Friday, March 27, 2009

Katika kuomba TITI unaweza usistukie MAKUNYANZI ya CHUCHU!

Katika KUOMBA,...
.... unaweza kuomba mpaka TAKO!:-(

LAKINI tako LAKO linaweza lisiwe na manufaa KAMA ya TITI ingawa huo ndio UKWELI usio tako kwa ATAKAYE kubonyeza TITI!:-(


DUH!

Kuna sababu ,...
.....na ni kawaida KUOMBA ingawa unaweza KUJISIKIA vizuri baada ya kuomba ,.....

....UKIPEWA.....

.... kwa kutumia VIGEZO a.k.a ZE vigezo VIHALALISHAVYO ni KWANINI uliomba MKEBE,.....


.... WAKATI,....


.... wakati ulitaka KIFUTIO TU kwenye MKEBE , na sasa una MKEBE wenye BIKARI na hakuna KIFUTIO kwenye mkebe.:-(

Swali:
  • Unakumbuka kuwa huhitaji kukumbushwa vigezo vya KUCHUCHUMAA KWA MZOEA CHOO CHA KUKAA kama swala ni KUNYA kwenye choo cha shimo ?
  • Unakumbuka kuwa pamoja na maringo yote ya kuchambia maji LABDA wewe ni shujaa wa KUTAWADHA kwa mchanga UKIPEWA nafasi?

Kinamna labda TUMEZALIWA na hatukuomba waliotuzaa WAJIFUNGUE sisi!:-(

Na,...
.... Maisha si ukweli kuwa ni RAHISI ingawa usijinyonge lakini kwa kudhani NI RAHISI vile kuamua kuendelea KUISHI!
Swali:
  • AU?

  • Katika kumuomba MUNGU yote hata yale ya kutaka kufuta makunyanzi ya CHUCHU, si ni KAWAIDA asilimia TISINI za tuombayo hata yasiyo na uhusiano na titi hata la kiume, si HATUJAPATA au MWENYEZI hatupi ndio maana tunaendelea KUOMBEA MPAKA chakula kilichopo mezani badala ya KUSHUKURU?
  • Hivi wanawake wanakumbuka wanaume wana CHUCHU ambazo sina uhakika wameumbwa nazo kwa sababu gani ingawa labda wewe unajua?
  • AU?

NIMEACHA!
Kumbuka NAWAZA tu na LABDA ni UJINGA!


Ngojea twende CONGO Classical Symphony Orchestra walete - Carmina Burana


Au tu Youssou Ndour na Koffi Olomide walete - Festival

Katika KUFIKIRIA yako!

Kama YANAKUGUSA,....
.... ni YAKO.

Mwisho wa siku UKO PEKEE katika YAKO.


Na,....
.... endelea KUTUNZA yaliyo YAKO.

Ingawa , ...
.......TUNAFAIDIKA ukifaidika na YAKO.

Ukweli bado yako ni YAKO.

Daima mhusika mkuu NI WEWE katika YAKO:-(



Lakini...
.....SI ni YAKO?:-)

Unauhakika na YAKO kama huthibitishiwi ......
.....na chako KITHIBITISHO kuwa ni
...
..YAKO?

--------______________------
Swali
  • AU?
:-(







Ngojea Burning Spear atukumbushe MWALIMU wa KIAFRIKA katika - African TEACHER


AU tu JOMO KENYATTA a.k.a Burning Spear azungumzie -THIS EXPERIENCE


SAMAHANI naacha baadhi ya picha zangu na WADAU waliokuwa nami baadhi ya MAENEO juzi ya jana ya juzi:-(

Wadau NIPO lakini....!



Photobucket




Photobucket



Photobucket


Photobucket


Photobucket




Photobucket


Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket


Photobucket


Photobucket




Photobucket





Photobucket









Photobucket



Photobucket





Photobucket








Photobucket





Photobucket




Photobucket



Photobucket





Photobucket

NIpo !....na kuhusu JUMUWATA!

SAMAHANI nimebanwa KISAWASAWA na haya........... , Ugonjwa PIA katikati ya yale ....., ingawa nipo!

Kuhusu JUMUWATA!

Nitapandisha KATIBA ilipofikia halafu TUTAFANYA UCHAGUZI WA VIONGOZI WAPYA watakao iendeleza JUMUWATA kwenye hatua MPYA ili WATANZANIA tujumuike!

SAMAHANI nimepotea hapa na nilishindwa kuwasilisha mengine yote PAMOJA NA HILI!:-(

_______________________---------------------------_______________

TUlia na ORCHESTRA MAKASSY katika kibao - MKE WANGU



Au tu MARIJANI RAJABU aseme -MAYASA

Friday, March 20, 2009

Wivu SINA , lakini sijui NAFIKIRI au NAHISI !

Kama unaamini huna WIVU,...
..... labda USIOMBEE kugundua GHAFLA una wivu USIJE ua MTU na BATA WAKE ghafla!


Na,..
...kila siku TUNAFIKIRI na KUHISI.....
Swali:

  • Unakumbuka kufikiria UNACHOFIKIRIA na kukumbuka ULICHOFIKIRIA jana na KUKIFIKIRIA tena leo?
  • Unakumbuka huwa HUKUMBUSHWI kuhisi?


Ukifikiria sana, LABDA unavyofikiri unavifikiria bado UNAVIHISI.

Na,...
....labda kama unafikiria HUNA wivu, basi wivu wako LABDA umelala na sina uhakika kama ni afya uuamshe udinde au tulia katika mkao huohuo wa sina WIVU ubakie umelala kwa utulivu!

Swali:
  • Au unahisije wewe baada ya kufikiria hili?

Labda kuna UKWELI kuwa ,....
...kila mtu anastaili na mkao wake wakusikilizia WIVU.

Labda kuna UKWELI kuwa,...
...kuna mwenye wivu na MKE WAKE na mwenye wivu na SEHEMU ZA SIRI za mke wake.

Na labda,...
..... wakati SHOGA anakuonea wivu , HATAKI KULA vyako, bali anataka usiwenavyo ULAVYO ili apate nafasi ya KUKUTETA kwa kisauti kisikikacho kikisema; ''Sasa tulione litaringia nini sasa hivi wakati HALINA NANIHII, lione vile mwanya kama PENGO!'', halafu wala ASIMENDEE ulichokuwa una KULA kwa rahaaaa!:-(


Swali:
  • Si unakumbuka roho ya kwanini?

SINAUSHAHIDI!

Lakini,...
... naamini unaweza UKAHISI halafu UKAFIKIRI bado unafikiri wakati UNAHISI tu utakiwacho SASA HIVI KUJUA baada ya KUFIKIRI na KUHISI.:-(
Swali:
  • AU?
NIMEACHA na WIVU SINA!

wiKIENdi njEMa!

Pumzika na Francky Vincent akizungumzia- Fruit de la passion

Bold
Au tu na Zouk Machine katika - maldon

Katika ya KIBINADAMU!

KUNA watumiao madawa ya KULEVYA,...
.. na walao MAPARACHICHI.



KUNA walewao na DINI za KULEVYA,...
....na kwa michikichi wavimbiwa na CHIKICHI.


Katika ya BINADAMUUUU!

Mpaka ya MUNGU wafanya KIBINADAMU.


BIN-ADAMU mwenye DAMU!

Katika kuhakikisha ya MUNGU kibinadamu,...
......atetea miti akimwaga damu.


BINADAMUUU!

Hahitaji KUFUNZWA kupumua na AKIPUMUA astukia kuna damu.



BIN-ADAMU!

HUSAHAU anapumua na ana damu kama TATIZO si KUPUMUA au DAMU!



BINADAMUUU!

----------------------___________--------------------------------------
Nawaza tu Mkuu!.-(


Tutulie tena na DELINQUENT HABITS watukumbushe- Goodtimes


AU tu Delinquent Habits FT Hurricane G (bado ni enzi zile)... wazidi kutukumbusha katika -Underground Connection.[jihadhari na lugha za chooni kama msikiliza maneno]

OMBI: Tafadhali mpigie KURA DADA YETU SANDRA!

Dada yetu SANDRA MUSHI wa SAHARA SOUL FOOD naombeni tumpeni tafu wajameni!

Soma zaidi kwa ung'eng'e.....


Please do vote for my short story – Jasmine – and ask your friends to do the same. Please go to http://www.dailywritingtips.com and vote!!!!



Meanwhile, do visit my website - www.sandrasden.com –where you will find more short stories, waiting to be published. Do visit the forum please and post your thoughts please.



Thank you and have a blessed day!!



Regards,



Sandra.

Wednesday, March 18, 2009

Labda UKITEKENYEKA ulikuwa tayari KUTEKENYWA!

Hutekenyeki NG'O kama hujakaa mkao wa kusikilizia MTEKENYO!
Swali:

  • AU?
Na akupendaye...
...... ukimstukia anafurahia ukicheka AKIKUTEKENYA, unaweza kujifanya UNATEKENYEKA mpaka UKAJISTUKIA mwenyewe jinsi ulivyobarikiwa UIGIZAJI MZURI kwa kuangua kicheko mpaka UKABANJA KIDOOOGO , wakati umeguswa GOTI wakati UKWELI ni kwenye KIKWAPA , chini kidogo ya KITOVU na kwenye wigo wa KIUNO , karibu na mipaka ya shanga TU ndiko UNAKOTEKENYEKA mwanawani weye na GOTI lako linauma.


Na,...
...HAICHEKESHI kama hakuna KITU KINGINE ukijuacho kisababishacho HIKI kikuchekeshacho udhani KINACHEKESHA.


Na,...
......AKUTEKENYAYE ukacheka, kunauwezekano umemruhusu AKUGUSE MWILI na KITEKENYEO ndio maana KAKUTEKENYA ukacheka badala ya KUMPIGA NGUMI pana, KONZI la nguvu, au tu KUMPIGA NGWALA baada ya KURUKA KICHWA , na wakati UMEMPIGA ROBA ukawa unaachia MSONYO MREFU na TUSI LENYE UJAZO ambalo kama sio la nguoni lihusianalo na mama yake, basi ni lile lifananalo na ;'' Mende wee nenda katekenye kuku wenu hukohuko! Nyooo !Lione vile!''


Na,..
...AKUCHEKESHAYE bila kukugusa , kuna uwezekano UNAMSIKILIZA au KUMUANGALIA kitu ambacho siku hizi kinasahaulika duniani, mpaka imefikia siku hizi BIN-ADAMU WENGI kufikia kupeana MPAKA mimba BILA KUANGALIANA na kabla ndoa haijafa, HAWASIKILIZANI.:-(


Swali:
  • Unakumbuka ulimi pia ni kitekenyeo?

Kumbuka tu kuwa,...
...UKIJIWEKA TAYARI , kumbukumbu hata za ulivyowahi KUTEKENYWA zinaweza KUKUCHEKESHA au KUKULIZA!:-(

Na kumbuka,...
... UKITEKENYWA sana UTALIA:-(


NIMEACHA!
Kumbuka NAWAZA tu MKUU!

siKU Njema!
Tutulie na Classic Rumba kutoka kwa KEKELE akidai -DELALI


Au tu Lokassa YA MBONGO amalizie kwa- Marie JOSE

Labda tunapoteza UBORA wa SANAA ya KUSUTA na KUPIGA MKWALA!

Unaweza KUPANDISHIWA sketi wakati UNASUTWA kwa madoido wakati unashushiwa DALILI za tusi MURWAA na adaiye anakupa UKWELI !

Lakini,...
... ni MSAMIATI na mrindimo wa jinsi upewavyo MSUTO na MKWALA ndio hukamilisha FANI katika kuchojoa ugumu wako wa kuumizwa na MSUTO hata ndani ya MKWALA.

  • Sikubishii lakini kama unaridhika na MSUTO ukibaniwa pua wakati UNASUTWA au unapenda tu kukoromewa UKIPIGWA MKWALA katika kujali kwako USIKILIVU wa MKWALA kama MKWALA!

Chakusikitisha ni,....
.... sanaa ya jinsi ya KUSUTA au KUCHIMBA MKWALA inabidi ujifunze mwenyewe.

Na....
  • Hakuna TUISHENI ya kuchimba MKWALA!:-(
  • Hakuna twisheni ya KUSUTA!:-(
.....na darasani WALIMU hakuna!:-(


Uzuri wa KUSUTWA ni uwezo wake wa kukusaidia KUMFAHAMU zaidi AKUSUTAYE hasa kwa kuwa anakuambia mpaka asiyofikiri ANAKUAMBIA, na kukufaidisha kwa KUKUKUMBUSHA kitu kuhusu WEWE MWENYEWE katika DUNIA hii tuliyofikia KUTOJALIANA na kufikia kuendekeza VITA kutokana na kutojulia kumaliza ugomvi kwa MKWALA na KUSUTA wakati amani INABOA.:-(

Swali:
  • Hivi India na Pakistani si wamesaidiwa kwa KUPIGANA mkwala ndio maana bado vita haijaanza?
  • Unafikiri kwa mkwala unaUAhamu ya vita?
  • Unataka kusema hata kama si wewe uliyesutwa au kupigwa mkwala, hujawahi kustukia ULIBURUDIKA kushuhudia hizi SANAA?

Tatizo la....
.... kuchimba MKWALA, ukikosea MSAMIATI ,flooo na kushindwa KUMTISHA mtu, mnaweza ishia KUPIGANA VITA.:-(

Swali:
  • Hivi kusutana na mkwala sio TAYARI vita?


Naacha!
NAWAZA TU Mheshimiwa!
Hebu twende Tanzania CNN wajadili miundo mbinu...

Au tu Mwanadada wa Kichaga NAKAAYA alonge---

DUH tubadili hali ya hewa kwa kumuachia Mystikal awaamrishe watu fulanni...-Shake ya ASS[tahadhari lugha chafu kama wewe ni msikilizaji wa maneno kama yule]

Tuesday, March 17, 2009

Nyolinyoli! NAKUIBIA halafu SIFUNGWI!

LIONE VILE!
Linajua nilikuwa masikini!


LIONE VILE!

Linajua nina mshahara mdogo na halioni ajabu ghafla nina nyumba na magari ya kifahari yangu naniliyo mnunulia hawala yangu!


LIONE VILE!
Halafu litanipigia kura tena!:-(


LIONE vile hasa hili Litanzania!

Bingwa la kunyoshea vidole wengine wajinga na kwa amani likiendeleza ujinga!:-(

LIONE VILE ZURIIII, halafu NALIIBIA!


Wako ,
MWANASIASA -KIONGOZI.

P.S.
Naomba kura YAKO!


Swali:
  • Inawezekana sikuongelei wewe?
  • Ghafla kutajirika kihalali katika nchi tajiri kama Tanzania si inawezekana?


Ngojea BOB MARLEY azungumzie kitu katika -Running Away

Katika SAYANSI ya KUKUBALIWA!

Si lazima uombe,....
.... lakini wahitaji KUHITAJI ili uvumiliwe na UKUBALIWE.

Unaweza kujichukulia kwa nguvu lakini,...
..... na watu wakaelewa baadaye kwanini ulijichukulia na UKAKUBALIWA.

Daima,...
....KUKUBALIWA kwako kunauhusiano na mahusiano yako ya MATAKWA yako na watu wengine.

La sivyo huhitaji KUKUBALIWA!

Na hata,...
.... katika taaluma ya kutongoza UNAHITAJi mtongozwa ili UKUBALIWE YAKO katika mtongozo.
Ila katika ,....
.. taaluma ya MAHUBIRI, ili YAKUBALIWE unahitaji kubobea kwa YASIYO YAKO UHUBIRIYO utakayo KUKUBALIWA.


Kumbuka,....

  • NI YAKO ya kutongozea UKUBALIWE!
  • NI YA WENGINE utumiayo KUHUBIRIA ukubaliwe!


Swali:
  • Katika KUKUBALIWA unafikiri wewe ni MTONGOZAJI au MHUBIRI?
Cha muhimu ni,...
.....kumbuka kukubali KUJIKUBALIA.

Wengi hata bila sababu za msingi hawata KUKUBALIA na kumbuka sababu yake kubwa ni kwamba HAWA JAMAA ni WATU bin BINADAMU.

Wasikilize lakini WAKIKUTONGOZA au KUKUHUBIRIA halafu kama unaroho nzuri WAKATALIE.

Swali:
  • AU?
  • AU unafikiri hujakubaliwa hata na MUNGU wa upendo?
NAACHA!
Tulia na Percy Sledge azungumzie jinsi mwanamme akipenda katika - When a man loves a Woman.

Iko UCHI!

Iko WAZIWAZI!
Haijafichwa!



F
unga macho UIKODOLEE macho!
Haijafichwa




Angalia halafu TAFSIRI!
Haijafichwa!



Ikivalishwa chupi iko mbele ya MACHO ya chupi!
Haijafichwa!



Iko wazi!
Haijafichwa!



Inamaana kinamna uko uchi!
Haifichiki!




Kumbuka hata kila nyani ana uchi!
Hajaficha!




Kwa MAAJABU kunaaringiaye wake uchi!
Kaficha!




Na pamoja na elimu dunia kuweka UJINGA uchi!
Inafichika!




Elimu bado yavalisha UJINGA chupi!
Imefichika!



Kama umeelimika ya uchi wayaona uchi?
Usifiche!

NIMEACHA!
Nawaza tu mkuu!
Swali:
  • Unakumbuka chini ya nguo uko uchi?


Tubadili hali ya hewa kwa kumsikiliza ASHANTI katika -Foolish


AU tubadili zaidi hali ya hewa kwa kuwasikiliza STILL COOL katika..-To be poor is a crime

Kwa wapenzi wa nyimbo za YESU au ajulikanaye PIA mtaani kama NABII ISSA!

A quick note to mention that this site allows you to download 5 worship songs now and get New Worship every single month (at No-Cost)

Simply click below to find out more:
uneditedworship.com

Blessings,
Maduhu


Asante Jumanne Maduhu!

Monday, March 16, 2009

JINSI ya kupotea KIMARIDADI!

Jifanye unajua uendapo KIMARIDADI!

Jifanye unajua usiyojua KIMARIDADI!

Dharau ushauriwayo na wanaojua KIMARIDADI!

JIFANYE!


POTEA!


SI wewe ni MARIDADI?

Labda nimepotea na wewe bado ni MARIDADI!

Au umepotea na niko kimya KIMARIDADI!


Maridadi profesa wa ya kupotea KIMARIDADI!:-(

MARIDADI!


---------------__________________------------------------

NIMEACHA na kumbuka NAWAZA tu hapa na siKU NJema!

Swali:
  • Unafikiri nimepotea?
  • Unauhakika hujapotea wee maridadi?

Bwana asifiwe!


Ngojea Nyerere azungumzie kitu.......kwa hisani ya SafiriSafari


Au tu Jimi Hendrix abadili mudi katika-All along the watch tower.

SAMAHANI!

LABDA nimekosea badala ya KUPATIA!:-(

KWA kufanya labda NINAHATIA!

KWA ujinga , werevu kiuno mauno HAKIJANIKATIKIA!


KWA ujinga naona NAPATIA!




KWA werevu wajua ni ujinga NINAPATIA!

NA kujitetea kwangu kwa ya ujinga ni HATIA!

NISAMEHE kama NINAHATIA!

INGAWA samahani yaweza geuka mazoea kwa mwenye HATIA!


SAMAHANI!


--------------______________________------------------------------


Swali:

  • Hivi unahitaji kufikiria jinsi ya kuomba msamaha kama unahatia?


Pumzika kwa kuangalia tofauti ya WANAWAKE na WENYEUUME.....



Au tu Teitur aimbe - Louis Louis

Sunday, March 15, 2009

SITAKI kufumba macho NISIJE kukuona uko UCHI bure!:-(

KATIKA...
... IMAJINESHENI za NCHI NZURI, unaweza kumuona MPAKA MWANAMKE mzuri wa KIAFGANISTANI mwenye USHUNGI na kusahau utajiri wake wa TITI KUBWA lenye CHUCHU PANA.


Na,...
.... kwa mpenda sana matako KUNA uwezekano asigundue UMEPAKA WANJA na unakucha ndefu kwenye vidole shujaa hata katika kushikilia NANIHII.:-(


Swali:

  • Unauhakika TANZANIA ni nzuri kuliko NAIROBI?
Na,...
....wakati tuko KIGOMA kumbuka ukifumba macho unaweza KUAMINI uko DAR-es-SALAAM.

Swali:

  • AU?

NIMEACHA!

Ngojea tupumzike kwa kumsikiliza TITI kutoka Senegal...


Au tu Koffi Olomide aongee kichina kwa waswahili wasiojua kifaransa katika...- Ultimatum

RAIS yupo USIJAMBE!

Labda,...
....HESHIMA ni kwenda KINYUME au nyuma na utakavyo kwenda mbele AU vya MBELE.

Ingawa,...
.... siongelei KIJAMBO cha mbele sasa hivi hapa ,...

...ILA....
kunauwezekano kuwa KWA heshima unajizuia kujamba kwa KUTUNZA heshima ya visivyo hitaji kuwa na UHUSIANO na NENO HESHIMA mbele KWA MBELE.


NI...
... aibu wakati VYA AIBU haionekani VINATIA aibu KWA sababu TU wenye HESHIMA NA AIBU wanavipa KIPAUMBELE visivyo stahili heshima KWA HESHIMA na aibu.

Swali:
  • AU?

  • Unauhakika unamheshimu RAIS wakati yeye pia anajamba AU huna uhakika labda sasa hivi kajamba kiheshima na SI aibu?
  • Unauhakika kujamba ni KITENDO au labda kuona aibu kwa kujamba HADHARANI au kisiri ndio KITENDO cha AIBU?

KWA heshima naacha hii topiki AMBAYO LABDA NI YA KIJINGA KAMA UNAUHAKIKA, ingawa labda haijanishinda BILA AIBU!


JUMATISA njema!

Hivi leo kunauwezekano sio jumamosi au ngojea nirudie kukuuliza kwa kisauti....





Au nikukumbushe TENA kawimbo...




Au tu...




Kuna adaio aliye kwenye PICHA kuwa nilikuwaPOA ZAIDI miaka fulani ILIYOPITA wakati wa picha hizi BAADA ya hii sentensi ya KIJINGA, ingawa najaribu kujitetea sijabadilika bado ingawa siku hizi ni kweli nataka kumpa mimba mtu kama kuna mwenye huruma bila kumpiga PICHA :-(










































































































































































































































































Ngojea I-Wayne anikumbushe katika - Cant SATISFY her


Au turudi tu tena nyumbani kwa ALI KIBA azungumzie- NAKSH naksh MREMBO...

Saturday, March 14, 2009

Jamani JAMANI shemeji KULA jamani![sentensi hii imebaniwa pua]:-(

Kabla WIFI hajala,.....

Swali:

  • Unakumbuka uwezekano wa asiye wako ni SHEMEJI yako?

Pamoja na ya NDUGU na JAMAA,...
.....labda.....
ni kweli binadamu wote ni NDUGU.


Kumbuka lakini kuwa WIFI haitwi wifi tu bila ukweli kuwa wamuitao wifi wanajua au kuhisi kuna kitu wasichoonja ANAKULA.



Na,...
....ni kweli SI lazima wakati
....SHEMEJI....
hajala, kuna ukweli SHEMEJI alitaka KULA.


Swali:

  • AU?

  • Unauhakika katika dunia ya leo ni kweli wifi ni MWANAMKE?

Nimeacha!
WikiENDI NJema!

Tupumzike kwa kuthibitishiwa kuwa RAIS KIBAKI ana mke mmoja.


Au tu Q-Tip na kundi zima la Tribe called Quest watuulize -Can i KICK IT

Au tu watukumbushe -We've got the JAZZ


Asanteni WADAU wote ambao hamkunitenga juzi ya jana ambao baadhi ni hawa katika picha nilizofanikiwa kuzidaka na kudakwa...



Photobucket



Photobucket

Photobucket


Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket



Photobucket


Photobucket

Photobucket



Photobucket


Photobucket


Photobucket




Photobucket



Photobucket


Photobucket


Photobucket


Photobucket


Photobucket



Photobucket


Photobucket


Photobucket

Photobucket



Photobucket

Photobucket



Photobucket


Photobucket


Photobucket


Photobucket


Photobucket


Photobucket

Photobucket

Papaa Aliko Mwakanjuki a.k.a Dj Altunes ASANTE!

Thursday, March 12, 2009

Pamoja na yote BADO mdomo unauhusiano na TOBO!:-(

Katika kurudia kuunganisha mahusiano ya vitu,....

labda......:-)...loves....:-(


...... sababu za kuweka MLENDA kwenye mdomo ni kulenga TUMBO na labda NIA ni kuufikisha tumboni , ingawa labda mdomo ni tobo la tumbo kama hujaziba TOBO.

Kinyeo pia ni USHAHIDI wakuwa TUMBO limetoboka, INGAWA unaweza kuendelea kubabaishwa na SIMULIZI za UTUMBO ukasahau uhusiano wa kinyeo na tumbo wakati tunazungumzia UMARIDADI wa KOO kabla ya TUMBO.

SIKUBISHII ukinibishia lakini!


Pamoja na yote,...
.....VITU karibu vyote vinauhusiano kama tu MIMI na WEWE ukiviangalia hata bila UMAKINI.

Swali:
  • Unakumbuka WEWE na MIMI tunahusiana?

Tatizo ni,...
.... katika vilivyotoboka, ni mpaka uwe na mtazamo au TABIA ya kuliangalia tobo na kuanza kufikiria uwezekano wa labda tobo LIMETOBOKA , iliKUGUNDUA labda si kweli kinyeo na mdomo vyote VIMETOBOKA katika huu uhusiano wa haya MAHUSIANO.:-(

Tatizo ni,...
....wakati unaulengesha mlenda kwenye TOBO la tumbo ,ni tatizo kama HUKUMBUKI kilengwacho na yote MARINGO na madahiro ya mlenda si tumbo bali AFYA YA MWILI.


NAACHA!
Kumbuka nawaza tu hapa na nakutakia kila la kheri chooni leo!

Siku Njema!


Swali:

  • Huwa unakumbuka kuangalia mahusiano ya UHUSIANO wa HIKI na KILE?
  • Unauhakika hujasoma ujinga PEKEE kama umefikia KUSOMA mpaka kwenye sentensi hii hasa kama HUWA huoni uhusiano wa ujinga na akili ?

Ngojea Manu Dibango abadilishe tena hali ya hewa katika-SOUL MAKOSSA

Au tu Manu Dibango alete za -Miss Cavasha

Katika KUTETEA SURA nzuri isiyo na CHUNUSI isiyokumbukwa SURA!

Kumbuka....
...... hata kinyeo kina SURA wakati unafikiria SURA.

Na kwa kuangalia picha kubwa unaweza usiione SURA YA CHUNUSI kwenye SURA.

Lakini,...
.... SURA yenye chunusi .....

.....BADO ....
INAchunusi HATA kama AJALIYE MADOGO kwenye USO haoni ndita za chunusi kwenye SURA.

Unaweza kutetea uso kwa kusisitizia udhaifu wa kudumu kwa CHUNUSI kwenye SURA lakini!:-(

Kumbuka tu kutosahau kuwa,....
.... CHUNUSI nayo ina SURA.

Na,...
.. uso mzuri labda ulikuwa na CHUNUSI yenye SURA NZURI tu!:-(

Swali:
  • Ushawahi kujiuliza ugumu wa kutunza chunusi ibakie usoni?
----------___________________-----------------------------------

Nimeacha!
Kumbuka nawaza tu!


Ngojea Naughty by Nature watukumbushe- OPP

Au tu Fresh Jumbe aturudishe nyumbani katika -AMA ZAKE AMA ZANGU

ANA macho, ngozi...na ulimi na KUKUPENDA kwa KUGUNA au MLIO!

Labda ni aibu KUKIRI,...
... udhaifu wa binadamu katika hisia mia ikiwa moja KASHIKILIA.


Labda ni aibu KUKIRI,...
.. kama mwenyemacho atumia dira ya mguno na kilio UKILIA.


Kwa maumivu au utamu katika KIKIRI,...
.....kakara maungo-tikisa na atahakiki ukiguna au KULIA.

Macho yanaona meno kama NGIRI,...
na ukikaa kimya hajui kapatia kama huguni au KULIA.


Ahitaji masikio kwa kuhakikisha yaonekanayo FIKIRI,...
... na wakati aonja kwa ngozi akiguna na KULIA.


Na mengi ya kuhudhunisha yapo FIKIRI,...
... na mengi wayaona ingawa wameacha kuguna na KULIA.


Labda bado watu wanahisia zote na watumia moja NAFIKIRI,...
....sababu za mengi ya kushoto bado yako kushoto na si KULIA.

Kama unagusa , kuonja,...na wasikia FIKIRI,...
.....wadhani si udhaifu ukitaka mpaka uone chozi ndio ujue mtu ANALIA?

-------------------------_________________________----------------------------


Nawaza tu USITISHIKE!
Swali:
  • Bado unafikiri unahitaji masikio uwenauhakika na unachoona kama macho yanaona?
  • Unafikiri unaona kwakua una macho na ulimi haukusaidii kuona kwa kuonja ukitaka kujua?


Naacha!
Namuachia Dr Alimantado katika -Best dressed chicken in town

Au tu Linton Kwesi Johnson azungumzie ya - Want Fi Goh Rave

Wednesday, March 11, 2009

MBOLEA!

Labda ukiinusa inanuka,...
..... na ukiilamba ni SUMU.


Mimea huhitajika,....
....kwa mbolea kujisikia ina maana na si SUMU.


Akili zako hazina mpango kama mbolea zisipotumika,...
.... kama hazitumiki kumea hata kama mmea hauhitaji SUMU.


Na kama UBONGO usiotumika,...
....mbolea isiyotumika ni SUMU.


Mbolea!

.....labda UKIINUSA inanuka,....
.......................na ukiilamba ni SUMU.

Hata kama inatumika,....
.....ukiizidisha bado ni SUMU:-(

-----------------------------------------________________--------------

Nawaza tu usitishike!

Siku Njema!

Tutulie na kazi za mwanamuziki nipendaye kazi zake tokea enzi za Tony Toni Tone, Lucy Pearl na hata akiwa solo kwa jina Raphael Saadiq.
Hapa nimuache Raphael Saadiq,akiwa na Ali Shaheed Muhammad na Dawn Robinson.
katika...kibao....-without U

Au tu niiache kazi yake nyingine akiwa katika Lucy Pearl , kibao cha akinadada kusutana- Don't Mess With My Man

LABDA kwa bahati nzuri WEWE ni MIMI!

Mimi sio wewe,...
... na yangu huyajui ingawa yangekupa KIWEWE.


Kuku sio Mwewe,...
.... na kicheche atakaye nundu anawezaishia kupata NGEWE.


Bado niko na wewe,...
.... ingawa hata kwa yangu tunafikiria ya WEWE.


Natulia kama wewe,...
...ingawa ninahasira na vurugu kama WEWE.


Nikichoka ninalala kama wewe,...
....ingawa ukilala ndotoni wasahau kuniona mimi ukijitazama WEWE.


Kumbuka pamoja na ujinga LABDA mimi ni wewe,...
...na yangu yaweza kuumiza yako WEWE.:-(


AU?
_______________________________-----------------_______________

Nawaza tu MKUU!
Ngojea Zhané waelezee matakwa katika - Hey Mr. D.J.


Au tu Manu DIBANGO azungumzie - Electric Africa

Tuesday, March 10, 2009

HALELUYAH labda MWANAMPOTEVU hajapotea!

Swali:

  • Kama dunia yenyewe imepotea si labda mwanampotevu anapatia kwa UDHANIAYO ni kupotea?
  • Kama dunia inapatia unafikiri una ndoto za mbinguni za nini?

BAADAYE!
Swali:
  • AU?

Monday, March 09, 2009

Kama UMESTUKIA unaweza na UNAJUA JINSI ya KUVUMILIA ukinyimwa na MALAYA!

WAKATI unaendelea KUVUMILIA wakati UMENYIMWA na MALAYA,....

.....bado....
AFRIKA inagawa kama malaya na kumnyima iliyomnyima liMTU kama ANYIMAVYO mtu MALAYA.


Labda,...
... AFRIKA ni BARA MALAYA ingawa kuna wanyimwao na MALAYA.


KATIKA.....
... KUVUMILIA ni bado unavumilia kwa kuwa ULITAKA na ukinyimwa ROHO INAUMA KWAKUWA ULITAKA ingawa uko katika uvumilivu na unafikiri imekuaje hunauhakika UTAPATA ya kawaida na unashangaa umenyimwa uliyofikiri ni YA UHAKIKA yake MALAYA.


Wakati UNAVUMILIA bado ni KWELI ulitaka kuifanya hata ambayo sio ya MALAYA ,na kunauwezekano unakumbuka au baada ya kunyimwa NDIO UMEKUMBUKA unaweza KUCHEUA mwenyewe na huhitaji MALAYA.

Swali:
  • Wakati unafikiria maendeleo umewahi kukumbuka kitu kiitwacho PUNYETO?

KAMA,...
.... unavumilia LABDA unafanya na uvumilivu WAKO NI DALILI za kubobea katika KUFANYA.

FANYA BASI!
Swali:
  • AU?
  • AU unanisubiri MIMI nifanye?

NA ni KWELI,...
.... mambo ya MALAYA MTAMU anajua aliyeonja na kula MALAYA.


NA,...
.... wengi waongeleao, KUPIGA KELELE au KUMZUNGUMZIA malaya,hawamjui MALAYA
Swali:
  • AU?
  • Kama AFRIKA ni demu mwenye chunusi unafikiri unge mtoa chunusi kwa kubinya chunusi au kwa kumsifia anachunusi ujualo halidumu kwenye uso mzuri?


NAACHA!


Ngojea nimuache rafiki yangu Papaa Kweba ofisini!Kweba eeh, unanitenga lakini!Tuko pamoja na salamu lukuki!
























Ngojea TONY HENRY alete tena muziki aina ya opera katika- NOW we are FREE.



Au ngojea TONY HENRY wa RNB alete za- Redemption Song


DUH!!
Basi tupate tu ZUKE kutoka kwa Jacob Devariux na wenzake...


Sunday, March 08, 2009

GHAFLA MTOTO kagundua kaota MAVUZI!

GHAFLA mtoto ushahidi anao KAKUA,...
... na aweza kudhani ni wakati wakumbishia mvuvi UVUVI, kakua.



CHUCHU imenenepa KAKUA,...
... na aweza sahau walio na mvi chini ya kalikiti bado WANAMVI na walikua.


NI safari KUKUA,...
.... inataka muda kukua na ya miaka yataka miaka hata vile kama hutaki vile HIVI, utakua.

KUA mwanawane KUA,...
.... kama na una mavuzi usiwe na wasiwasi, SUBIRI yatapata MVI mavuzi ukikua hata bila MVI ukikua.

Ingawa mvi si kukua,...
....labda wahitaji ujue wapi pamenyolewa ingawa ni kipara UGUSACHO na unadhani hakina MVI hujakua.

--------------------------------------------------------------------

NAACHA!
Swali:
  • AU?
  • Unauhakika umekua?
  • Unauhakika unajua?
Twende tena SENEGAL kupata- bes bi sa bessa katika miondoko ya muziki aina ya Mbalakh




Au tu Gregory Isaacs katika - Rough Neck

Saturday, March 07, 2009

Nimewahi KUONA mtu MWEUSI , na LABDA SIJAWAHI kumuona mtu MWEUPE!

Labda,...
....unapenda rangi ya JIPU LIKIIVA au tu rangi ya NUNDU kesho yake baada ya kupewa NUNDU.

Na,...
.... inawezekana WEWE ni MBAGUZI kama unauhakika wa MAANA YA UBAGUZI ni nini.:-(

Swali:

  • Kama unajua RANGI , kwa kawaida unazungumzia RANGI GANI nyeupe ya MTU kama katika SIMULIZI zako za karatasi JEUPE unazungumzia NYEUPE?
  • Ushawahi kuona mtu BILA rangi wakati unaangalia mavuzi au masharubu CHOMACHOMA ya MTU?[Samahani kama jina la nywelenywele nyingine inawezekana ni matusi.:-(]
Lakini,..
.....katika kuona KIBOGOYO unaweza kukumbuka MENO na ukajifanya ni kawaida yako kupiga MSWAKI wakati meno yako yameoza na yana rangi ya DHAHABU -MAVI.

Swali:
  • AU?

Na,..
... wakati unaona RANGI YA BLUU BAHARINI,ni KWELI inawezekana ukasahau BAHARI HAINA RANGI BLUU na uonacho BAHARINI ni rangi ya anga la BLUU.:-(

Swali:
  • Kama wewe ni MTANZANIA unauhakika MZUNGU na ALBINO wanatofauti YA uweupe wa rangi wakati kwako MAALBINO ndio DILI?
  • Unauhakika unajua JINA la rangi yako?

NAACHA!

Ngojea tutulie kwa kwenda CHINA kushuhudia mwanamama AKILIA kwa kuchelewa ndege......


Au TYRA Banks anisaidie kwa kujishebedua katika-Shake YA body

Au tu Whitney Huston arudishe UMAHIRI ingawa ni UONGO katika - I will always LOVE U

Friday, March 06, 2009

HESHIMU MAFISADI kama ni UAFRIKA kuheshimu WAKUBWA!

Labda,...
.... WAAFRIKA TUNAHESHIMA mpaka TUKATAWALIWA.:-(


HESHIMA ni kitu cha bure na labda ndio maana inasemekana WAAFRIKA wanaheshima sana kutokana na ukweli kuwa heshima ni BEI CHEE , kama hukiri kuwa ni BURE, mpaka kwa heshima tunategemea vya BURE na kwa heshima ni MASIKINI kwenye UTAJIRI.



Na,...
.... ukisema WAFRIKA wanaheshima sana hasa KWA WENGINE kuliko WAJIHESHIMUVYO WAO, .....

.... naweza kushindwa KUKUBISHIA wakati NIMESHUHUDIA kuanzia WATU mpaka DINI ZA KIAFRIKA wasivyo na zisivyoheshimiwa na WAAFRIKA, na watafiti mpaka wa guenea worms wazinguao Waafrika wako au wanatoka UGHAIBUNI.

Labda ni kweli,...
....SIKU HIZI kuna wataalamu kutoka nje wa mambo ya AFRIKA wakati Waafrika tuko mstari wa mbele katika imani na tafiti za wengine kwa ajili ya WENGINE!:-(


Swali:
  • Hivi si HIP HOP ni bomba kuliko MDUMANGE, Mdundiko, CHAKACHA na TAARABU kwa pamoja?

  • Hivi unauhakika Taarabu na Mlimani park JAZZ BANDI ,ni miziki ya Kiafrika?

  • Hivi WAAFRIKA pamoja na kuuana unauhakika wana na wali-KUWA na HESHIMA?

Turudi katika hoja,.....

Wakati unataka KULETA ZA KULETA za kuwalaumu mafisadi wajanja MTOTO WEYE, kumbuka KIAFRIKA tokea enzi hizo TUNAHESHIMU WAKUBWA na tulitawaliwa salama SALIMINI kwa heshima.


HESHIMU wakubwa weye usije laanika bure wakati unajua kwa kuwa masikini ni rahisi zaidi kwenda mbinguni kuliko tajiri kupenya katika tundu la sindano, na ukikosa heshima UTALAANIKA.

Swali

  • AU?

  • Hivi unauhakika UKIHESHIMU utaheshimika hata na waheshimiwa wasiojua heshima ni nini?

  • Hivi unatofautisha kuogopwa na kuheshimiwa?


Nauhakika tu,...
... wakati WAAFRIKA kwa heshima TUNALALAMIKA, kwa kulala TUNATENDA na matunda yanaonekana katika mkao wa kuendelea kuujaza ulimwengu kwa KUJIFUNGUA akina totoz zenye majina kama MIKAELA na MIKA hata kwa Kihindu, Kiislamu na Kigagagigikoko .

MUNGU IBARIKI AFRIKA!

Au kama na nyie MIUNGU mpo na mna BARAKA kinamna , BARIKINI BASI AFRIKA na WAAFRIKA kama mbarikivyo wengine na acheni NOMA!

AAAGH!

NAACHA!
Kumbuka nawaza tu hapa MKUU na labda sitendi!:-(
wiKIENdi njEma!

Tulia na YERBA BUENA katika- Guajira

NEPI mwanzo na nepi MWISHO!

UKIZALIWA unaweza kubahatika kuanza na NEPI au tu lichupi la kanga , shuka au kitenge, kama si linguo tu lililochanwa katika kaptura ya kaka,......

..... katika jitihada za WALEZI kukusitiri TOTO ZURI wakati unajinyea na kujikojole kwa utoto.


Kwa UJANJA na BAHATI unaweza kukwepa kuaga dunia MAPEMA mpaka ikafikia WALEZI kukusitiri kwa NEPI au tu chupi ya kanga, shuka,.... au kitenge , ZEE ZURI usitirike wakati unajinyea na kujikojolea kwa kusahau ya choo kwa uzee.


MAMBO YOTE ni NEPI kulia-nepi KUSHOTO katika dansi hili kama unabahati katika wimbo huu na sebene hili la MAISHA.


TUNAKUMBUSHANA TU na hatutishani!

Swali:
  • AU?
  • Bado unauhakika unataka kuishi sana ?
  • Au unamuogopa Mungu nini ndio maana hutaki kuanza mapema?

Tuendelee na ya CUBA kama CELIA CRUZ adaivyo katika - OYE COMO VA


AU tu CELIA CRUZ amalizie kwa -Azuca Medley

Natafuta SHUGA MAMA mdogo-MKUBWA ninywee BILAURI ya kwenye GLASI!

Mama SUKARI ,...
...lete ASALI!



MAMA tamutamu mwenye ASKARI,...
.....najua ushapitia na unajua machungu, tufurahi kwa kuonja ACHALI.



NATAFUTA ya futari,...
... wajua kwa AFUNGAE tamu si pekee ASALI.



WENYE kelele wanatafuta GARI,....
.... mie nitaridhika na mzoefu wa kubinuka akinipa hata kwa kulala CHALI.



WADOGO wasio shuga mama kwenye sinia kubwa la KACHUMBARI,...
...wanajiamini kwa kisimi kikubwa MADHABAHUNI na kufikiri sala zitafika kwakua TUNASALI.



WAZEE walio shuga mama kwenye SAFARI,...
...kutoka Nairobi kwenda HUNGARY, naogopa twawezaishia MALI.



NA magugu ni kitanda cha NGIRI,...
....na kwa ajuaye ajua meno kama ngiri , kwa ngiri ni urembo kama BANGILI.



SHUGA mama mzoefu wa alichokula JUMA na alacho BAKARI,....
.... nimatumaini yangu utanilisha cha Serina , Asha , Rose kwa uzoefu wakati ukinijulia HALI.



SHUGA mama ukinifikisha usije shangaa nikitaka kutoa MAHARI,....
.... unajua safari zetu siku hizi hata kwa TREKTA bado matope mengi na hatufiki MBALI.



Ni kweli kama tamu nitataka yote KACHUMBARI,...
..... katika uadimu wa nyanya ndogo ZENYE MAKUBWA ,zikifikia mzani nisamehe kwa ULAFI katika hii HALI.

------------------------------------------------------------------------------------

Nimeacha!
NAWAZA tu MKUU!

Swali:
  • Ushawahi kukutana na adaiye ana uzoefu wa siasa wakati hapatii siasa?
  • Ushawahi kukutana na shuga mama asiye mzoefu?



Turudi tena CUBA kwa Buena Vista Social Club katika kitu - Chan Chan

Thursday, March 05, 2009

STIGMA na DOGMA!

Unaweza kuogopa kuanguka hadharani kwa kuogopa STIGMA iambatanayo na KIFAFA ukianguka badala ya kuogopa MAUMIVU ya kuanguka , wakati kuanguka ni kawaida hasa kama umewahi kusimama au kutembea, ingawa kama WEWE ni mjanja , inawezekana ulishawahi kuanguka wakati umelala.

DOGMA zaweza kukusababishia usijiulize uwezekano wa uwepo wa MUNGU WENGI au SHETANI WENGI kutokana na kuaminishwa kuwa kuna ukweli mmoja na ukweli wenyewe ni kwamba kuna MUNGU MMOJA mzuri na SHETANI MMOJA mwenye sura mbaya.



Labda,...

  • kuna ambaye hafanyi kitu ingawa kinafanyika kwa kuogopa STIGMA.

  • HAKIPINGIKI kitu ingawa kinapingika kwa sababu ya DOGMA.


Labda,...
  • DOGMA ni kukana MACHALE yako!
  • STIGMA ni kuogopa yako TAFSIRI ya machale yako , kwa sababu jamii inatafsiri na kuoanisha tafsiri na kitu .Kitu uofiacho kinakuathiri!


Dosari za stigma ni pale wewe mwenyewe utakapofikia kuamini waaminiyo kuwa ni dosari hata visivyo na dosari kwa sababu kuna stigma iliyojengeka katika jamii hata kama ni ya kuoanisha kula sana na ulafi hata kama kazi yako ni mgonga kokoto na umbo lako ni kubwa kuliko, na sahani kubwa inakuja na hali halisi na si kwa ulafi kwako .

Dosari za DOGMA ni ukweli kuwa ni mtu mwingine yalimshinda kuelewa na kuelezea KWA NINI, na kaamua kuwa HIYO iwe ndio kweli tupu kwa wengine wote na USIBISHE.

Labda,...
.... katika kulainisha mambo ya STIGMA unaweza kuunganisha na ya jamii ya KiTZ ya kama labda :

  • Ukibana matumizi na kama wewe ni MPARE kama mimi, watu wataendelea kufikiri wewe ni BAHIRI kwa sababu Wapare wana STIGMA ya ubahiri.

  • Hata kama wewe tajiri , ukiomba halafu ikajulikana wewe ni MGOGO, watu wataamini kuomba kwako kuko kwenye damu kwa sababu kuna waaminio ombaomba ni Wagogo.

  • Ukiiba kama wewe MCHAGA kama watani zangu, kuna watakaodhani unatunza na kudumisha MILA na DESTURI kutokana na STIGMA iwalengeshayo Wachaga na wizi.

  • Tukipenda ngono kama WEWE halafu ikawa sisi ni Wahaya , LABDA kuna....
  • Nakadhalika tatu katika stigma na....


Na maswala ya DOGMA yanaweza yakakuchanganya hasa katika mambo ya dini ambapo usipoangalia utashindwa kuelewa akusimuliaye kuna MUNGU MMOJA lakini hapo hapo kuna Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu roho Mtakatifu , wakati unamsikiliza adaiye yeye kapatia kwa kuamini kuna MUNGU MMOJA na SHETANI MMOJA katika ya Mungu mengi na ya Shetani lukuki.

Swali:

  • AU?
  • Kwani STIGMA ni mpaka iwe ya UKIMWI au UKOMA mtaani na DOGMA aamue PAPA wa Kiroma VATICAN?

Katika STIGMA labda kunamchango wako kama unasaidia kuamini kuwa kuna dosari ambazo zinamng'ang'ania mtu daima na kwa mahesabu yaleyale uliosimuliwa ni MAHESABU ambayo ukitekenya lazima yazae DOSARI.

Katika DOGMA , sema unataka tu kurahisisha ili kujisaidia usijishughulishe kuelewa tofauti.

Swali:
  • AU?


STIGMA na DOGMA
DOGMA na STIGMA
......na labda vyote ni UJINGA.:-(

NAACHA!
KUMBUKA NINAWAZA tu hapa!
Nakutakia mafanikio MEMA NA MAKUBWA chooni leo!


Tutulie na Dave Chappelle alete busara za kukojoa katika- Piss On You


Au DAVE Chapelle aendelee katika- NIGGAR FAMILLY


AU tu Burning Spear a kumbuke katika -Days of Slavery

TUKANA katika staili ya kujaribu KUEPUSHA usistukiwe huna HOJA!:-(

Kama unajulia , kuna ambao HAWATASTUKIA!

Na,..
... kama unajua kutoa HOJA wakati UNAHASIRA, basi wewe BINGWA.



UKIKASIRIKA usipoangalia BADALA ya kueleza unaweza kujikuta UNAJIELEZEA.

Swali:

  • Ushawahi KUJISIKIA kutukana kwa kukosa NGUVU ya hoja?
  • Hivi tusi sio HOJA?


HONGERA!


Naacha!
Nipo lakini!:-(
Photobucket
Au ngojea nijaribu tena kusema....


Au tu Eddy Grant azungumzie - Killer On The Rampage

Tuesday, March 03, 2009

Labda UNAONJEKA!

Kuna watakaodai ukila si lazima uonje kama ladha hakuna, kama tu watakaodai shughuli ya leo muhimu ya viumbe ni kubugia ili kuishi hata kama kiumbe KINA kionjea ladha.

SIKUBISHII!!

NA,..
... wakati unajiandaa kujitetea kuwa huonjeki, WAULIZE minyoo na mafinyofinyo makaburini ni watu wangapi wameshawaONJA!:-(

Katika safari ya kumalizia safari ya umeumbwa kwa udongo na utarudi kwa udongoni , LABDA ni lazima uonjeke ili ugeuke udongo.:-(

Swali:

  • Hivi busara za majeneza ya chuma kama sio almasi kwenye kaburi la sementi si nikumuingilia Mungu na vipingamizi katika kuhakikisha alivyokuumba kwa udongo usirudi kuwa udongo?
  • Unakumbuka kama huna dhambi na ukafa bila kuwahi kufanya dhambi na kwenda mbinguni ,labda si utaanza kujiuliza utamu wa dhambi ulikuwa ni nini?

Wakati unadai huonjwi , usiende kwa daktari asije akahakikisha uogopacho kwa kusema kuna virusi na bakiteria vinavyokuonja sasa hivi hata kama hujisikii kuumwa leo kama jana!:-(

SAMAHANI KAMA ninakukwaza ingawa naamini kama unadini fulani kuna uwezekano ukatubu na kujisikia vizuri.
Swali:
AU?
Si dini ni za kuwasikilizisha watu VIBAYA au VIZURI kutokana na mahitaji ya mfuata dini?

SIku njeMA!


Namuachia Nusrat Fateh Ali Khan atupe muziki aina ya QAWWALI katika - Improvisation..

Au tu NIN na mshairi SAUL WILLIAMS wazungumzie- List of Demands

MKE mmoja, MME mmoja NA matamanio MAWILI na nusu!

Mke mmoja, Mume mmoja MTAMU!

.....Wakati ananoga,....
kikunogeacho hakiongezeki utamu UKINOGEWA.



Mume mmoja, Mke mmoja MTAMU!
.... Akiacha kunoga,....
kikunogeacho bado kitamu ingawa MWANABIBI kaacha kuonja na chakulambia,
......kama alivyokuwa akionja wakati tamu AKINOGEWA.



Mke mmoja, Mume mmoja hakuna UTAMU!
---Hakikuwepo kinachonoga...
hakikuwepo katika mhusika tokea mwanzo, ingawa MABURUKI adai
......kilikuwepo na utamu ALINOGEWA.



Mume mmoja, Mke mmoja vuguvugu UTAMU!
.....Mapungufu ya kunoga ....
ingawa Mme yupo na Mke yupo na bado mawazoni ni KITU- FANTASI ya mhusika wa tatu,
....kitu kikusogezeacho utamu UKINOGEWA.



Mke mmoja , Mme mmoja.
Mme mmoja , Mke mmoja.
.... Mawazoni una watu wangapi?



Mtu mmoja na Limchumba moja ndani ya UTAMU!
... Utamu wa wawili ukinoga,....
jumla ya utamu bado ni elfu tano
,
... na LABDA ndoa bado zipo hata mmoja USIPONOGEWA.

-------------------------------------------------------------------------------------

NAACHA!
Kumbuka nawaza tu na usitishike usiponielewa ingawa labda kuna watakao nielewa naongea nini kinamna!:-(

Swali
  • Hivi mpenzi wako UBWABWA ni mzuri na anakaribia kufanana na yule umpendaye AKILINI-MUKICHWA au katika fantasi za WALI?
  • Hivi unauhakika ndoa ni zaidi ya neno ndoa wakati bado MWILI WAKO uko kwenye ndoa na MAWAZO YAKO yameacha MWILI na YANAJARIBU ndoa IENDELEE kufanana na uaminicho ni ndoa?
  • Mke mmoja Wanaume sita si ni NDOA kama ilivyo kwa Mume mmoja Wanawake ishirini na nusu?
  • Hivi mchumba ni mtu?

Samahani naenda kukojoa!:-(
Baadaye!
Ngojea Teddy Pendergrass azungumzie - My Greatest Inspiration


Au turudi tu tena Ethiopia kukutana na TEDDY AFRO atulize mshawasha akisema- JAH

Monday, March 02, 2009

Watu WEUSI wadhaniapo MWENYE ROHO MBAYA ana ROHO NYEUSI!

Kuna WATU WEUSI wafikiriao na KUAMINI rangi nyeusi ni ishara ya kitu kibaya kama tu wabaguzi wa watu weusi wajaribuvyo kuwaaminisha watu kuwa MTU MWEUSI ana kasoro na ni MTU MBAYA.
Swali:

  • Si umecheki walivyofanikiwa eeh?

Unaweza mpaka kuwasikitikia WATU WEUSI ambao wanadiriki mpaka kutamka kuwa RANGI NYEUSI nishai na ni rangi ya mavi kwa mapungufu yao ya kugundua kuwa mavi yana utajiri wa rangi nyingi.


RANGI na MAANA ZAKE hutofautiana karibu kila mahali.Kuna nchi rangi nyekundu ni mbaya na inaashiria maovu wakati katika jamii nyingine rangi hiyohiyo ina ashiria MAFANIKIO.
Swali :
  • Samahani kwakukuuliza; lakini hivi unafikiri tokea uzaliwe mpaka leo umefanikisha vinyesi vya rangi aina ngapi?

Tukirudi kwenye hoja........,

Kuna watakao sifia suti NYEUSI kama tu Benzi JEUSI kuwa zina rangi ya heshima na mafanikio, wakati wakikataa kuitwa WEUSI kwa sababu za;

  • Weusi
  • Giza, Usiku, -Maana yake huoni vizuri.
  • Mtu mweusi ,-maana yake si mweupe.
  • Nguvu za giza, nyeusi ,- maana yake ni za shetani.

na..
...nakadhalika tatu na nusu, ya kitu kilichowatoa kujiamini kwa kuwa WEUSI .

Swali:
  • Umeshastukia KIDUME mpenda ngono hupenda kuiingiza kitu sehemu za giza asizoziona vizuri kwa furaha na hahitaji tochi?

  • Hujawahi kugundua nguvu waziitazo za GIZA hufanyika zaidi MCHANA kwenye mwanga?

  • Bado unaamini shetani ni mweusi na JINI ni mweupe?

Kumbuka SIRI ya DUA la KUKU kutompata MWEWE ni ukweli Mwewe hana imani na hajui kalaaniwa na KUKU.

WAKATI Mtu MWEUSI.....
.... anaamini UWEUSI ni LAANA , labda kwa AAMINIYE inakuwa kweli LAANA.

Cha kufurahisha,...
.... tupo ambao tunajua kuwa kuna ulaini pia uletwao na kuwa MWEUSI.

Cha kusikitisha ni,...
.... WAPO waaminio kuwa kwa kuwa WEUSI wamelaaniwa na watakao tumia mpaka vitabu kama BIBLIA kuhalalisha.:-(
Swali:
  • Kama hakuna aliyewahi kuona ROHO, WEWE kakuambia nani kuna WENYE roho NYEUPE au ya RANGI ya MAVI?

NAACHA!
Siku Njema!

Tubakie Mozambique kwa André Cabaço ...



Au twende tena Cape Verde tukapate- Music Mix...

TULIA!

Kuna UWEZEKANO kabisa......
...... ukitulia kisaikolojia UTASIKILIZIA vizuri.

UKITULIA utakuwa na uwezo zaidi wa kufuatilia hatua za utamu ZIKUSOGELEAVYO kabla ya KUSIKILIZIA ingawa unajua unaonja nini.

Kama hujui uonjacho,...
....UKIKUZA sana TEGEMEO la UKUBWA wa paja la utamu wakati hujui utamu wa bata na hukuona BATA aliyechinjwa, unaweza usiridhike na KAPAJA ka kuku utakakopata ingawa bado kuku ni MTAMU.

Labda Kisaikolojia,...
... ukiamini itauma au itaumiza kunauwezekano ikawa CHUNGU au usifaidi utamu wakati uonjacho ni kitamu kwa kuwa unahofia labda ni kona ya pili yenye UCHUNGU ingawa MASAJI upewayo ni FULU UTAMU kona hii.
Swali:

  • AU?

Naacha!
Twende Mozambique ukutane na GITO....

Sunday, March 01, 2009

Wakati tunaendelea KUKATAZA wanawake WASITAHIRIWE au KU-ze-KUKEKETWA!

Nashauri,...
..... tuendelee kupinga mkeketo wa NANIHII kutokana na madhara ya KIAFYA, Kisaikolojia na hata ya KIKUJINOMA.

Tukumbuke tu!
......Ukichomoa uwe na CHA kuingiza kama hutaki kishimo kibakie kitupu.

Kumbuka,...
...hata kama unataka kuacha POMBE, jiandae kuwa na KITU kingine kitakacho CHUCHUMAA pale ULEVI ulipokuwa unachuchumaa , la sivyo utarudia POMBE a.k.a KILAJI tu, kama umeacha tu na KIU ipo tu na haina tiba tofauti ijaziayo palipoachwa na KILAJI.

Kumbuka pia moja ya kiwafanyacho watu waende KISIMANI ni kwa sababu za kuishi katika mazingira yenye KISIMA la sivyo kama katika mazingira kungekua hakuna KISIMA , labda tungeweza kwenda NAO kuvizia mademu bombani.
Swali:

  • AU?
Kwa hiyo wakati unaacha au kuachisha, jiandae au ANDAA vilevile MAZINGIRA yasaidiayo ari mpya na nguvu mpya ya MUACHO . Na kama nia yako ni KUOKOKA na KUACHA POMBE , labda kwepa walevi na jichanganye na WALOKOLE, ingawa labda kama unajiamini , unaweza kuwa Mlokole wa Kikristu ujichanganyaye na waislamu na kuzawadiwa KUJUA zaidi ulokole na UISLAMU.
Swali:

  • AU?
  • Si sehemu watumiayo kisima , watu wanaweza kuridhika na bomba la maji kama tatizo ni MAJI?
Kuna waliofanikiwa kuondoa JANDO na UNYAGO bila kuwa na elimu nyingine imfunzayo KIGOLI shughuli na KIDUME aliye balehe KUSHUGHULIKA , matokeo yake SHUGHULI NA NDOA zinashindikana na tunalaumu TV na MAISHA MAGUMU , ingawa pia siku hizi KUNA wajanja wanafikiri somo litolewalo na SOMO linatosha kufunzwa kwa siku moja kwenye KICHENI PATI .

Somo lililohitaji MKUFUNZI ahakikishe MWANAWANI anapitia UCHUNGU na UTAMU, siku hizi lina WAKUFUNZI wasisitiziao UTAMU TU na ni kwa siku moja, kwa kuandaa LIMTU kwenye maisha yenye MACHUNGU labda zaidi ya utamu.

NI muhimu UKISHACHOMOA , ingiza kama unataka mchezo uendelee.
Swali:
  • Unafikiri madhumuni ya maumivu ya Kidume kukatwa jando bila ganzi yanatimizwa na Kidume akikatwa maeneo na ganzi hospitalini?
  • Hivi madhumuni ya JKT ilikuwa nikuwatesa vijana Tanzania?

NA ,..
..... ni muhimu kabla HUJATOA na unajua kuna madhara ya KISHIMO kubakia kitupu, UJUE utaingiza nini katika kujazia.

SI lazima kama ukitoa SEMENTI , ukijazia UDONGO utakuwa umedhoofisha UMADHUBUTI wa KISHIMO. Labda SEMENTI ilikuwa inaumiza tu KISHIMO na kujazia kishimo KWA unga wa ULEZI ndio ilikuwa na NI dawa ya NYUFA.

Swali:
  • AU?


Kumbuka,...
.... wakeketaji walikuwa na sababu zao na jaribu kuzijua kabla ya KUTOA na kujikuta hauna cha KUINGIZA, au tu kujikuta kuwa kutokana na kutokujua PICHA NZIMA unashindwa kutetea hoja zako za KUCHOMOA hata kama una cha KUINGIZA.
Swali:
  • Hivi ukijua ni lazima uchomoe na hujui cha kuingiza, uiachie MUMOMUMO nini?
  • Kwani ukiacha ya SHETANI ni lazima ufuate ya MUNGU?

Naacha!
Topiki IMENISHINDA:-(
Tuendelee kuwepo South Africa kwa Busi Mhlongo katika- Urbanzulu


Au tu twende PANAMA kukutana na KAFU BANTON enzi hizo kabla watu hawajastukia Reggaeton katika - EL MAD MAN

Wakati KUNA vitu JAMII INAENDELEA kuamua ni MWIKO KUVIONGELEA kama tu KUCHEZEA mavi!

Ni kweli,...
.....CHA AJABU ni kwamba jamiii imeamua kukataa mambo fulani yasiongelewe.

Lakini,.....
......MAMBO yanaendelea KUFANYIKA katika jamii ingawa hatutakiwi KUYAONGELEA.

Tatizo ni,....
.... jamii na JAMII hutofautiana na MIIKO ya jamii moja ni ruksa katika jamii nyingine.

Wakati jamii moja ni mwiko adhabu ya KIFO, nyingine kifo ni jambo la kawaida na KAMA WEWE MWANAFUNZI ukiandamana, hukawii kupigwa virungu na ukifa poa tu.

Na,...
....kuna JAMII ziaminizo ni mwiko kula kwa mkono kama tu waaminio kula kunahitaji KIJIKO, UMMA na KISU.

Swali:

  • Hivi JAMII ndio akina nani kama wewe hauhusiki?
  • Si labda KUTAWAZA msalani ni kuchezea mavi ingawa ni mwiko kuwa na huo MTAZAMO katika JAMII?

Miiko NI KIBOKO na inaweza kumfanya MUISLAMU ajifanye MLOKOLE kama jamii ni ya KILOKOLE.

Na,....
..... MWANAKIJIJI anaweza kufikiri ni lazima ajifanye ni MTOTO wa MJINI kama anahisi kuna MIIKO inayomkumbusha kuwa hayuko KIJIJINI kama tu Msenge ajaribuvyo kujifanya basha maeneo mengine.

WAKATI katika jamii MIIKO inaweza kumfanya MKATOLIKI ASIKIRI kaokoka, MLOKOLE anaweza akamkana YESU katika kusawazisha ya KIDUNIA kama ya KUOPOA NGOMA.

Labda,...
.... sababu za MENGI kutoongelewa ni fikra kuwa:
  • SI heshima KUNONG'ONEZA
  • SI busara KUONGELEA
  • NI aibu KUSEMA
  • NI matusi KUSIKIKA

AU
....LABDA hatuna uhakika na MAANA ya UYASEMAYO nayanachangiaje katika MUONEKANO WAO katika JAMII hata zaidi ya MUONEKANO WAKO.


Tatizo ni,....
...... ukichukua muda kufikiria ni kwa nini jamii INAMTISHA mwanaJAMII , unaweza kugundua ni kwa sababu MWANAJAMII HUTISHIKA.

Swali:
  • Unakumbuka lakini kuwa hata ukianguka sokoni kwenye UMATI wa watu , ni asilimia ndogo sana tu ya watu inayoweza kushuhudia UMEANGUKA au hata kukumbuka ULIPIGA chini?

  • Ushawahi kusikia AIBU kwa afanyayo MTU mwingine wakati hakuhusu na afanyayo HAYAKUHUSU?
  • Kwanini?

  • Ushawahi KUJIPENDEKEZA kwenye sifa za MWINGINE hata kwa kudai unauhusiano naye au mnatoka kijiji kimoja wakati HAKUHUSU na yake HAYAKUHUSU?

NAJUA baadhi ya niandikayo hapa kijiweni KUNA waaminiyo hayafai kwa kubwa zima KUONGELEA.

Lakini narudia,....
.... JAMII zina TOFAUTIANA kutokana na wanajamii KUTOFAUTIANA.
......JAMIII zinaendelea KUTOFAUTIANA kutokana na WANAJAMII kuendelea kutofautiana.


Na,....
......JAMII zilizotofauti ZINAENDELEA kuungana hasa kwa jinsi DUNIA inavyozidi kugeuka KIJIJI.

Usishangae kupigwa BUTWAA kila kukicha kwa kushuhudia MIIKO ikivunjwa kuanzia kwenye TV yako sebuleni mpaka kwenye uchochoro wa pembeni ya KANISA lako , MSIKITI wako , SINAGOGI lako au PALE uchochoroni, pale kati ya BAFU na CHOO chako.

Lakini,...
.... MIIKO ni gundi ya jamii na kama unavunja MIIKO kaa katika mkao wakujua kuwa BINADAMU ni king'ang'anizi wa MIIKO aliyoizoea imfanyayo aamini ANAELEWA na KUJIELEWA.

UKIVUNJA miiko unaweza ukawa ni tishio katika JAMII na BINADAMU kama MBWA KOKO , si kila mara ukimtisha anakimbia.

Mara nyingine BINADAMU kama MBWAKOKO ukimtisha akajisikia unamuweka kwenye KONA , anaweza kukung'ata MAENEO kama MJUSI tu.

Swali:

  • LEO umekwepa KUONGELEA mangapi kwa kuhofia JAMII itakuelewaje?
  • SI unakumbuka JAMII inaweza kuwa MAMA, Baba, DADA, Kaka, Mchumba, Kimada, Rafiki wa Mpenzi wako utamaniye KUMKONYEZA,.....na WEWE?


Tukumbuke tu LABDA,...
.....katika JAMII kuna wakwepao NYAMA YA NGURUWE na kula YA MBWA, kama tu ambavyo wapo wakwepao NYAMA YA MBWA na kula YA POPO . Na hata kama mambo yote ni MCHICHA , mwiko wako wa kula PEREGE labda haumuhusu mwenye mwiko wa kula SATO kwa CHUNGA.

SHIKILIA yako yenye MAANA kwako, YA wengine kama hayakuathiri wewe WAACHIE wenyewe WAHUSIKA hata kama yaletayo maana kwa WAHUSIKA ni KUCHEZEA mikojo.

Swali:
  • Miiko ya Mkatoliki Itali unafikiri inafanana na MIIKO ya Mkatoliki TANGA?
  • Miiko ya MUISLAMU Yemeni unafikiri inafanana na MIIKO ya Muislamu KAGERA?
  • HIVI miiko yako SEBULENI inafanana na ya CHUMBANI?
  • Hivi DINI yako sio KIONGEZO cha mkusanyiko wa MIIKO yako na labda SI lazima wengine IWAHUSU?


NAACHA MAHUBIRI!
Topiki imenishinda!:-(

Twende South Africa kuangalia somo katika -Music and apartheid in South Africa


Au tu huko huko South Afrika , Black Mambazo & PJ Powers wazungumzie -Knocking on Heaven's Door