Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

FARAGHA!

>> Saturday, March 27, 2010

[Tahadhari  : Wazo limepinda!:-(]


Tatizo la FARAGHA,...
... ni kwamba hurahisisha mpaka  LILE TATIZO ULIJUALO LINAMKERA MHESHIMIWA liwekwe pembeni kwa kuwa kuna FARAGHA na kufanya lile tatizo ambalo hujui mtu analo likawa ndilo LINAPEWA KIPAUMBELE ambalo ni la MHESHIMIWA kujiangalia  uchi kila nafasi ikitokea kutokana na kukwazika kwake ambako HADHARANI hakujulikani,...

...kuwa  MHESHIMIWA anajihisi ana uchi wenye sura mbaya kitu ambacho  ndicho kimpacho MOTISHA NA nguvu ya kukivulia gwaguro ilia KUJICHUNGULIA  kuliko ILE MOTISHA YA KUDAI HAKI YA MNYONGE  Mheshimiwa AJULIKANAYO KUITETEA  kwenye hutuba zake zisizo kuwa  faragha.:-(



LAKINI  uzuri wa FARAGHA,...
...ni kwamba  inaweza kukufanya UTULIE na kufikiri VIZURI jinsi ya kutatua MATATIZO YAKO na hata  YA DUNIA  kwa kuwa haubughuziwi  na WAKUDA hapo KWENYE faragha.:-(

Swali:
  • Kwani unabisha kuwa kuna watu FARAGHA ZAO huzitumia zaidi kufanya vitu vyenye undugu na KUNUSA chupi zao ili kujihakikishia ni kweli mkojo wao ukivunda haunuki vibaya sana  kuliko WAFIKIRIAVYO watajiinuaje KIMAISHA wakati  maisha mazuri yanapendelea MAFISADI?

  • Unauhakika aamuaye kuloga mtu huwa anawazia hilo FARAGHANI au katika kijiwe cha wachawi?
  • Unauhakika FARAGHA yako huwa unaitumia kufanya vya faragha au unaitumia ZAIDI kuwaza maswala yenye undugu zaidi na kitu kama  kati ya KITUMBUA na MAANDAZI nini ni TAMU TAMU KAMA SUKARI zaidi?

FARAGHAAAA!
NI kweli mawazo YA MTU  yasingekuwa  YA FARAGHA labda tungestukia MHESHIMIWA sasa hivi umuaminiye kwa ufundi wa kusali,....

...SASA HIVI   anafikiria kikojoleo na baada ya hapo wazo HILO ,...

....kitakacho hitimisha siku ni lile WAZO lake la kila siku la kufikiria UBWABWA na wala sio jinsi gani Tanzania itapata umeme wa kuaminika  au wataunyimaje UKIMWI usinenepe kama ifikiriwavyo na wamheshimuo MHESHIMIWA wafikiriavyo ndivyo MHESHIMIWA anafikiria.:-(

HILI NI WAZO TU na halijafanyiwa utafiti wa kina  kwa hiyo  kifaraja unaweza kulitukania ZAIDI ya SHENZI.:-(





Hebu Matonya abadili kwa kuongelea-Spair Tairi






Diamond alainishe zaidi kwa ndude-Kamwambie




Hebu Isley Brothers waje live na kitu -Between the Sheets



Au nimuachie tu na Notorious B.I.G a sample Between the sheets na kuifanya kitu kiitwacho  -Big Poppa

1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 9:11 pm  

mmmmmhhh:-(

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP