Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Tanzania NDOTO iko hai au NDIO imeshageuka JINAMIZI?

>> Friday, July 01, 2011

Kama ndoto ilikuwa ni kupata UHURU,...
.... baada ya UHURU,...
.... ndoto ihai au imeshageuka JINAMIZI?



Kama NDOTO ilikuwa ni kuwa na VIONGOZI wazalendo,...
.....ndoto ihai au ishageuka JINAMIZI?


Kama ndoto ilikuwa maisha bora kwa kila MTANZANIA,...
.... ndoto ihai au imeshageuka JINAMIZI?



Ndio,...
.....JINAMIZI ni ndoto BADO,....
... ila TANZANIA kama NDOTO ,...
... je ndoto hii sio JINAMIZI?


Nawaza tu kwa SAUTI!:-(
Ijumaa na WIKIENDI NJEMA!

Hebu tugawiwe Dream a Little Dream kutoka kwa- Louis Armstrong




The Golden Gate Quartet waingilie kati kwa - Nobody knows the trouble I've seen





Au hebu tubadili kwa kwenda tena Senegal ili Daara-J wakumbushie tena - Slavery




Halafu Konshens kwa kubadilisha wamalizie tu kwa - Insanity

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

emu-three 12:07 pm  

Juzi mkuu tukiwa ndani ya daladala wengine tukiwa tunapaka rangi(tumesimama, hatuna siti)..kukawa na mjadala, wengi walikuwa wakisema kuwa ni heri tusingepata uhuru, tuendele kutawalia, kwani maendeleo yangekuwa makubwa...hutamini wanaoongea hivyo ni wasomi..
Hivi nini maana ya Uhuru? nikajiuliza kichwani na swali hilo likajibiwa hata kabla ya kuuliza kuwa uhuru ni hali ya kuwa na uwezo wa kujitegemea, na kutotawaliwa kwa aina yoyote ile...sasa je tuna uhuruu huo? ...mjadala ukawa mreefu, na ndipp nikawasikia hawo jamaaa wakisema ni heri tusingepata uhuru mapema kwasababau sasa ndio tunatawaliwa ile mbaya...kwa vipi nilishindwa kuelewa, kwani haiji akilini!
Hivi watu wanajua kutawaliwa kweli?mpo kwenu mnaambiwa msiendee choo hiki ni cha wadhungu, huku ni kwa bwana wakubwa, msitembelee mitaa hii kwasababu ni kwa wakubwa, msifanye hiki na kile kwasababu hamstahili...!

Simon Kitururu 5:54 pm  

@Mkuu M3: Yani we acha tu! Inasikitisha sana ukifuatilia mambo yetu lakini!:-(

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP