Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

MUDA fulani KATIKATI ya maisha ni NYOKO hata kwa wa LEO ajisikiaye ni MTOTO MZURI!:-(

>> Thursday, September 03, 2009

[Tahadhari: Hadithi hii labda haimuhusu msichana ingawa imeandikwa kwa kuegemea mrengo wa kiume.:-(]



Kila MTU anamuda wake wa NYOKO katika MAISHA,...
... .. hasa pale UTOTO UZURI inapobidi uishe mbele za watu....
...na ukubwa kuingia na unajua ukubwa NI MWANAHARAMU!:-(


Na kuna MUDA kuna PRESHA kwenye MAISHA,...
..... na ndizo zigeuzazo waliojulikana watoto wazuri na watu....
....kuwa hawahawa uwashangaao kwa wafanyayo UYASIKIAYO na KUSHUHUDIA yageuzayo dunia JEHANAMU.


Na labda ipo siku utampa au utapewa mimba na HILO ni moja katika MAISHA,...
...na watoto wazuri utakaototoa[ Hapa nazungumza kwa mrengo na mtazamo kuwa labda bado hujatotoleshwa au kutotolesha:-(] wasio hata na DOSARI moja ya NYOKO wapendwao na watu...
...kwa DUNIA ilivyo sasa hivi usishangae wakageuka BOMBA LA NYOKO na WANAHARAMU!:-(


SAMAHANI ngojea nilainishe nyoko ya hoja hii!
Nacho jaribu kusema ni:

Muda fulani katika MAISHA,...
....Mtoto mzuri aliyezoea kusifiwa mzuri na watu....
...atakujashuhudia bado KUNA WATU mtu kibao tena ZA KUTOSHA wasiovutiwanaye ndipo atakapostukia JICHO kila mtu analo na hata kama unapenda nyonyo kama soksi iliyojaa maji kwa kuzipapasa , bado JICHO NI MWANAHARAMU!:-(

Na YUPO ambaye MUDA fulani katika MAISHA,...
...atastukia uzuri wake aliyekuwa anauona sana ni MAMA YAKE TU MZAZI na ajipendekezao kwao wanamuona ni mzuri kama harufu ya viatu VICHAFU vilivyoloa jana vya wenye fangasi watu....
... na awapaparikiao , KWA KUPAPARIKA hao watu BADO watadai kidude chake hakiwapandishi HAMU.

Ingawa pia YUPO atakayestukia katika muda fulani katika MAISHA,...
....alichotaniwa na kudhaniwa ni miguu kama za baiskeli SPOKU, matako mny'ong'onyeo au tu lile BICHWA kama tofali na watu....
.... ndio vilivyo kwenye CHATI sasa na kwenye fasheni kipindi hiki ,na sasa ni zamu yake kuchekewa kwa sana na linawavutia WALOKOLE mpaka WANAHARAMU.



Lakini KUMBUKA kuna MUDA katika MAISHA,....
...hata uwe MTOTO MZURI na ni kipenzi cha watu...
... utabaini KILA SIKU UNAZEEKA na MVUTO WA JANA si WA LEO kama UNATUMIA AKILI, na kama hutumii akili USISHANGAE ukijastuka wakati UREMBO WAKO UMESINYAA na WALIONOGEWA nawe JANA leo wamestukia yako IMESINYAA na hunogi tena kama JANA na KIPENGELE CHAKO kwao hakiwapandishi MDADI WA HAMU.


Na katika MUDA fulani katika MAISHA,...
...Mtoto mzuri kumbuka kubalansi ya Ubongo,KIMWILI na ROHO [AU kwa Kichina ya:''MIND,Body & Soul] wakati unahangaika na watu.....
....LA SIVYO usipoulisha UBONGO utaishi ukijisikia mjinga, usipolisha ya MWILI unaweza kufa kwa njaa uko uchi huku bado una nyege, na usiposhibisha YA ROHO, mapungufu yake yatasababisha UZIDI KUOGOPA kujisikia kufakufa na hapo ndipo WAJANJA hawakawii KUINGIZA GIA KUBWA katika kukutishia ya JEHANAMU.:-(

DUH nisikutishe !
Bado Mie MTAKATIFU Simon Kitururu na imani na uhusiano wa kati ya BINADAMU na WATU!



Swali:

  • Bado ya ukubwa hayajawahi kukusikilizisha KUFAKUFA?
  • Unakumbuka dakika hii unaendelea kuzeeka?

NALIKATIZIA WAZO hili NYOKO hapa!:-(!
KUMBUKA TU hili NI WAZO TU Mheshimiwa weye ULIYEWAHI KUWA Mtoto Mzuri huku MAPENGO!

Ngojea Lokua Kanza atulize mcheche kwa kitu-Salle


Au tu Cesaria Evora azidi kutuliza mchecheto kwa kitu-Sodade

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP