Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Undugu wa RATIBA ya MHESHIMIWA ya kwenda MSALANI na msosi MHESHIMIWA aliokula!

>> Thursday, October 21, 2010

[Tahadhari: Taralila hii ina wazo linalocheza zigzag kimpindo katika kupukuchua hoja.:-(]



Kufuata RATIBA ni moja ya kitu kisemekanacho,....
.... kimechangia mwendo wa kinyonga wa maendeleo AFRIKA,...

.... kwa kuwa YASEMEKANA PIA kuwa WAAFRIKA na kufuata RATIBA ni vitu mbalimbali,...
... labda kwa mifano zaidi ili TUELEWE NACHO MAANISHA ni kwamba;...

.....uhusiano wa WAAFRIKA na KUFUATA RATIBA  wawezwa kulinganishwa na ule wa WANAUME wa KIPARE na KUJIPAKA WANJA kama wanawake kwa jinsi usivyoendana , uhusiano wa WAMASAI na uvuvi wa samaki au kufanya samaki ndio kitoweo kwa jinsi usivyoendana, WASUKUMA wa Usukumani na WALI kama MSOSI MKUU wa siku na sio kiburudisho kabla ya chakula kwa jinsi usivyoendana AU TU ni kama  uhusiano wa WATANZANIA kwa ujumla na msosi wa kiheshima wa KIFARANSA ule wa konokono.:-(



Swali:
  • Una RATIBA ambayo unaifuata ambayo ulikuwa unaijua tokea jana kuwa leo Saa tisa ungekwenda chooni au tu angalau  ungekuwa unazima KOMPUTA??
  • SI unajua kwa bingwa wa kufuata RATIBA , siku huwa inatosha kwenda kazini , kupitia kumridhisha HAWALA na kuwa na nguvu pia za kurmridhisha LAAZIZI MPENZI MKE wa nyumbani kwa mgao tosha wa hali , mali na mkuno wa kipele?


RATIBA ni kitu cha ajabu,.....
..... kwa kuwa kwa kung'ang'ania kukifuata chaweza kukufanya MTUMWA wake pia kwa kusababisha baadhi ya vitu uharakishe zaidi mpaka utamu usisikie au tu RATIBA kukuondoa faraja inayotokana na utulivu usiosumbuliwa na malengo ya lini ufikie goli  katika penzi , GOLI KIMAISHA la kutozaa uzeeni .:-(


RATIBA  ni kitu cha ajabu,.....
..... kwa kuwa ukiifuata wawezastukia MIPANGO YAKO ya MWAKA HUU ya kuachana na kuvaa chupi za mitumba inatimia MWAKA HUU na wala sio mpaka ufikie UZEENI.:-(

Swali:
  • SI kunauwezekano nisemalo lina ukweli?



Lakini,....
.... kama tu uijuavyo RATIBA YAKO ya kwenda MSALANI ilivyo,....
.... utulivu wake wawezwa badilishwa sana tu na nini umekula ,....
.... kwa hiyo waweza kuta kunasiku waweza kujikuta umewahi zaidi kuripoti CHOONI kuliko kawaida na KWA MWENDO USIO WAKAWAIDA jichoni mwa waliozoea kukupigia chabo katika mwendo wako wamaringo WAKATI UNAENDA MSALANI huku wakijaribu kupeleleza mipaka ya kificha nyeti aka CHUPI YAKO imepita wapi katika VAZI mwanana,.....

....na kama kwa bahati mbaya huko MSALANI kuna mtu wakati huo uko katika RATIBA za DHARURA za kwenda msalani kama mweupe twaweza kustukia ukigeuka rangi kuwa mwekundu.:-(

Nachojaribu kukilenga hapo juu kwa lugha na stori makini kiwanzabanga,....

... ni hoja kuwa RATIBA huyumba kutokana na baadhi ya tuilishayo siku,...
.... kwa hiyo ukiwa makini na ni yapi muhimu ndani ya siku na kujinyima  kuwa na papara na utakayo  yafanyike kwenye siku ,.....

.... waweza kukuta pamoja na KIBANO na MICHECHETO iwezayo kujitokeza ndani ya siku ,...
.... ukitulia utatunza RATIBA.:-(

Swali:
  • Kwani huoni uhusiano wa unacholisha tumbo na RATIBA yako MHESHIMIWA ya kwenda MSALANI?


NIMEACHA!:-(

Hebu tuendelee na Aaron Neville arudie-Everybody plays the fool



Au tu ngoje Majek Fashek aingilie shughuli kwa kubadili mkao kwa -I am not Tired


Majek Fashek aendelee kwa - Majek Beware



Au tu Jack Radics abadili kidogo na kudinya -Groovin'

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP