU labda zaidi ya utamu.

NI muhimu UKISHACHOMOA , ingiza kama unataka mchezo uendelee.
Swali:
  • Unafikiri madhumuni ya maumivu ya Kidume kukatwa jando bila ganzi yanatimizwa na Kidume akikatwa maeneo na ganzi hospitalini?
  • Hivi madhumuni ya JKT ilikuwa nikuwatesa vijana Tanzania?

NA ,..
..... ni muhimu kabla HUJATOA na unajua kuna madhara ya KISHIMO kubakia kitupu, UJUE utaingiza nini katika kujazia.

SI lazima kama ukitoa SEMENTI , ukijazia UDONGO utakuwa umedhoofisha UMADHUBUTI wa KISHIMO. Labda SEMENTI ilikuwa inaumiza tu KISHIMO na kujazia kishimo KWA unga wa ULEZI ndio ilikuwa na NI dawa ya NYUFA.

Swali:
  • AU?


Kumbuka,...
.... wakeketaji walikuwa na sababu zao na jaribu kuzijua kabla ya KUTOA na kujikuta hauna cha KUINGIZA, au tu kujikuta kuwa kutokana na kutokujua PICHA NZIMA unashindwa kutetea hoja zako za KUCHOMOA hata kama una cha KUINGIZA.
Swali:
  • Hivi ukijua ni lazima uchomoe na hujui cha kuingiza, uiachie MUMOMUMO nini?
  • Kwani ukiacha ya SHETANI ni lazima ufuate ya MUNGU?

Naacha!
Topiki IMENISHINDA:-(
Tuendelee kuwepo South Africa kwa Busi Mhlongo katika- Urbanzulu


Au tu twende PANAMA kukutana na KAFU BANTON enzi hizo kabla watu hawajastukia Reggaeton katika - EL MAD MAN

3 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 1:30 pm  

kusuma kweli ni unyama kabisa yaani nimeshikwa na hasira. Ni jambo ambalo linabidi liangaliwe kwa makini mmo.

Mzee wa Changamoto 9:46 pm  

we Mkodo weeeee! Kazi kwelikweli

Simon Kitururu 9:12 am  

@Dada Yasinta: Kweli tupu!
@Mzee wa Changamoto: :-)

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP