Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Sikiliza LABDA unaweza kuelewa, SIKILIZIA , na labda KWA HILO utapata OGAZIMU!:-(

>> Friday, October 29, 2010

[Tahadhari: Wazo katika TARALILA HII limepinda na linamapengo!:-(]


Tatizo moja LA WATU ni kuwa WANAPAPARA na,....
..... ndio maana  wwanaweza kunogewa kwa papara kama WATANZANIA wawezavyo kunonogewa kwa papara na Waziri  LIYATONGA MREMA kuliko,...
......Waziri MKUU MORINGE Sokoine.:-(


Swali:
  • AU?
  • Samahani kama huzijui siasa za Tanzania na kama hilo linakusaidia kutojua SIASA ya Liyatonga Mrema na Moringe Sokoine si nasikia sikuizi kunakitu kina itwa GOOGLE ambacho ukigoogle unaweza kujua kuwa Profesa Lipumba ni PROFESA kweli?

Kama HUNIELEWI,....


....tulia,....
...na wakati umetulia UKIKUNWA sikilizia,....
..... na akiguna SIKILIZA pia,....

...na labda KISIKILIZWACHO bila PAPARA  katika MAISHA kinaweza mpaka kukuwekea wazi  UDHAIFU WA DINI YAKO PIA katika tu kukuelewesha MACHACHE utakayo ELEWA au tu utakayo kuwa na moyo wa kukubali kuwa umeelewa na hayako kama uyafuatavyo kisa PAPA BENEDIKTI kasema usitumie KONDOMU,...


... hata kwa kisingizio kuna kitu unajua sasa kuliko BABU YAKO kama wanasiasa wa CCM walivyojua hata kabla NYERERE hajafa kuwa kuna kitu  alikuwa anawaficha kwa kuwa yeye IKULU alikuwa anaangalia BBC kwenye TV  tokea enzi TANZANIA kunaaminika hakuna TV wakati wewe TANZANIA BARA  KUWA NA VIDEO ilikuwa noma.:-(


SWALI:
  • SI unajua ni RUKSA kutoelewa TARARILA HII inalenga hasa nini?
Ndio,...
.....sikiliza LABDA unaweza kuelewa, SIKILIZIA  , na labda  KWA HILO utapata OGAZIMU!:-(

NIMEACHA !

WIKIENDI NJEMA kwa kuwa naiunganisha kiKHERI KWAKO Ijumaa hiii kwenye hiyo kitu WIKIENDI kwako MHESHIMIWA!:-(


Tuko PAMOJA!




Hebu SHAKIRA alete -LOCA



SHAKIRA arudie pia -  HIPS dont lie


Au tu  hebu BIG YOUTH awaulize TENA wajifanyao wajanja SIKU HIZI kuwa wakati   SHUGHULI inafanyika mwanzo -Where were all dem boys

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Mzee wa Changamoto 5:53 am  

Kusikiliza ni DAWA.
Ni mahala ambapo MAMBO YOTE HUANZA.
Ukisikiliza unaweza kupata BUSARA na UJINGA PIA
Unajua...
Kuwa kama hutaki kitu hutakiwi kukipa nafasi ya kukisikiliza? Unajua kwanini wale wanaofanya biashara za "impromptu" kwenye malls wanakuwa hawana wateja lakini wanalotaka ni KUSIKIIZWA TUUU?
HUSHANGAI....
wale wengine hawakujui wala kukuhisi lakini wanataka uwasikilize ili wakuuzie vitu kwenye simu?
HUJAONA...
nguvu ya kusikiliza tu?
LABDA...
Ni zaidi ya OGAZIMU
NA LABDA.....
OGAZIMU ni kitu kipendwacho na kama akipataye ananufaika na kuburudika, basi afikirie kuhamisha nguvu hizo za "mnaso" kwenye mengine mema.
TATIZO...
Ni kuwa watu wanatumia nguvu hizi kutenda ya sirini
BADALA.....
ya kutenda ya sirini na nuruni.

NA LABDA....
Nililoandika silo ulilotegemea lakini kuniwaza uniwazako sasa ni kwa kuwa umenipa nafasi ya kusoma nilichoandika (ambacho ni kama umesikiliza nilichowaza)

DUH!!!! Ni wazo kibonge na wacha niachie hapa
TUONANE "NEXT IJAYO"

Simon Kitururu 6:26 am  

@Papaa Mubelwa: Mahubiri yamenuna vizuri kweli!Kifundisho mie umeniondoa UPAGANI na miye sasa mlokole!

Ningeshukuru kweli kama watu wengi wengekuwa wanatekenyeka na neno ki-DEEP namna hiyo na siyo tu kuwa na PAPARA za kusikikia na mila kumeng'enyu wanachosikiliza kuwa hata kama ni nyama ya kuchoma kuwa moja ya utamu wa waipendayo nyama ni damu isiyoiva vizuri, chumvi na labda hata pilipili kabla hata ya mazingira kuingilia kati kuwa wanaililia kwenye sherehe yakuwa wamekatwa jando.:-(

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP