Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

WAKATI unampenda sana ASHURA ,....

>> Wednesday, October 13, 2010

... hata akiimba kwa sauti yachura anayebanja,....
.... ni rahisi KUVUMILIA.:-(


Na inasemekana kama unampenda ASHURA hata kwa mwili kipotabo, mashavu ya kumimina na MACHO kama gololi,....
.... katika ulimwengu wa video  , sinema na LUNINGA  aka televisheni,.....
.... nyimbo zake MBAYA  waweza fikiria ni nzuri kwa kuwa unazisikiliza huku ukiangalia anavyokutia dhambi ya matamanio KIMUONEKAN O  kwa kuwa kwa macho tu unahisi yeye mtamu kitu kisababishacho ufikirie na SAUTI yake inavutia.

Swali:
  • Kwani unafikiri ni kwanini WANAMZIKI wengi siku hizi wanavideo za kikahaba hata kwenye nyimbo za msibani?

  • Unadhani kama sauti ingekuwa inatosha Madonna,.......  BEYONCE na RIHANNA wange kaa uchi kidogo ili unogewe na nyimbo zao?

Ndio,....
...... labda MANENO tu HUWA  hayatoshi ndio maana hata YESU ijulikanaye hakuwahi kupigwa picha wala kuchorwa AKIWA HAI kuna wajanja walichora BAADAYE picha ambayo kuna waaminio kuwa ni ya YESU kikweli,....
....ili tu waiambatanishe na UJUMBE wa YESU  wa alikuwa anasema nini ili baadhi ya watu WANOGEWE na waaminivyo kwenye PICHA aonekanavyo ANATESEKA ndivyo ambavyo kiliandikwa jinsi ALIVYOKUWA ANASIKILIZIA MAUMIVU katika mkao wa kusulubiwa.:-(

Swali:
  • SI unakumbuka pointi za MATALIBANI za ni kwanini hawataki taswira ?

Ndio,...
.... hata kama UMPENDAYE ni mme wako,....
..... kwa pendo lako LABDA kuna mengi tu ya kidhaifu HUYASTUKII na wakati huo kirahisi kwa kuwa WAMPENDA anachokipenda wampanulia au tu kumpikia.

Na kama na HUYO UMPENDAYE  tayari ni MKE wako,...
..... labda anukavyo MDOMO ASUBUHI ni moja ya machache usiyostukia kuwa unayavumilia.:-(


Na labda KWA LIMTU likupendalo  hasa lile lenye pendo lako,.....
.... ingawa KIMWANA ni VIBAYA walitanulia lawalawa ya penzi ,....
..... kuna watakao kuambia kuwa hilo kwakuwa limeshanogewa ,....
...KIDUCHU tu hufikisha utamu mpaka kisogoni kwahiyo kama hutoi yote hilo wala KWAKO sio kitu cha KUHOFIA.:-(

Swali:
  • AU?

  • Unafikiri umpendaye ANA CHA ZAIDI SANA ukizingatia kidogo tu kwa kuwa wampenda yatosha kutonesha VIZURI unavyojisikia?


Ndio,...
.... yasemekana kwa KIPENDA ROHO,...
... kidogo TU  yatosha utamu ukizingatia KIPENDA ROHO hufikia hata KULA NYAMA MBICHI.:-(



NI wazo tu hili BI MKORA!

Hebu Marlaw atongoze tena katika - Bembeleza



Hebu na Juliana Kanyomozi na Bushoke warudie-Usiende MBALI




Au tu ALI KIBA arudiye naye-Cinderella

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP