Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Nachosema na UNACHOSIKIA vinaweza visiwe na uhusiano!:-(

>> Tuesday, October 26, 2010

Labda sio unachosema ndio chenye umuhimu,.....
.... kwa kuwa ni kile wanaokusikiliza wanachosikia ndicho  KASHESHE!:-(

Na kwa bahati mbaya si kila asemaye cha muhimu,....
...... husikilizwa na akisemacho kutiliwa maanani moja kwa moja na ndio maana hicho hicho CHA MAANA  kitu akikiongea Mama NTILIE adharauliwaye  chaweza kutopewa umuhimu  ingawa akikiongea hivyohivyo MANDELA kuna watu watasikiliza na kukipa umuhimu kama ubwabwa wa msibani kwa aliyezamia msibani  bila KASHESHE.:-(


Swali:
  • SI bado kunauwezekano nilichoandika na ulichotafsiri baada ya kunisoma labda havina uhusiano?

Naendelea kuwaza....:-(

Lakini unaweza tu  kujiliwaza kwa kushuhudia ulimwenguni katika SHOO BIZ ustaarabu wa watu umefikia wapi kwa kudeku hii promosheni ya Puppetry of the PENIS



Au tu cheki na Puppetry of the vagina

1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

emu-three 10:21 am  

Ndio mkuu, wakati mwingine `hali' za kimaisha zinaweza zikampa `sifa'mzungumzaji hata kama akiongea utumbo. Na watu watamshangilia na hata kumsifia. Eti kwasababu ni `mtu wa watu', kijogoo, au mkuu...,
Lakini utumbo huo akiuongea akina pangu pakavu tilia mchuzi, watu watamzomea na kumwambia anatembea uchi, hata kama uchi wake upo ndani ya chupi!
Ni hayo tu mkuu

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP