Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

SANAA ya KUAHIRISHA ugomvi mpaka WAGENI WAONDOKE!

>> Saturday, March 13, 2010

Ni sanaa kuutafutia UGOMVI muda na MAHALI pake,...

....NA labda  uaminivyo MAJIRANI ZAKO daima WANAFURAHA  ni kwa kuwa tu WANAPATIA  kuahirisha MUDA WA ugomvi  au tu hualikwi KATIKA sehemu yao MAALUMU  wapendeleayo kutekenyea UGOMVI.

Swali:
  • Unabisha?

Kwa bahati MBAYA,...
....wakati unatembea na ugomvi KICHWANI unaweza mpaka ukawa mchoyo  wa NANIHII kwa hata wasiohusika na UGOMVI wako na NANIHINO.

Na  kwa bahati MBAYA,...
....ni sanaa kuahirisha UGOMVI mpaka wageni waondoke kwa kuwa  yaweza kusababisha TOPIKI zote uongeazo na wageni zijae KUBARAGUZA tu na wala hazikuchokonoi KUMAANISHA kweli kuwa nanihiii ina.NANIHINO.:-(

Swali:

  • AU?


Na kwabahati MBAYA,...
.... labda kama WEWE unaweza kukaa MKAO  wa kusubiri WAGENI waondoke ili UGOMVI uendelee yawezekana ndicho kipimo kikubwa kuhusu USTAARABU wako.:-(


Swali:
  • Unakumbuka sentensi ya kurudishia UGOMVI palepale ULIPOKUWEPO kabla WAGENI HAWAJAJA uitumiayo  baada ya wageni kuondoka?





NIMEACHA hili wazo MHESHIMIWA na labda wala topiki haikuhusu na usikonde HASA  kama hujawahi kuahirisha UGOMVI kwa kuwa SHEKHE na PADRI au TU uwaheshimuo pamoja na MAMA wamekuja kukutembelea.:-(



Hebu GEORGE MICHAEL abadili tena kwa -Careless Whispers



Au Elton John amuongelee tena -NIKITA



Na JIM REEVES akaribishe katika-Welcome to my WORLD

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 4:51 pm  

Sio utakuwa uongo na kiroho kuuma kusubiri mpaka wageni waondoke na kujifanya hakuna kilichotokea???...:-(

Simon Kitururu 2:18 am  

@Dada Yasinta:Kwani Yasinta ni mambo mangapi unasubiri watoto walale au unayasawazishia chumbani na shemeji?

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP