Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Anachokumbukwa mteja na MALAYA , baada ya malaya kulipwa na mteja!

>> Tuesday, October 19, 2010



Kunauwezekano  vikumbukwavyo hata kuhusu MAREHEMU,....

..... wala sio vingi sana kwa kuwa AKUMBUKAYE ni mchaguzi wa nini akumbuke kuhusu MAREHEMU,....

....na  labda MAISHA ya akumbukaye  yanavyoguswa na MAREHEMU ndicho kifanyacho anakumbukwa vipi MAREHEMU  hata kwa hayo machache yakumbukwayo.:-(

Swali:

  • SI unajua labda Marehemu Kambona na Marehemu KAWAWA jinsi walivyomkumbuka Marehemu NYERERE havikuwa na uwiano na vyaweza kuwa  viko kinyume ingawa wamkumbukaye ni huyo huyo Marehemu NYERERE?

  • SI unajua  kuna ambao wakumbukacho kuhusu marehemu wala sio MAREHEMU ila ni jinsi UBWABWA MSIBANI ulivyokuwa mtamu?
  • Si pia inasemekana kuna wanafunzi waliowahi kusoma enzi za kuchapwa shuleni ambao wakumbukalo kuhusu MWALIMU ni jinsi alivyokuwa anawachapa na wala sio alikuwa anawafunzanini darasani au tu katika kile kitendo cha kuwachapa?


Ndio,.....
..... anavyokumbukwa mteja wa MALAYA,....
.... yaweza kuwa ni MALIPO kwa kipimo cha shilingi,....
.... ingawa  biashara yenyewe iliyosababisha kuwe na MTEJA na MFANYABIASHARA ya utupu,....
.... ilikuwa na mengi tu yakukumbuka yenye kugusa udhaifu wa SHUGHULIKIO LA SWALA la kitendo cha unyumba,....

.....ambacho labda ndicho kilichoshulikiwa kwa muda mwingi kidakika kuliko lilivyoshughulikiwa swala la kulipana pesa kwa shughuli ya chapuchapu kabla MTEJA hajarudi nyumbani kwa mke wake.:-(

Swali:
  • SI kunauwezekano hakuna zaidi ya vitu viwili ambavyo baadhi ya uwajuao kuwa ni WAKEREKETWA wa KITANZANIA  kwa ya KITANZANIA wakumbukao ni nini Marehemu Edward Moringe Sokoine alifanya kilichosababisha aonekane ni bonge la MFANYAKAZI?

  • SI unajua baada ya kunitembelea kwenye blogu hii unaweza usikumbuke zaidi ya ufikiriacho ni matusi ni nini kingine Mtakatifu Simon Kitururu aliwahi kuongelea?
 Ndio,....
.... upo uwezekano hata ndani ya siku hii SI MENGI yakumbukwayo ,....

..... na kuna uwezekano MKUBWA kuna wahitajio kukunakichwa ili angalau kukumbuka ni nini kisicho na maana ambacho wamenogewa nacho ukizingatia viko LUKUKI  hata kabla sijaingizia UDAKU ambao unamaana sana tu ,....
..... hasa ukizingati UDAKU ni kiburudisho kwa baazi ya WAFANYAKAZI BORA wautumiao kupooza kichwa kwa kuchekelea kusikia tetesi kuna MKE wa WAZIRI anamatako ya BANDIA aliyonunuliwa na asiyemme wake  ambaye anakaa nyumba ya jirani.:-(


Ni wazo tu hili MKUU na nimeliacha!:-(


Hebu moja kwa moja Pharoahe Monch ,Common na Talib Kweli warudie jiwe- The Truth



Pharoahe Monch na STYLES P wakune kidude kwa -My life




Au tu Pharoahe Monch , Mos Def na Nate Dogg warudie tu na kitu- Oh No

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP