Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

JANA, leo na KESHO vimebanana!:-(

>> Thursday, February 10, 2011

... bila kusahau LEO, kesho, KESHO KUTWA na siku ifuatayo kesho kutwa,...
... kuna eneo vimeungana KAMA SIO TU kuwa vimegusana!:-(


Na inasemekana vilivyobanana,...
..... vinamchezo wa  kuambukizana kitu  hata kama havijaingiliana ila tu  vimegusana.:-(

Swali:

  • Si wakati ndani ya MAISHA ya MTU ni mfululizo tu wa SIKU zilizoungana?

Ndio,...
.... katika siku zilizo BANANA,...
..... ya KESHO KUTWA , leo na SIKU ZIJAZO  yanaweza kuwa yameambukizwa  katika mfululizo wa yaliyokutokea JANA,...
.... kimtazamo , au mpaka  KIUYATAFSIRIVYO tu  mambo!:-(


Swali:

  • SI kuna maswala YAATHIRIO TOTO KUBWA aka MTU MZIMA  siku za UKUBWANI ni matokeo ya yaliyolitokea TOTO siku za wakati KUBWA ZIMA lilipokuwa bado KINDA?


Ni wazo tu hili MKUU !:-(
Na nakutakia SIKU NJEMA Mheshimiwa!:-(


Hebu MUSEVENI abadili wazo kwa kushuka rap tena katika -Do you want another rap



Au tukutane tu tena na Toto Tundu IDD AMIN katika kitu siriasi kidogo...


2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

emu-three 12:41 pm  

Sijui mkuu kama nimekupata vyema, ni kuwa TABIA NA HULKA ya mtu hutokana na `asili' yake. Katika mtiririko wa ukuaji kama mzee mzima alikuwa anakwiba nyama jikoni, ni yumkini akawa `mwizi'!
Na pia ukikaa kweny uturi ni yumkini ukanukia, kwasababu `umeambukizwa na harufu!
Kama yalivyo masiku kuwa jana na leo, na kesho na keshokutwa, hivi unaweza `ukaona tofauti' labda ...kwenye mpangilio wako wa kukaa kwenye `viti virefu' leo hapa kesho kule, au kama ni mchoroaji wa vyupi...leo huyu kesho yule...lakini siku na `ile zinafanana, kama hulka ya mtu toka utotoni inavyofanana naye!
Mhhh, mkuu naona nami kazi `ZIMEBANANA' na ulishindwa kunijibu swali langu kama kweli unatokea huko milimani? Au ndio nyie mumezaliwa `MUJINI?

Rachel Siwa 6:14 pm  

HAHAHHAHHA YES SEVOOOOOOOOOOO!!!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP