Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kuna MAMBO huhitaji KUYAELEWA!:-(

>> Friday, April 17, 2009

Ndani ya mambo MILIONI ndani ya siku,....
.... KUBALI kushindwa yote KUELEWA ili uishi kwa furaha.

KUELEWA sana ni siri ya KUTOELEWA SANA,...
....hasa katika pande na SURA MIA za KITU KIMOJA wakati mmoja.


LAKINI elewa KIELEWEKACHO,...
... kwa kuwa ukijifanya HUELEWI UELEWACHO,...

KUNA JAMBO UNAELEWA!:-(


Swali

  • AU?
NAWAZA tu USITISHIKE!
Ngojea Kool and THE Gang waseme -Hi De Hi Hi De Ho

Au tu YellowMAN adai -AFRICAN CHRISTMASS

5 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 9:29 pm  
This comment has been removed by the author.
Yasinta Ngonyani 9:19 pm  

Mi sijaelewa:-(

Koero Mkundi 6:41 am  

kaka Kitururu,
Ni siku nyingi sijapita hapa kibarazani kwako....
kusoma vibweka na vifikirishi vyako...
bnaona umepunguza ukali wa maneno...
Hongera

Christian Bwaya 10:47 am  

Simon,

Umenena yaliyo kweli. KUna mambo mengi ukiyajua, ndio unakuwa mwanzo wa mwisho wako.

Ndio maana kuna rafiki yangu mmoja alikuwa akitania siku moja kwamba akili ya mwanadamu ni vyema ikawa gizani (tuwe wajinga) ili tuishi kwa amani. Tuchukuliane na watu. Kwa sababu hatuoni tunachopaswa kuona.

Akili hiyo hiyo ikifunguliwa kwa kupewa elimu ya kweli kweli, ndipo mgogoro unapoanzia. Kila kitu kuhoji. Kwa kuona wasichokiona wengine basi unakuta unakosana na watu.

Huenda ni kweli. Bila shaka.

Lakini je, hasara ya kuyajua mambo inaweza kufanana na hasara ya ujinga?

Simon Kitururu 2:12 pm  

@Yasinta: :-(
@Dada Koero: Asante!
@Bwaya: Halafu inatisha!Bado mimi ninafeva kujua lakini!:-(

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP