Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Katika kuuangalia UTAAHIRA wa NYAU a.k.a PUSI !

>> Friday, October 15, 2010

[Tahadhari: Wazo limepinda!]





Ili kustukia NYAU ni taahira,....
.... LABDA wahitaji kujua tabia ya nyau a.k.a PUSI mwenye akili  TIMAMU  anatabia za aina  gani.:-(




Na tukiachana na YA PAKA SHUME  na kupima hata WA MTU utaahira,....
..... LABDA  wawezagundua  wahitaji MZANI WA UELEWA ukusaidiao kujua LIJAMAA ni taahira sana, LIKO NOMOaka LINA TABIA ZAKAWAIDA  au tu limeshapitiliza na tuuongeleao ni WA MTU ukichaa wa namna gani.:-(

Swali:
  • AU?
  • SI kunauwezekano wakati unazidisha kitu  muda huo kuna kitu unapunguza ili uwe NOMO?




Ndio,...
....LABDA kama hauna KILE,...
..... kwa kukosa KILE inaweza kusababisha unataka sana HIKI.


Nikiwa na maana,....
..... tukiachana na NYAU na kumuangalia mtu TIMAMU,......
..... maisha kama tu UTU huhitaji BALANSI katika mzani wa MAISHA au tu UTU na ukizidisha KILE,.....

......  unaweza ukajikuta unalazimika kupunguza HIKI kingine ili  mzani ukae sawa  ILI  uwe NOMO au kwa lugha ya kitaalamu  UWE mtu wa kawaida ambaye :

  • Siyo TAAHIRA
  • Huna KICHAA
  • Sio MLAFI
  • Hujishindishi njaa tukuone unabonge la figa
  • Husomi kupindukia kutaka kuhakikishia watu unaakili kwa kupasi ambayo KWA BAHATI MBAYA  watu wengine hupasi bila kusoma
  • Sio MGOMVi kwa kuwa una mihasira kedekede kwa kuwa hujiamini na hiyo ndiyo siri yako
  • Unateta sana walao uroda kwa kuwa unaminyege na kikusumbuacho ni kuwa unashindwa kufikiria mambo mengine zaidi ya kituliza ashki.

  • nk...

....ambavyo vyote  vyaweza kuwa  ni dalili ya UTU, mtu , KITU  tu katika  MAISHA  katika MZANI kuna upande umezidi na ndio maana HUJATULIA au UMETULIA SANA kupita kiasi..

Swali:
  • SI unajua Ukizidisha SANA kula ni balaa na UKIPUNGUZA SANA kula nayo ni balaa na ujanja kiafya ni kujulia jinsi ya kucheza na mzani UBALANSI kama lengo ni  AFYA BORA?
  • SI kuna uwezekano kila kitu katika MTU kinahitaji KUBALANSI MZANI kama tu  AFYA ya mtu iitajivyo CHAKULA KINAVYO BALANSIWA ili kama  ni wivu uwe wivu wakutosha kukufanya utake maendeleo na sio  uwe ule uliopitiliza wa mpaka kutaka kumtia pilipili mwenzio kwenye kidude au tu umpe sumu ili naye afe  akose ?






Ndio,....
.... LABDA ndani ya MTU katika UTU wa MTU ,....
.... mzani unatakiwa UBALANSI ,....
.... na kitu kikipungua kingine kitajazia.

Na  kama mzani haujakaa sawa KIAKILI ,....
.... akili zikipungua katika MZANI  waweza itwa TAAHIRA;...
.... ingawa na MIAKILI ikizidi sana katika mzani pamoja na uwepo wa watakao hisi  wewe JINIASI,....
.... wapo  wengi watakaodai wewe ni KICHAA,....

.... ingawa pia  NI KAWAIDA huwa kuna tetesi kuwa AKILI ZIKIZIDI SANA au  ZIKIPUNGUA SANA matokeo yake  NI NGOMA DROO  kwa kuwa KINACHOKUSIBU kirahisi kitaitwa tu jina moja ambalo ni UKICHAA.:-(



Swali:
  • SI labda HOJA niipapasayo labda ina ukweli MHESHIMIWA?

Ndio,....
..... na labda anayejazia kwa KUPENDA kusifiwa sana ,....
....... kilichopungua ni kujiamini katika YEYE na YAKE.:-(



Na anayejazia katika kuweka sawa mzani kwa KUONYESHA UMATI anachukia  MABASHA sana ,..
... labda ni msenge kwa mbaaali na afichayo kwa jazba za chuki ZA MABASHA hadharani YOTE ni katika kuficha usenge  wake KITU AMBACHO  ndiyo siri yake.:-(

Na ajaziaye kwa kutaka tujue KAOKOKA sana,....
.... labda ANAJIJUA anadhambi sana zimsumbuazo na hapa siongelei zile zitokanazo na ahisiwavyo kuwa gizani kakubuhu kwa UMALAYA na  UTOAJI JICHO  bila kubembelezwa sana kitu kimfanyacho  KINONIHINO  awe na wateja  KATIKA WATEJA wake ni wa aina yake.:-(




Na ajaziaye sana  kwa kujaribu sana ajulikane ANAJUA sana,....
.....LABDA ajaziacho  ni utupu  wa ajisikiavyo kwa kutojua na MAKELELE YOTE ni kuficha asivyojua  ambacho ndicho kimuondoleacho kutojisikia HAJUI  ambacho kunamfanya asijiamini kitu ambacho ndiyo siri yake.:-(

Swali:
  • Unauhakika wewe UMEBALANSI au kuna lililoegemea upande mmoja sehemu katika UTU, vitu na MAISHA yako?

  • Na si unajua  NYAU anaweza kudhaniwa ANAMTINDIO WA AKILI  kama NYAU HUYO haijulikani  moja ya tabia zake za kawaida ZA KIPUSI  ni PAMOJA na  kufukuza SAMAKI NCHANGA aka PANYA BUKU kama atapimwa kwa mzani wa KIUTU  ambao KWA MTU  unadai  ufukuzaji panya buku  kwa MTU  ni moja ya dalili ya mtindio wa akili?

Ndio,.....
.... UTAAHIRA wa NYAU unahitaji  ujuzi wa NYAU la sivyo ,.....
..... hakuna  uwezekano wa kirahisi wa kustukia NYAU aka PUSI  yupi anatabia za kawaida na NYAU yupi ni TAAHIRA .

Na katika MZANI,....
..... HIKI kikipungua kunamatokeo yake tu na HAYO waweza kuyastukia katika MATENDO YA NYAU katika kile.:-(

Swali:
  • Si unajua WANAWAKE walao UDONGO wakati wa MIMBA ni matokeo tu ya UPUNGUFU wa kitu fulani ndio maana unaweza kuwa ulistukia walikuwa HAWABWII udongo kabla ya kupigwa chini na kuvimba juu?



SAMAHANI kwa WAZO DHAIFU  nikiamini unakumbuka KUTOLIELEWA ni RUKSA Mheshimiwa!:-(


IJUMAA na WIKIENDI NJEMA MHESHIMIWA!
BWANA na BIBI wasifiwe! AMEN!

Hebu Patience Ibembo aingilie kati shughuli na kutonesha kidonda kwa - Sentiment



Twende tena CUBA tena Los VAN VAN wanyuke tena-Aqui el que baila gana




Au tu DJ Jazzy Jeff na J-live  wabadili mkao kwa kuongelea umuhimu wa -Practice

1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

chib 7:36 am  

Mkuu, hapa umeniacha, napiga bongo nikupate vizuri.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP