Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Wakati tunamkumbuka Nyerere, ....Rashid KAWAWA OYEE!

>> Thursday, October 14, 2010

Wakati tunamkumbuka NYERERE,...
.... ni muhimu pia kukumbuka yasemekana KAWAWA ndiye mmoja wa waliyekuwa KIBOKO katika kutekeleza ya NYERERE ambayo yanasaidia NYERERE anavyokumbukwa sasa.,....

.... na kama unabisha waweza kushauriwa angalau wakati NYERERE anaongelea VIJIJI VYA UJAMAA ni nani hasa alikuwa anatekeleza kiutekelezaji na si maneno ili viwepo vijiji vya UJAMAA.:-(


Kwa kifupi:

...Kila PAPA JOHN PAUL II  kuna Kadinali Joseph Alois Ratzinger wake ambaye PAPA JOHN PAUL akisakizia mbwa a.k.a kidogi ; shikashikashika 
- Ratzinger anang'ata mtu.


Swali:
  • SI unajua tukichukulia kuwa DR Slaa ni RAIS WA TANZANIA anaweza akawa ni BOMBA la muongeaji na bila MTEKELEZAJI chadema itagundulika kuwa haina meno katika kung'ata?
  • Si unajua kuwa HAPA najaribu TU kukumbusha kuwa MAFANIKIO ya NYERERE labda kuna umuhimu yakiwagusa na ambao walikuwa mstari wa mbele KIUTEKELEZAJI kuhakikisha PAMOJA NA MENGINE MENGI labda ni pamoja na kufanya katika  kabila lenu CHIFU hana nguvu kikweli kitu kilichosaidia wewe sio mkabila sana kama Waganda?

PUMZIKA VYEMA Kingunge NYERERE na ASANTE KWA YOTE ulioufanyia UTANZANIA na TANZANIA!

Mie  moja kwa moja naenda kumsikiliza Dr REMMY akitonesha kidonda kwa kuzungumzia-KIFO

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

EDNA 12:59 pm  

Daima tutakukumbuka Nyerere.Tanzania uliyoiacha si hii ya sasa, mambo ni shagalabagala...kiufupi mambo si shwari babu.
R.I.P

Yasinta Ngonyani 1:05 pm  

Tutakukumbuka daima na daima. Utuombee nasi kwani wote tutakuja huko.Ustarehe kwa amani!!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP