Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Jicho katika MAISHA YA BINADAMU kama tukichukulia kuwa NI KWELI kwa mara ya kwanza UASHERATI sio MTAMU.:-(

>> Thursday, September 09, 2010

Unaweza kusoma safari ya kunogewa kwa BINADAMU,...

.... kwa kumuhoji MLEVI WA BIA na kustukia kuwa KWA MARA YA KWANZA kuonja bia,BIA  kwake haikuwa TAMU



Unaweza kuchanganyikiwa na UBINADAMU,...
.... kwa kumsikiliza MALAYA na kustukia kuwa  kumbe naye KWA MARA YA KWANZA kuonjea ENEO ANUAI la chini  utamu wa kiutu uzima,  NANIHII au KITENDO CHA KIWANZABANGA hakikuwa kama alivyofikiria  , na nanii iliuma na KWA HILO wala hakukioanisha KITENDO  na UTAMU.:-(

Swali:
  • Si unajua unaruhusiwa KUNIBISHIA au kufyonza kidogo kama HAPA  sichezi karibu na uelewavyo mahubiri ?

Ndio,...
.... unaweza kujifunza NI KWANINI  busara za ENZI za ``WAHENGA WALISEMA´´ kuchagulia mtu LIMCHUMBA wala ilikuwa sio kitu cha ajabu kwa KUKAA MKAO WA KUANGALI A kuwa  kama KONYAGI chungu kwa mara ya kwanza yaweza kugeuka kwa MLEVI wa KONYAGI kuwa tamu,...


.... basi hata LIMCHUMBA USILOLIPENDA kwa KULIDEKU au kulisikia tu LISAUTI lake la CHURA kwa MARA YA KWANZA ulilochaguliwa na BIBI laweza geuka bonge la MKE au MUME TAMU ukilizoea ingawa ni kweli bado lina tako moja dogo , BONGE la MATEGE yasiyooana na KIFUA kikubwa  chenye nyonyo SAIZI  NDOGO kama njegere kwa kuwa tu UMELIZOEA na kustukia kuwa hilo ukilichukulia lote kwa jumla kutoka kwenye NYWELE zake za  KIPILIPILI, ubongo, ROHO YAKE NZURI, lipatiavyo  kupika ubwabwa wa nazi wenye utandu na ukoko fresh, STAILI ya likupavyo starehe za KIUTU UZIMA, mpaka kwenye miguu yenye magaga  isaidiayo kuchana shuka,...

... hilo bado ni TAMU.:-(


Swali:
  • AU?

Ndio,...
... binadamu cha kwanza afanyacho akizaliwa tu ni KULIA kitu kiashiriacho UCHUNGU ,...
... ingawa kuna siku PAMOJA na UCHUNGU WOTE WA MAISHA MAGUMU utalikuta linachekelea kanyau au tu linaguna kisa eti linasikia UTAMU.:-(

NIMEACHA nikiwa na matumaini unatambua hili ni WAZO tu MHESHIMIWA!:-(

Hebu tujikumbushe tena YESU  wa kilatino ndani ya MAREKANI




Tujikumbushe Isse Sagawa Mjapani MLA WATU/ mwenye hamu ya kula watu katika -The Cannibal that walked Free



Au tu Sambulumaa wabadili mkao kwa -DEZO DEZO

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP