Kwa kuwa kunauwezekano MWIZI hajisikii ni MWIZI wakati anaiba!:-(
>> Tuesday, March 02, 2010
Kwa bahati mbaya,...
.... UWEZO WA KUNYA hauhakikishii MNYAJI kuwa wakati anakunya ANAJISIKIA anakunya:-(
Kabla sijaanza,....
Swali:
- Unafikiri umjuaye kuwa ni MALAYA huwa ni kweli anajisikia MALAYA wakati anafanya umalaya?
Ndio,...
.... kuna uwezekano MJINGA hajisikii anafanya ujinga ,...
.... ndio maana LABDA ufanyikaji wa YAKIJINGA kwa kawaida  ni rahisi.:-(Ndio,....
.....YAFANYIKAYO Iringa,...
... labda ni yaleyale ya DAR-es SALAAM  kama  hayaoanishwi na IRINGA kwa kuwa KIMPUMU au tu KONYAGI ileweshayo  ni ileile ,...
...na kama UKILEWA HUFANYA UJINGA  waweza kurudia ujinga uleule uliofanya SUMBAWANGA  ukiwa KIBAHA kirahisi.
Swali:
- Si unajua KUUA MTU ni rahisi kwa baadhi ya watu kama wafikiriacho WAKATI WANAUA MTU sio KUUA ila ni kwamba wanampiga tu MWIZI?
Ndio,....
.....kuna uwezekano unachofanya sasa hivi  unakifanikisha kwa kuwa hujisikii na KUONANISHA wewe ULIVYO na WEWE  UFANYACHO,...
... ndio maana kirahisi unaweza kuwa  mahiri katika KAZI YAKO  ya UZIBUA CHOO wakati unajisikia  VYEMA TU kuwa wewe ni  bonge la MKURUGENZI hasa kwa kuwa choo usafishacho ni cha IKULU nasio cha STENDI na jina la cheo chako ni AFISA USAFI.:-(
NI WAZO TU HILI Mheshimiwa na nimeliacha!
AU?
Hebu DOROTHY MASUKA abadili hali ya hewa kwa kitu- IMALI YAMI
DOROTHY MASUKA aendeleze kwa ndude-Kwa Nhingirikiri
Au hebu tu DOROTHY MASUKA arudie pia ndude- TEYA TEYA
 
  
 Posts
Posts
 
 




3 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:
Lakini kweli mkubwa!
Nimekubali Simon.
@Kadinali Ng'wanambiti + Dada Mija: Si utani!:-(
Post a Comment