Ushawahi kumchungulia na sio kumuangalia MTANZANIA akijifunza Kingereza?
Wewe unashuka ung'eng'e?
Hivi Rais wa Ufaransa ni fala eeh kwa kuwa ung'eng'e haupandi?
Katika hii shughuli unaweza kujikuta unabana pua ikiwa yote ni katika miondoko yakujifunza UNG'ENG'E.
Na unaweza ukajikuta unaiga mapozi ya Padre Wakiitaliano asiyejua Kiingereza akiongea ,yote ikiwa katika kudhani ni miondoko ya lugha ya Ung'eng'e, hasa katika kudhani Wazungu wote wanashusha UNG'ENG'E.
Na kama ni mpenda miziki ya HIPHOP , hukawii kujikuta Dar-es-Salaam umevaa nguo za Winter , yote ni katika kudhani mapozi na azungumzavyo 50 Cent ni Kiingereza safi mpaka usikie eti ni akina OBAMA katika Wamarekani Weusi ndio waelewekao na kushusha lugha ipaswavyo na sio akina P. DIDDY.
Na wale wampendao Bob Marley , basi jasho litakutoka tukianza kuongea Kijamaika kwa lafudhi ya KIPARE au KIHAYA.
Hii shughuli wee acha tu!
Lakini kujifunza lugha yoyote mtiririko wa kujua ni uleule!
Na huwezi kupatia kabla hujakosea mara kenda zisizohesabika!
Swali:
Unakumbuka mapozi yako wakati unajifunza Kiswahili au kwa sababu umezaliwa Tanzania unadhani ulizaliwa unajua Kiswahili?
Kwani kujua lugha ni mpaka uwe na lafudhi ya lugha?
Na kumbuka kumcheki ajifunzaye lugha, kuna starehe zake na bado BINGWA ni MTOTO.
Kumbuka kama unajifunza kukosea imo ndani ya huu mchezo. Na kama kuna akuchekaye, kumbuka inachekesha lakini maishani kuna ulivyomcheka mtu na hiyo sio siri ya kuacha kunoa NANIHII kama lengo ni kujua NANIHII hata kama unachekwa kwa kithembe.
Na kumbuka mwisho wa yote , lugha ni kwa ajili ya mawasiliano.
Na kama Wakatoliki wanamuelewa Papa, basi kama mtu akikuelewa ndani ya sentensi ''ze milk is standing'' huongelei maziwa ya kunywa bali titi lenye misuli ya nguvu na ncha kali iliyonuna , basi ujumbe umefika na matumizi ya lugha yameshamaliza kazi yake.
Swali :
AU?
Umestukia hata uongee kwa ufasaha gani kuna tutakaoshindwa kukuelewa unamaanisha nini?
Ni Watanzania wangapi unadhani wanajua Kiswahili fasaha ambacho ndicho Kiswahili?
Nimeacha! Ni moja ya wazo tu na WIKIendinjeMA!
Narudi tena Nigeria kwa Majek Fashek aongee...
Au tu TMK Wanaume FAMILY wadai -DAR mpaka MORO
ASANTENI WADAU WOTE msionitenga! Nakuacha na baadhi za Picha na Washikaji!
Watoto ni wabunifu kuliko wakubwa wa HADITHI na kama unabisha wavizie wakicheza usikie wanavyosimuliana hadithi walizobuni wakati wanaendelea kuzibuni.
Kikubwa ni,... ... hata mtoto ukimuacha acheze mwenyewe, kama aliwahi kuona gari anaweza kugeuza ndala liwe gari na pia akajisimulia mwenyewe STORI kuhusu kuwa hilo gari aina ya NOLINOLI a.k.a ZIMAMOTO au ze AMBULANSI na jinsi lilivyookoa mtu na mende!
Swali:
Hivi hapa sijadanganya kweli kuwa watoto Wakibongo waliowengi wanajua kuna gari la wagonjwa na zimamoto a.k.a NOLINOLI?
Tuendelee.....
Ukikutana na MKUBWA anamsimulia mtoto hadithi iliyotungwa na MTOTO basi huyo mkubwa SPESHO!
Tatizo ni,... .... stori a.k.a hadithi za wakubwa ndio zisakiziwazo watoto kwa kigezo cha kuwa zinamafunzo.
Na kama wakubwa wangekuwa wanajifunza na wanamafunzo , akina Yesu, Mohamedi, Gandhi, Babu Mrinde, na hata BULICHEKA na ABUNUWASI kuna mambo wangekuwa wamemaliza enzi hizo kufunza waliotutangulia wenye uume na uke, na siye wengine hata wasiwasi wa UKIMWI kama tu KASWENDE achilia mbali KUFA NA NJAA , tungekuwa hatuna kama jinsi tusivyokuwa na wasiwasi na matumizi ya choo cha shimo.
Na naamini HISTORIA haitufundishi kitu kutokana na STORI za wakubwa kufundishwa watoto , WATOTO wenye stori orijino.
Stori za wakubwa ukiziangalia vizuri , ni za Kiyesuyesu au za TISHA TOTO zisababishazo watoto HATA WAKIKUA wanakuwa WATOTO WAKUBWA halafu wengine ndio hawa tunawaita VIONGOZI WAHESHIMIWA WAKUBWA waendeleao kuongoza na KUTULEA kwa staili za TISHA TOTO!
Sikatai umuhimu wa uzoefu! Sikatai ukisimulia uzoefu wako, na labda ndio maana wengine tumejifunza mpaka katerero kutokana na stori na sio kupiga chabo.
Lakini ukitazama , utastukia kuwa ni hadithi za wakubwa zinazopelekwa kwa watoto na kuendeleza sanaa za kutaka kutafsiri kwa watoto kuwa kwa kuwa wewe sio kama mimi kwa kuwa mimi na kifafa, basi unikwepe nikijamba usijepata kifafa , wakati kifafa inajulikana hakiambukizwi kwa ushuzi.
Na stori hizi a.k.a hadithi hizi ndio hizo zinasababisha toto likikuwa lifikirie sijui likubake au kukupiga konzi kama sio kukubagua kwa sababu wewe:
Zeruzeru
Muarabu,
Muhindi
Chotara
Jeusiiiii
Pua kama nundu
Sangara wamo
Titi ndimu na chuchu mwiba
Meno kama ngiri
Ustadh
Mlokole
BAYAAAA!
ZURIIII!
Muafrika
Muislamu
Mkristo
nakadhalika tatu na nusu.
Swali:
AU?
Na,... ...KUBWA ZIMA sikiliza watoto wakisimuliana hadithi orijino ugundue kitu au hata ugundue HADITHI NI NINI.
Na kama simulizi lako ni la yaliyotokea kweli, SIMULIA ingawa nayo inaweza kuwa ni HADITHI ila isiyotungwa. Na simulia kama unafikiri ni kweli ni lazima kila stori huwa inabidi isimuliwe.
Swali:
AU?
Si unakumbuka kuwa si kila hadithi hutungwa?
Unafikiri ni kwanini kuna unavyoacha kutusimulia na kwa vigezo gani kuna utusimuliavyo?
Nimeacha na ni moja ya wazo tu ! SAMAHANI!
Tulia na stori ya SamnaEsther(WARNING! Ni ya HUZUNI!)
Au mpate tu Innocent Galinoma asimulie kuhusu ya- RAIN
Na kama akina.... ..... Hitler, Mao , Mandela, Kenyatta, Nyerere na Kawawa walishaongea na kufanya na halihalisi ndio hii , akina Kikwete, Kibaki, Museveni na Zuma watakachofanikiwa kufanya ni kututafutia cha kuangalia pale watakapo ishia na labda pasipoeleweka wala kutosha!
Swali:
Na kama akina BUDDHA na .. walishahubiri na kufanya, watuhubirio leo wanajipya la kuongea na kufanya libadilishalo au kuongezea ONGEO au HUBIRI?
Na kumbuka,.. ... kama hufanyi na tunaongea, hata ukifanya tutaongea.
Tatizo ni,.... ...... kuna watu hawatajua ya Yesu, Mohamedi , Buddha au hata Mtikila kesho kama hutaongea.
Swali:
AU?
Nimeacha!
Ni wazo tu Kingunge! USITISHIKE!
Namuachia Justin Kalikawe aseme ya -UGENINI
Au turudi kwa Mnijeria ASA azungumzie tena- Jailler....
NA ukiamka ili ndoto itimie ,.... ....kumbuka ufanyacho kwa kukitolea macho si NDOTO!
Na ukifikiri ulipata mimba au kumpa mtu mimba ndotoni, hiyo ni kubaka na haikuwa NDOTO.
Ndoto ni KISURA!
Ndoto ni JINAMIZI!
Na ukiamka waweza tengeneza JINAMIZI au KISURA na chachandu ya shughuli inakolea kwa kuwa UKIAMKA , wewe UKO MACHO!:-(
Na,... ... Amka ndoto itimie ! Ingawa tukikuona UMEAMKA na unalia tutajua nini KIMETIMIA!:-( Na ukilia ni dawa ya majonzi na mwanzo wa utamu wa yasiyo NDOTO na unajua tayari kilichoKULIZA!
Swali:
Unauhakika uko macho?
DUH! Wazo na linakomea hapa kwa leo!
Ngojea Richard Pryor abadili hali ya hewa kwa Kuongelea watoto wakidanganya katika- KIDS Lying
Au ngojea Beenie Man naBarbee warudishe kitu katika- GIVE IT UP
Kusoma nishai, ... .... ghafla unaweza ukasoma kitu halafu ukajua na kustukia kumbe unadalili za MIMBA!
Halafu,.. ....kulalamika ni bomba la faraja kwetu wote NA karibu kila MTU ni PROFESA :-(
Wakati unalalamika kuwa vijana wa siku hizi hawapendi kusoma , KUNAUWEZEKANO unachangia KUSABABISHA tupende kuangalia TV na labda PICHA ZA UTUPU mtandaoni kwa kuwa unatuandikia maandishi yasiyonyegelesha watu kujifunza HESABU.
Lakini,... ... watu wasiposoma inasaidia !
Na kama unanibishia waulize MAPAPA wa KIROMA wakukumbushe enzi zile za waumini kutojisomea wenyewe BIBLIA jinsi ilivyokuwa starehe kuwasimulia watu biblia inasema nini halafu mtazamo wako na TAFSIRI ZAKO unakuwa ndio kweli tupu na hakuna wakukubishia.
Samahani LAKINI PAPA WAKIROMA!
Nilisahau kuwa watu hata siku hizi hawasomi biblia wala korani (ingawa vipo gesti pembeni ya kitanda tukienda kupona), kitabu cha JUMA na ROSA wala KAMASUTRA, na kwa kukubishia HUTEGEMEA ZAIDI ni kwa mtazamo wa nani MWINGINE wanafuata TAFSIRI ZAKE na mtazamo wake katika kuelewa njia ya kwenda mbinguni au tu ile ya LIMBWATA kidume aitulize nyumbani.
Na Lakini UNAYEANDIKA labda usitishike! Bado tupo tunaosoma na kuandika hata ujinga kwa hiyo MHESHIMIWA ukiandika uandikayo YA MAANA na YAHESHIMA labda tupo tutakao soma hata kwa nia ya KUJARIBU KUKUELEWA TU au kujiweka katika mkao wa kutaka KUKUTUKANA , kwa hiyo usiache kuandika KINGUNGE. Swali:
Au?
Hivi nilikuwa naandika kuhusu nini vile?
NA nimeacha KINGUNGE mheshimiwa! Kumbuka ni wazo tu hapa MAWAZONI! BAADAYE! Ngojea Basi ERYKAH BADU alete -FUNKY NASSAU
Kwa kujiheshimu,... ... unajikaza ILI tusijue , ujitunzie HESHIMA. Kwa kujiheshimu,.... .... unajitunzia yale ambayo unayo ila hutakituyaone ili TUKUHESHIMU.
Tatizo ni,.... .... waheshimuo wezi huheshimu wezi na kama wewe sio mwizi HUSTAHILI kwao HESHIMA.
LAKINI Jiheshimu tu huku ukijua kuwa,... ... wasiojiheshimu wanaheshimiwa pia hata kwa vigezo hivyohivyo vya kutojiheshimu.
Kizuri ni,... ... heshima ni kitu cha bure , hakitakukosti hata ngawira pesa mbili.
Tatizo la kutojisheshimu ni,... ......unaweza heshimiwa na wasiojiheshimu!
Swali:
Unapendelea kuheshimiwa na wanaojiheshimu au na wasio jiheshimu?
Ushastukia kama usingekuwa unajiheshimu , leo ungekuwa tajiri kidoooogo zaidi ya ulivyo sasa na labda ungekuwa umenuna zaidi?
NI wazo tu na NIMEACHA MHESHIMIWA!
Ngojea MZEE MZIMA gwiji la COMEDY a.k.a REDD FOXX aongee kwa heshima ya kujiheshimu katika-WASH YOUR ASS...( WARNING!Lugha chafu na mambo ya WATU WAZIMA)
ASHKI za kula MTU, si lazima iwe UNAKULA kwa KUTUMIA MDOMO!:-(
MAFISADI kwa KUMLA MTU , wanamuacha na NJAA.
CHEKIBOBU kwa KUMLA MTU , bado anabaki ashaliwa lakini bado ANAHAMU.
MSENGE kwa kula MTU , inasemekana huchagua nakuvutiwa KUMLA nyuma.
ASIYE MSENGE akila, anahisi anakula mbele ila LABDA ni analia mbele ya NYUMA.
MCHUNGAJI WA KANISA kwa KULA WATU , bado mpaka kwa wajinga huwadai SADAKA.
SHEKHE kwa kula ,anaweza asistukie umekaa mkao wakuliwa vizuri kwakua wengi HATA wainamao , wamkumbusha msikitini wakiinama ni katika mkao wa kuomba MUNGU.
WANAWAKE kwa KULA , wanaume waweza kuzidi kustukia utamu mpya wa CHAKULA.
WANAUME kwa UANAMME WAKILA, mama na mwana KAENICHONJO kama mwataka KULA.
WATOTO kwa KULA, mabaki ya wakubwa hayakawii kuwaacha na NJAA kwa ulafi WAKIKUBWA.
WEWE KWA KULA,.... ....NYANI kasingiziwa.
Swali :
AU?
NI moja ya WAZO ndani ya kucheza na lugha ya KISWAHILI TU! SAMAHANI usitishike Mheshimiwa!
Ngojea John LEE Hookerakiwa na Carlos Santana abadili wazo kwa kibao...-CHILL OUT
MOja ya shughuli ya BINADAMU ni KUTAFUTA MAANA ya VITU!:-( Na akisikia simulizi za KIBOXI MANYOYA ataoanisha nini kinamjia akilini katika mrengo wa KIBOXI MANYOYA.:-(
Na labda manyoya NI ushahidi kitu ni KUKU au NGURUWE!
KIBOXI MANYOYA labda maana yake UMEKUA!:-(
KIBOXI manyoya LABDA maana yake wewe ni NYOYA na nikipuliza UTAPEPERUKA!:-(
KIBOXI MANYOYA labda ni KIBOKSI cha MANYOYA chini kidogo ya KITOVU pamoja na ukweli kwamba ni NYWELENYWELE na wewe UNAJUA NI MTU na huna MANYOYA.
Kiboxi MANYOYA ni ushahidi binadamu anavisivyo na mpango wala matumizi MWILINI na AKILINI.
KIBOKSI MANYOYA ni ukubwa hata kama bado MJINGA.!
KIBOXI Manyoya labda ni kiboksi chenye MANYOYA na maana yake ni tafsiri za ubongo wako na kama ni mfikiraji wa matusi labda KIBOXI Manyoya ni MATUSI!:-(
Swali:
Unauhakika kuna kitu ninamaanisha?
Kwani ni lazima kila kitu uelewe mwaniwane?
LIONE VILE!
NIMEACHA na kumbuka nikatika kupitia moja ya wazo katika MAWAZO na ,WIkienDI Njema KINGUNGE!
Ngojea basi kidogo MACY GRAY achokonoe kwa kibao-I TRY
GHAFLA maoni ya wazazi hayatoshi.... ... Wazazi katika uchaguzi wa kigoli hawalipi umuhimu kama magazeti yalipavyo kipaumbele TAKO.
GHAFLA tabia nzuri iliyozoeleka haitoshi,... .... Nikitazama TV nastukia ni ya kishamba na naogopa nitachekwa kijiweni tukikaa KITAKO.
GHAFLA titi ni dogo na mnuno wa chuchu isiyomumunyika haitoshi,... ... hasa katika staili za siku hizi za hata wasiopata kwa kukuna kichwa wawezapata kwa kukuna TAKO.
GHAFLA hata wastaarabu wavaavyo haitoshi,... ... baada ya kuangalia tangazo sijali roho wala moyo mkubwa, kama nguo itaonyesha japo udogo wa TAKO.
GHAFLA aitwaye modo asiye na tako ingawa alikuwa hatoshi,... ....baada ya tangazo kwenye luninga nimejifunza jinsi ya kuligundua lake TAKO.
Labda na GHAFLA mke nitakayepata atakuwahatoshi,... ... Lakini TV na Magazeti yatakuwa na tangazo nitakaloletewa lenye dawa ya tiba ya huzuni nikikaa KITAKO.
Si hata nitakao wasikiliza wakinishauri haitoshi,... ... na si busara zao zatoka kwenye matangazo na wanapenda kubwa au dogo TAKO?
Matangazo mwanaharamu weye na tuombee iwe hautoshi,... .... la sivyo kwa waitwao wajanja ubongo utatoka kichwani na kuhamia kwenye TAKO.:-(
NIMEACHA! Swali:
Unafikiri matangazo hata ya pipi hayajakuathiri au kukufunza ununue pipi gani?
NI moja ya wazo tu USITISHIKE!
siKUNJema!
Au tu St Germain waje tena na kibao nikihusuducho kiitwacho- SURE THING...
Event:Saturday Night Live! Tukio:Performance Sehemu: Sweet Eazy Restaurant and lounge Muda wa shoo: Saturday, April 18 at 9:00pm Muda wakumalizika shoo:Sunday, April 19 at 1:00am Mahali:Oysterbay, Dar-es-Salaam
Hakuna fomwula za kuacha au kujifunza ,.... ......kwa kuwa tu jambo UMELIPITIA!:-(
Unaweza kuzeeka na UJINGA ingawa tokea ujanani .... .....Ujinga UMEPITIA.
Kwa kupitia kitu unaweza ukachanganyikiwa na kuchanganyishwa zaidi na ... ......usijifunze wala kujua ingawa yote UMEPITIA.
Na kwa kuuzoea ujinga , ... .... unaweza kukomaa kwa ujinga usiuone tena ujinga na yote ni kwa sababu UMEUPITIA.
Kwa kuzeekea shughuli ,... ... unaweza kuzeeka na shughuli tu, na usijue shughuli UNAYOIPITIA.
Swali:
Unafikiri ndoa ihusishayo mabikira wawili ambao shughuli bado hawajapitia sio bora kuliko ya wale waliokomazwa na shughuli na advencha za hughuli wameacha kupitia?
Kwani hujawahi kukutana na Mzee MJINGA?
NA bado ni kweli,... ..... kila mtu anachakukufundisha kwa kuwa karibu kila mtu kuna kitu sio MJINGA! Na,... .... mjinga anaweza kukufunza jinsi ya kuwa mjinga madhubuti! Swali:
AU?
Ni moja ya wazo tu katikaUjingaBUSARAna USITISHIKE!
Siku njema!
Ngojea Sanchez aseme -Baby can I hold U tonight
Au tu Buju Bantonna Wayne Wonder wadai-I dont know why
Inasemekana wanawake hawasikii kama wanaume na wanaume wenye sikio zuri la wanakike , ni wasenge!:-(
Na labda ni kweli kama wewe unamtunza MPENZI au una penzi basi wewe ni bingwa wa michezo ya akili.
Na,... ...hata ukilivutia punzi penzi unaweza kuambulia mwili na sio penzi ndani ya michezo ya akili ya apendaye na apendwaye yenye mwili.
Na usipoangalia huu ndio wakati unaweza kufikiri unapatapenzi, kumbe mtu kafikia hatua ya kuwa anachokupa ni kikojoleo na kiungo cha kutemea mate na sio tena kiungo cha penzi na busu katika penzi.
Na huhitaji kuvutia punzi au kututumua misuli kujua umeachana na mpenzi, kwani kitendo chakumuacha mtu hakihitaji nguvu wala akili:
Siku ya kumuacha mpenzi kimapenzi utajua tu umemuacha hata kama hutamuambia na utaendelea kuendelea kuishi naye katika hii michezo ya AKILI ya PENZI na kutobadili uliyokuwa unafanya wakati unapenzi! Na kikwapa chake utakistukia.
Na katika michezo ya akili, anayechunwa buzi anaweza akawa anajua anachunwa buzi na hiyo ndio kete yake katika michezo ya akili ya PENZI na anajisikia vizuri angalau unaona anafaa angalau kwa kuchunwa buzi, na ni PENZI!
Na pamoja na yote bado nivigumu kuwa na uhakika umepata mpenzi hasa katika dunia hii ambayo mwanamke na mwanaume wanatokea sayari tofauti na swali moja linaweza likawa linataka jibu tofauti na swali hasa kama ni mwanamke anauliza na sio katika PENZI.
Na bado,.. ..... katika MICHEZO YA AKILI hata kulia IMO , ingawa wakati unalia ili mpenzi AKUONEE HURUMA, unaweza ukawa unalia kirahisi kwa kufikiria lile shamba la mihogo ambalo mkiachana ndio nalo limetoka hivyo:-(
NIMEACHA! Nawaza tu kumbuka hilo MKUBWA!
Swali:
Unauhakika gani kuwa wapenzi uwaonao wanapendana na sio mmoja ndio ampendaye mwingine?
.... YA MUNGU yanachanganya..... .... na ya SHETANI hayakawii kuisha UTAMU.
Binadamu katika kujazia mapungufu, ..... ..... hujaribu kuongezea ya MUNGU, Miungu au hata ya SHETANI na ukweli katika imani kirahisi tu unaweza kujikuta unapitia
Kutokuwa na IMANI,
Kujifunza Imani,
KUAMINI ,
kupungua imani,
kuacha kuendekeza imani na hata mwisho kuanza KUAMINI TENA!
Yote huwezekana ndani ya maisha ya binadamu!
Na ukifa wakati tunaamini unaamini tunachoamini kama vile MUNGU, katika mazishi yako tutadai umeenda MBINGUNI!
Na tukiwa na wasiwasi na imani yako wakati unatutoka, BADO tunaweza tusikiri hadharani kwa kusema tunauhakika unakwenda kwa SHETANI ingawa kwa kimoyo wazo hilo lipo.
Swali:
AU?
Kuna sababu karibu kila jamii DUNIANI kuna kitu inaamini ambacho kinaoanishwa na kuwa na uwezo kuliko binadamu hata kama hicho kitu ni binadamu kama walivyokuwa MAFARAO Misri.
Na atafutaye jawabu na faraja KATIKA IMANI ashawahi kukwama kibinadamu!
Na kama ushawahi kukwama kibinadamu labda ushaanza kuwa na BUSARA.
Swali:
AU?
Bado hushangazwi kwa wasiojua vizuri hata dini zao walivyonauhakika na kasoro za dini za wenzao?
NAWAZA TU MKUU hapa MAWAZONI usitishike! Tutulie na Black Uhuru waulize- What is life
FARAGHA bomba ya kitu labda ndio maana ndio kutengenezewako watoto!
Hadharani nishai ndio maana MPAKA wapenda ngono wanaweza kukupiga MKONG'OTO ukionja hadharani kama vile hawajui kwanini unaonja , kama Padre wakikatoliki asiye MBONGO!:-(
Na labda padre asiyeonja anatubu faraghani kwa kumfikiria tu hata muumini mwanana akaaye kiti cha mbele kanisani ambaye anahisi faraghani au hadharani akibinuka kunatatizo la dhambi hata ambayo haijatendeka inatendeka.
Swali:
Umestukia ni hadharani tu unawatia aibu WATU?
Umewahi kujiuliza kama MUNGU anakuona mpaka chooni wakati unafikiri hujamtia aibu hata kwa staili yako ya kuchamba?
Kumbuka hata ukijinyea faraghani tusipojua ni poa tu !
Na labda,.. ..... waheshimiwa wanaheshimiwa kwa yasiyo faraghani na ndio maana labda WANAHESHIMIWA! Swali:
AU?
NIMEACHA Na kumbuka ni moja ya wazo tu hili na labda ni lakijinga kwako MHESHIMIWA!
Narudi tena NIGERIA kwa the best Afro Beat artist ever in my opinion kwa jina LAGBAJA aseme -FEYINE
Lakini,... ...HERI ya PASAKA labda pia PAMOJA na YOTE , ni HERI ya kuokolewa kwa waumini HASA waaminio walitakatishwa kwa YESU KUFA, hasa kwa waaminio kwa IMANI! :-(
Swali:
AU?
Labda ni kitu kizuri kama wewe ni miongoni mwawaokolewao na damu ya YESU!:-(
Tatizo ni... .... katika vigezo, VIGEZO vinaweza kusisitizia tarehe , au tu leo, au TU wewe, na sio kutokana na nguvu ya imani.:-(
Swali:
Unauhakika hii ndio ile tarehe?
Unauhakika kama HII sio tarehe huhitaji kutubu kwa kusherehekea siku ya kufa MAREHEMU wakati sio siku yenyewe marehemu alikufa?
Kama wewe ni Mkristo unasikiliziaje CHANSI zako za paradiso leo hii ya PASAKA?
HIVI ni kweli wewe MUUNGWANA huwa unafurahia KUFIWA na ALIYEKUPENDA ?
Heri ya PASAKA! Na labda kama unaamini kwa hilo, HILO ni kweli na LEO NI PASAKA!:-)
Na NIMEACHA! KUMBUKA nawaza tu na niombee au tubu kama unakwazika!
Wapuuzi wengi hawana nia ya kufanya UPUUZI, nikatika kumalizia kitendo wanastukia au kustuliwa kilikuwa ni kitendo cha kipuuzi!:-(
Na,... ... upuuzi NISHAI! Upuuzi wa LEO unaweza usiustukie mpaka MWAKA KESHO,
....Na...
Isingekuwa hivyo waheshimiwa wengi wasingeumia roho baada ya kufumaniwa baadaye kidogo baada ya kuwa WAHESHIMIWA kuwa yaliyowapa sifa JANA labda hata uheshimiwa, karibu yote LEO ni UPUUZI.
Na labda,... .... wengi wasiofanya UPUUZI hawafanyi upuuzi kwa kuwa hawajitahidi kutofanya upuuzi bali wamebobea TU kujaribu kuishi tu LEO maisha yao kama kawaida , kama ilivyokuwa JUZI.
Na ,.... ... wale wajitahidio kutoonyesha upuuzi wanasifa labda hata za kujisifia,...
.... ingawa....
ukiwaangalia wengi wao wamenunia shughuli nzima leo usijekushuhudia wakifanya upuuzi leo ingawa kama kawaida ya ubinadamu wapo WATAZAMAJI na WASIKILIZAO wasubirio mpaka kesho kutafsiri ya leo. Swali:
Unauhakika mheshimiwa ahitajiye kuheshimiwa sio mpuuzi kwa hilo?
Unauhakika hujawahi kubadili mawazo kuhusu ulichodhani ni upuuzi na leo unadhani ni njia ya kwenda mbinguni?
Ni kweli kabisa,... ... wengi wakati wanahangaikia kukwepa upuuzi hufanya UPUUZI kwa kuwa vigezo vyao vya kwanini sio upuuzi ndio KIINI, MISINGI na tako la UPUUZI!
Sikubishii lakini ukinibishia! Naacha UPUUZI kama unauhakika nilichoandika ni upuuzi!:-( Swali:
Unauhakika wakati unataka kumbishia ambaye haelewi utakachokufanya sio UPUUZI kama hujajaribu kumelimisha?
Kumbuka HATUKUONI na USIJIHAMI!:-(
siKU Njema!
Hebu tumsikilize AL PACINO katika sinema SCARFACE....atoe -BAD GUY SPEECH (jihadhari lugha chafu!)
Au tena Les Wanyika wamuongelee -Paulina
Au tu twende Ivory Coast tukutane na Joelle C - MAN DINKA
Wakati unataka kuwa kama WAZAZI wako LABDA ni kweli wazazi wako hawataki uwe kama wao!
Kunauwezekano kabisa wazazi wako wanataka uwe kama WAZAZI WAKO walivyotaka kuwa na ikashindikana .
Na ni kweli,... .....ukizaliwa tu wazazi wako ndio wanakuwa kioo chako na kama wanaongea Kichina kunauwezekano utaongea KICHINA.
Swali:
Unauhakika kuwa wewe hujawahi kama bado sio Mkristo , Muislamu au Mpagani kutokana na wazaziwako kutoamini kuwa ubinadamu ni dini?
Lakini ,... ..... wewe sio WAZAZI wako!:-(
Wazazi wako wanaweza wakawa wamefanikiwa mpaka unaweza ukataka kuwa kama WAZAZI WAKO,.....
....Lakini...
.... wewe ni WEWE!:-(
Na unaweza ukawa ni miongoni mwa ambao hawakulelewa na wazazi wao wakibaolojia lakini kuna waliokuwa kiioo chako cha maisha hata kama ni cha jinsi ya kuwa ombaomba au jambazi,...
...na....
....hao ni wazazi kinamna kama katika kundi, ni hao unaweza kukiri walikuwa kama wazazi wako wakati unawaelezea WATU kuhusu hao ila unataka tujue hawakukuzaa.
Labda hamu ya kuwa kama wazazi wako ikififia ndio mwanzo wa KUWAKOSEA HESHIMA wazazi.
Kabla hujaacha kuheshimu wazazi kwa KUSHINDWA KUFIKIA KUSTAHILI , jaribu kupata jibu la kiswali KWANINI....
Kwa nini wameshindwa
Kwa nini wangefanikiwa
Kwa nini
Na kwanini unafikiri jibu la yote ni kutoWAHESHIMU.
Na bado binadamu pamoja na kuwa tofauti, jinsi wengine walivyo kunasaidia kutengeneza sisi tulivyo.
Mwingine akivaa JINSI anaweza akawa ndio sababu tunavaa KODRAI .
Mwingine akivaa KODRAI labda ndio sababu tunavaa KODRAI.
Hamu ya KUTOKUWA inaundugu na HAMU YA KUWA, na kwa hivyo anayetaka KUWA kama wazazi wake na ASIYETAKA wote wanafanya jambo moja ukizingatia kuwa hakuna mtoto aishiye katika umri na wakati sawa na WAZAZI wake . Nikiwa namaana wakati mtoto ana miaka mitano mwaka 2000 labda Mzazi alikuwa ana miaka hiyo mitano mwaka 1960 na hauwezi kulingana na wazazi wako ingawa mnaishi pamoja.
NAWEZA kusema,... .....ukitaka kuwa kama wazazi au usipotaka kuwa kama wazazi vyote ni vitendo vya kujaribu tu lisilowezekana. Swali:
Unauhakika kuwa unamjua hata mtu mmoja aliyefanikiwa kuwa kama wazazi wake?
NI MOJA ya wazo tu na sio kweli tupu!
Baadaye!
Ngojea Bozi Boziana anisaidie kubadili hali ya hewa kwa kibao-Demayo
Au Peter Tosh arudie kuongelea msiba katika -Burial
Inawezekana kwa SISIMIZI mtu haonekani na maisha ya mtu kwa sisimizi ni MILELE.
Na ukipiga teke jiwe alilopo sisimizi lika vuka mfereji na sisimizi , kwa SISIMIZI ataona MUUJIZA umetokea kama tu ukidondosha kibonge cha sukari na kumletea SISIMIZI kitoweo pale asipotarajia.
Swali:
Ushawahi kujiuliza kuwa labda MUNGU wa BINADAMU hasa yule wamuaminiye wawamuaminio MUNGU ASIYEONEKANA , haonekani kwa binadamu kutokana na UKUBWA TU kama SISIMIZI asivyomuona MTU?
Ushawahi kustukia kuwa hata utumbo wako ni ulimwengu wa baadhi ya bacteria ambao wanaumbwa na kufa kabla yako MUMO KWA MUMO wakiishi kwa manufaa yako ya kulainisha chakula na kukusaidia kukutengenezea kinyesi bomba?
Na ukimkanyaga sisimizi ni kiama kwa sisimizi!:-(
Nimeacha! Na ni moja ya wazo tu kumbuka!
Badili Mudi kwa kusikiliza En Vogue wadai -Dont let GO...
Au tu Michael Jackson aseme -WORKING DAY and NIGHT
Shujaa ni shujaa kwa sababu anafanya usichofanya ukitumia AKILI.
Na kumbuka,... ... mashujaa karibu wote HUKUMBUKWA kwa JAMBO MOJA TU la kishujaa LILILOSHUHUDIWA katika maisha haya ya binadamu yenye mambo mengi YASIYOSHUHUDIWA.
Na ni kweli,.... .... unahitaji jambo moja tu ili ukumbukwe kama SHUJAA au MJINGA.
Na tendo la kishujaa karibu mara zote hukaribiana na tendo la KIJINGA zaidi kuliko tendo la BUSARA ndio maana ukikosea kidogo tu, jitihada zako za kutaka kuleta ushujaa zinaweza kutafsiriwa kuwa ni UJINGA.
Swali
Unauhakika wewe sio shujaa na hatujashuhudia tu TENDO MOJA lako ambalo litakuoanisha wewe na neno SHUJAA?
Kumbuka tu ,.... ... mjinga umjuaye kwa ujinga kwa kuwa umeshuhudia ujinga , kuna wamtambuaye kwa jina shujaa kwa kuwa WALISHUHUDIA wake USHUJAA!
NIMEACHA! Tupumzike kwa kubadili hali ya hewa na kusikiliza ni kitabu gani hakiuziki Kenya wakati tukifikiria ya Tanzania...
Ngojea JAMES DANDU aongelee- MPENZI
Au tu REMMY ONGALA aulize- MIZIKI ASILI YAKE WAPI?
Ni mchanganyiko wa kemikali UBONGONI ukuambiao UNAFURAHA na kikufurahishacho ni katalisti tua.k.a kichocheo, kisaidiacho ubongo kukushawishi kuwa UNAFURAHA.
Na kwa kawaida Homoni , Nevu,....- mwilini , husahaulika katika mchango wake katika kufanya kikufurahishacho kikufanye UNAFURAHA.:-(
Na kwa kuwa tunafurahia FURAHA bila kutafakari ni nini HASA kiko kwenye kitufurahishacho kwenye FURAHA,...
... daima kitaadimika hiki kitu FURAHA!
NAWAZA tu usistuke! Swali:
AU?
Unafuraha?
Au pata WORD OF WISDOM ya kinamna kama unamoyo....
ASANTENI Ndugu, jamaa , marafiki pamojanaMAADUI!
Asanteni sana wadau wote ambao wengine ni hawa kwenye picha nilizodakwa na kudaka juzi ya jana ya juzi.......
Labda ,.. ... umzimiaye KWA HILI hana kasoro katika hili kwa sababu HUMJUI!
Ukianza kumjua umzimikiaye na kama hujapofuliwa na UKIZIMIACHO, labda UMZIMIAYE ndiye bingwa wa USIYOYAZIMIA.
Lakini ku -ADI-MAYA mtu bado ni bomba kama kuna kusaidia kupata nguvu mpya ya kufanya tendo badala ya kulifikiria tu TENDO.
Na labda unaye M-ADIMAYA kwa sura na umbo zuri ndiye mwenye tabia MBAYA. Na labda unaye M-ADIMAYA kwa kumsikia tu, ukikutananaye ndio itakuwa mwanzo wa chuki yako kwake.
Na labda kuna unayemnunia kwa hili lakini ungejua lake lile sasa hivi ungekuwa unajishughulisha akuone ili UMCHEKEE. Swali :
Bado unauhakika unataka kujua zaidi kikufurahishacho wakati unajua kunauwezekano kwa kujua sana hata maziwa, ni kweli maziwa ya mtindi ni maziwa yaliyoharibika na unayanywa kwa sababu za kutoyafikiria kuwa yameoza?
INASEMEKANA kama unataka UHURU wakutaka kuongea utakayo na kuyaweka wazi bila vipingamizi vya mhariri, UNAWEZA kuanzisha BLOGU au kuweka tu mawazo yako kwenye internet!
Lakini kumbuka,... ...hata UHURU WA KUSOMA unawezakusababisha USISOME!
Tatizo ni,... ..... unaweza kustukia jinsi gani usivyo huru kwa kujikuta hauko huru HATA kama uko peke yako kwenye BLOGU na internet!
Na usipoangalia LABDA umeshajibatiza mpaka jina jingine kwenye BLOGU au INTERNET kwa UHURU kama wewe hutumii jina LILE maarufu la ANONYMOUS ,hasa PALE ukitaka kujaribu kwa mara nyingine kuwa HURU angalau kutoa dukuduku lako kwa uhuru wewe UDAIYE UKO HURU.:-(
NA,.... ..... baada ya miaka kibao ya HABARI kuwa ni BIDHAA HADIMU ambayo watu wachache ndio wawasimuliao wengine kuwa leo HABARI ni nini, sasa kumezaliwa Blogu, Twitter ,nk. na YOUTUBE inashindana na TELEVISHENI ingwa ni wachache watumiao hizi tekinolojia WAKO HURU kukuambia wanachofikiria kama wewe ni mlengwa na wanadhani hawatanufaika kwa wewe kujua wanavyo kufikiria.
Swali:
Unauhakika katika KUNDI hujali na kuthamini zaidi kusikilizwa na BAADHI tu ya watu fulani katika kundi la watu ukipewa uhuru?
Unakumbuka kuwa kwa udhaniaye ana akili huwa unaruka kutilia maanani YALE yake ya kijinga kwa uhuru?
NA,.... .....Kumbuka wote tunaongea ingawa UNAMSIKILIZA zaidi kwa HIARI na UHURU aongeaye upendayo KUSIKILIZA!:-(
Kabla sijaongelea JELA ya UHURU , .....
....KUMBUKA inasemekana,...
Kwa uhuru ni rahisi kukimbilia mambo rahisi kwa BINADAMU mwenye silika ya UVIVU na hamu ya kurahisisha!
Na binadamu unaweza kumgawanya katika makundi mengi ingawa kirahisi unaweza kumgawa katika makundi kwa kustukia kuwa ni Mwanamke au Mwanamme na je ana UMRI GANI hasa kama hamu yako ni KUSIKILIZWA. Lakini pamoja na kumjua utakaye kumuongelesha, bado unaweza kukosa uhuru wa kusema UNACHOFIKIRIA.
Na,... .....hata kwa kutumia KIGEZO CHA KIJINSIA TU, inajulikana binadamu anavutiwa na kupitiwa mawazoni na mambo kadhaa yajirudiayo kila siku kwa kigezo hata hicho cha kuwa ni mwanamke au mwanaume.
Na kama unataka kumdaka umtakaye akusome au UMTAKAYE TU, jaribu kumjua umlengaye yuko katika kundi gani, hata kama vigezo vyenyewe ni vya kumsaidia mlengwa aliyeko kwenye kundi kuendelea kubakia katika kundi zaidi ya kuondoka katika kundi, kwa kuneemesha dalili za UDHAIFU wa mlengwa utakaye akusikilize kwa KUTOKUWA HURU HATA KUMSHAURI kama amepotea ili asikuone wewe MBAYA kitu ambacho kinakukosesha UHURU.
Lakini bado ;.....
Kama unataka kusikilizwa na MCHAMUNGU ongelea DINI au MUNGU.
Kama unataka ueleweke na mvivu wa kufikiria lakini anapenda korosho na miwa, rahisisha topiki kwa kumuonyesha picha ya korosho kuliko riwaya ya korosho na mkatie vipandevipande MUWA ili asione uvivu kula miwa.
Kama ni mwanamume wa umri fulani, ni rahisi kujua kuwa hata bila ya kumuuliza ni mara kadhaa anafikiria mwanamke na yahusianayo na uke na kirahisi atakuwa rafikiyo ukiongelea matiti na uke.
Kama unamjua aliyezoea kulalamika , jifanye unaelewa alalamikacho halafu na wewe KILALAMIKIE.
Kama anapenda UDAKU rahisisha ujumbe kwa kuwa anaweza kukubishia wewePROFESA WA SWALA kwa vigezo alivyosimuliwa na MWANA SHULE YA VIDUDU.
..... na kwa kufanya utarajiwacho kufanya ikiwa ni katika kumlenga mlengwa ili akusikilize, bado UNAJIPUNGUZIA UHURU.
Kabla sijagusa KIINI cha KIDONDA, ngojea nianze kwa kusema;.......
Kumbuka tena wote tunaongea ingawa UNAMSIKILIZA zaidi kwa HIARI na UHURU aongeaye upendayo KUSIKILIZA!:-(
Kumbuka kila utembeapo unakutana na MAMIA kama sio MAELFU ingawa unamuona na kumkumbuka uliyemuona katika mamia KWA UHURU ni yule ULIYEMLENGA KUTOKANA NA AKUGUSAVYO ingawa aliyepembeni yake labda ndiye mwenye jibu la TATIZO LAKO hata lile la UKAME!
Kumbuka ukiwa huru, ... .... uhuru hauna maana, na neno UHURU halitakuwa katika MSAMIATI WAKO.
Na,... ..... usipoangalia unaweza kuendelea kudhani watumiao hizi teknolojia mpya za KUHABARISHANA kwa uhuru kuwa wako HURU kwa kuwa wanasema WEWE USICHOTHUBUTU KUKIONGELEA HADHARANI.!:-(
Na labda,... ..... waandikao au wawekao video zao kwenye neti, wanatumia tu zaidi UHURU WAO WAKUTOKUWA HURU!
Swali:
Kwani ni tatizo kutotumia uhuru kama uko HURU?
Uko huru kwenye INTERNET kama usivyo huru mtaani?
NIMEACHA!
Pumzika kwa hizi Motivational quotes..
na Bill Withers adai tena -Aint no sunshine when she is gone
Kama asiyelewa ndiye haelewi mlevi kuna uwezekano asiyelewa haelewi hata yake aaminio hayana ULEVI!
KAMA unalewa,.... ....labda usiamini wasiolewa kwa kuwa kuna MTAZAMO unajua hawana.
Na jihami na asiyelewa anayekojoa pembeni ya barabara !:-(
Na,.... .... ukimfuatilia ASIYELEWA anaweza kukusimulia hata CHAI wakati hana jibu ukimuuliza ni nini LADHA ya chai.
Swali:
Unajua ladha ya chai ni nini ingawa labda hata huwezi kutungia shairi chai na HUJALEWA?
Na ni kweli,... ... WASIOLEWA ndio MAJORITI ya waliofikia UTAALAMU wa kujiua wa KITALIBANI au kwa sababu za kuamini bila kuamini kuwa wamelewa na wasivyoita ULEVI, wanaamini mpaka hata yale YASIYOAMINIKA kama yale waitayo DINI. Swali:
SI unakumbuka kuna walewao NYUMBANI na kunajisi ingawa alalamikiwaye kulewa ni arahisishaye kujulikana mlevi kwa kunywea pombe baa?
Unakumbuka washindwao kutatua matatizo ya nchi karibu wote hawajalewa na wafanyacho hakieleweki hata na haohao wasiolewa?
Kumbuka sisifii ulevi hapa na bado POMBE SI CHAI!
DUH! Ngojea tu AWILO LOMGOMBA azungumzie-COUPE BIBAMBA....
AU ngojea turudi tena JAPANI kukutana na HIKARU UTADA aongelee kitu katika wimbo uitwao - Boku wa KUMA
Labda kuna KITU unafikiria .... ....ndio maana kuna mwili UNAKUVUTIA!
Kuna kitu unahitaji shikilia.... .... ndio maana HATA umbo la kitasa ni la KUVUTIA.
Na katika umbo unalokimbilia.... ...... LABDA ni kwa ahadi zake unahisi mimba itazaa watoto WANAOVUTIA.
LAKINI mpenzi ni hata atakayekimbilia... .... MANOTI-PESA kama hilo ndio sehemu la umbo lako LINALOVUTIA.
NA hata uzuri wa ROHO ukikimbilia..... ....umbo la nje lidundishalo moyo bado LINAVUTIA.
NA jifariji hata na ufunguo wa kufungulia...... ..... na uhitajilo umbo la mwili ,bado linashabihiana na tundu la ufunguo USIOVUTIA.
NA mpenzi endelea kumkimbilia.... .... wakati ukikumbuka ukipenda, hata NYANI ANAVUTIA. -----------------------------------------------------------____-----
Swali:
AU?
Unauhakika kichwa cha habari hii si cha kijinga ingawa labda ndio kilichokusaidia wewe usiyemjinga kutaka kujua naongea ujinga gani?
NIMEACHA! Tulia na DEPECHE MODE katika-PERSONAL JESUS
Au KANYE WESTWAKINAMNA ahubiri kuhusu ya- GOLD DIGGER!
Pamoja na ubora wa MUNGU WAKO, kuna wenye MUNGU KIBUYU na anajibu tu kama MUNGU WAKO ndio maana kunaulivyoomba na hujapata. Swali:
Si umeshawahi kumuona MPAGANI wa KICHINA akipeta?
Umestukia kitu pale Taifa lenye MUNGU wainafulani na mpaka pesa iliyoandikwa IN GOD WE TRUST likisaidiwa na Taifa la kikomunisti kama CHINA lisilokiri kuna MUNGU waaina fulani?
Ni MAPUNGUFU na UDHAIFU wa ya kibinadamu usababishao binadamu hata ambao HAWAJASIMULIWA KUHUSU umuitaye MUNGU na uendeleaye kujitahidi kumjua ili abakie kuwa ndiye MUNGU WA KWELI ,waanze kuhisi labda kuna kiumbe chenye nguvu zaidi kuliko binadamu chenye uwezo wakuleta unafuu kwenye ya KIBINADAMU yenye udhaifu wa mpaka kufikia BINADAMU kutokuwa na uhakika wa mpaka kutojua kama ni kweli leo SIMON akilala labda hata AAMKA!.:-(
Swali:
Hivi unauhakika MUNGU sio KIUMBE?
Unauhakika MBUNG'O na KUKUNGUNI wanakuona umbo lako zima wewe BINADAMU na kiganja chako sio ulimwengu wa SISIMIZI?
Ngojea NIRUDIE!:-(
Labda ni kweli,.. ... mapungufu yako ya kibinadamu ndio yanasaidia kukuhakikishia MUNGU! Na jinsi unavyoendelea kutishika na mapungufu ya ubinadamu wako ndio unavyoneemesha na kustawisha MATEGEMEZI yako ya MUNGU. Swali:
Unauhakika kwa kumuomba MUNGU humtegei MUNGU afanye hata UWEZAYO kufanya?
Unauhakika ungeamini kuna MUNGU kama usingekuwa na udhaifu wa KUTISHIKA?
Nimeacha na kumbuka ninawaza tu hapa!Tubu lakini kama UMETISHIKA!
wiKIEndi nJEma!
Ngojea basi tumsikilize huyu MCHUNGAJIRev ANN HOLMES REDDING adai kuwa amekuwa MKRISTO mzuri kwa kuwa MUISLAMU
Au tu turudi NIGERIA kukutana na FEMI KUTI adai-BENG BENG BENG...
LABDA,... .... huwezi kuwa huru DUNIANI kama nia yako ni kwenda MBINGUNI!
Na labda,... ... walio huru ni wale wafanyao DHAMBI kwa uhuru wakijua ni DHAMBI!
Na,.. ... huwezi kuwa HURU NA YAKO kama nia ni kutunzia mpaka NDUGU, JAMII na MUNGU heshima!
Na labda,... ... kutunza kwako HESHIMA ni aina ya UTUMWA!:-(
.......utumwa wa kujaribu KUTOVUNJA heshima!
.......utumwa wa KUHAKIKISHA unaheshimiwa!
.........utumwa wa KUTAKA uheshimike!
Na labda,... ... kutafuta elimu ni kukiri HAUKO huru!:-(
HAUKO HURU na ujinga!
HAUKO tu HURU!
Na labda,... .... kuelimika ni KUKIRI kunakitu HUJUI na kwa kujua HILO unaongeza UHURU wa kujaribu KUJUA.
LAKINI pamoja na yote labda ,... ..... haiwezekani KUJUA , na huwa tunajaribu tu kujua MAZINGIRA HAYA yakiruhusu ya mazingira haya, ingawa MAZINGIRA YAKIBADILIKA ujuayo ndio USHAHIDI ukutambulishao kuwa HUJUI.
Swali:
Uko huru?
Unakumbuka kuna starehe pia ya kukosa uhuru kama huhitaji kuwa huru?
Na,.... .... kama kuna kitu UNALAZIMIKA hata kama ni kulazimika kuamka, LABDA hauko HURU!:-(
Kumbuka ninawaza tu! ALHAMISI NJEMA!
Pumzika kidogo na Idi Amini mtu wa famili, kama una muda.
Au twende tu REUNION kukutana na Granmoun Lele aseme - Soleye
YA MUHIMU na YASIYO MUHIMU hutenganishwa na mpaka ULIOKONDA.
Na,.. .... unaweza kupoteza UMUHIMU kwa KUPOTELEA katika YA MUHIMU.
Ni kweli,... ... mambo ya muhimu yanahitaji muda wako INGAWA unaweza kupoteza UWEZO WA KUSTUKIA umuhimu wa ya muhimu kwa KUBOBEA SANA kwenye ya muhimu mpaka UKAPOTEZA NI KWANINI MUHIMU!:-(
Kumbuka KUBALANSI umuhimu wa YA MUHIMU na YASIYO MUHIMU kama hutaki KUPOFUA jicho lako la maisha katika YA MUHIMU hasa hapa duniani PALIPOJAA yasiyo MUHIMU.
Kumbuka,... ....yasiyo muhimu ni MUHIMU kama unataka kutunza afya ya MUHIMU!
Na kukazania ya MUHIMU tu sio AFYA!
Swali:
Au?
Tulia na MLIMANI PARK ORCHESTRA kwa hisani ya tizedboy na kibao - MV MAPENZI
KUNA sababu kwa nini SENTENSI ''NIVULIE SHATI'' haina mvuto kwa MTU FULANI kama sentensi ''NIVULIE CHUPI'' ingawa kwa KIISLAMU kitovu kikionekana nje au MAGOTI yakishuhudiwa bila kufichwa na BICHI KOMA, basi wewe OFISHALE uko UCHI!
NA,.. ....KATIKA SIMULIZI za uvivu na kama jinsia inafaa kibandiko AU ombi LA;........NIVULIE CHUPI kuna uwezekano una CHUPI ndiomaana unataka kuhakikisha kama ni kweli naongelea CHUPI!:-(
Dini NI nzuri kwa sababu inatusaidia kutofikiria SANA katika DUNIA HII ihitajio KUFIKIRI KUBWA KULIKO kwa kutufariji kwa kutupatia WALE tuambiwao kuwa YAO ni KWELI na UKIAMINI ni KWELIKWELI. :-(
Unaweza kumbishia Mtakatifu SIMON KITURURU kwa sababu hujaambiwa au KUFUNDISHWA na umuaminiye kuwa SIMON KITURURU ni MTAKATIFU na anabikira ya TONGOTONGO.
Lakini labda,... ...kwa jina la Papa MTAKATIFU asiye wa Kikatoliki au wa KINZABANGA Simon KITURURU, katika dini yake ukiifuata anaweza akawa anasema ukweli wakitakatifu kuwa UKIPEKECHA,...
.....huwa inapata JOTO katika MPEKECHO.
Swali:
AU?
Kwa wakuulizao au kukushauri jinsi ya kutumia KONDOMU, unauhakika wanajua staili yako ya KUDINDA?
Unauhakika naweza kukushauri jinsi ya kutumia jiko la kuni wakati sijui kukata kuni wala jiko la kuni?
SIKUBISHIII!:-(
Lakini,... ... kabla hujachapwa KIBAO kama RAIS MWINYI kwenye maulidi kwa kushauri watu wavae SOKSI,.... Swali:
UNAJUA sababu za ukiwa na GOVI unadaka MDUDU na kumehakikishwa kisayansi unadaka ZAIDI KULIKO ukila bila KIFUNIKA KITUNGUU? Kongoli CIRCUMCISION vs AIDS
Unauhakika matumizi ya kondomu ni yako kama hudindishi kidindacho kwa manufaa ya KIDINDACHO kuhifadhiwa kwa muda kwenye hifadhi-KIPENYO kama unadinda?
SIKUBISHI kama wewe nimsikilizaji wawasio tumia koroboi wakufundishao kutafuta MBU wako wapi na koroboi!:-(
JINYIME TU kumkojolea kama unauwezo wa kujikojolea! DUH!
Swali:
AU?
Nani kakuambia kuwa kuna akojoaye wakati BADO hakuna ateteaye mharisho hata wa KIPINDUPINDU ufananao na maji ya mchelemchele kuwa ni mkojo kwa sababu za kufanana rangi na mkojo kwa sababu za ujasiri wake wa KUPITIA njia ya mkato ya nyuma??
NIMEACHA! NAwaZA tu MKUU na samahani kama ninakukwaza wewe MSTAARABU ujuaye kuchagua yakuongea HADHARANI!:-(
Tutulie kwa kwenda SOUTH AFRICA kupata tena AFROPOP na NANA COYOTE..
Au twende tu Rwanda kwa MWANADADA nimzimiaye arudishe kiswahili katika bomba la wimbo ...sikilizia basi SOMIaongelee-INGELE
UKIHISI wanafanya SIRI ya TOBO,... .... unaweza TAKA KUWACHUNGULIA wenye tobo hata kama MBELE ya TUNDU kuna hata kishimo chenye SIRI YENYE TOBO ujuayo, INGAWA KWAO ni tundu wasiloridhika nalo ingawa hutambulika kwenye MACHO kwao kuwa ni TOBO.:-( Na,... ... kuchungulia BADO ni kuangalia HATA KAMA ni kwa SIRI na unajificha kwa WAO unaowachungulia.
BAFUNI au CHOOONI hakuna siri kama SEBULENI hujawahi kustukia ndio UNAHITAJI kuchungulia kama ni muhimu NA ,.... ........ huleta BARAKA za MCHUNGULIO kama wewe umestukia siri zifaazo kuchunguliwa HUCHUNGULIWA ila HUJASTUKIA siri ziko wazi na LABDA ,....
....ziko SEBULENI ingawa huchungulii bado kwa kufikiri sebuleni si PAKUMCHUNGULIA wakati anaoga bafuni!:-(
Swali:
AU?
Kumchungulia MTU ni yako SIRI ingawa waweza MPAKA kumstukia MUNGU pale YAKIBINADAMU ukichungulia. Swali:
Au?
NIMEACHA! NAWAZA TU KUMBUKA!:-(
Jikumbushe baadhi ya maana ya LOOK au Peep Tutulie kwa kurudi TANZANIA kukutana na MATONYA aongelee kitu- TAXI BUBU