CHUPI ibanayo, bado INABANA hata kama haichaniki kwa kuwa aivaaye ANAPATIA STAILI ya KUINAMA!
>> Thursday, December 03, 2009
NDIO!
....Ni suruali ILIYOBANA na sio CHUPI ambayo kwa kawaida NDIYO  ishuhudiwayo NA ASIYE KIPOFU ikitatuka wakati   MWENYE TAKO  hata AMBALO HALIJANUNA anainama kuokota kidude,...
.... na KATIKA HILO pia kwa kawaida  ABANWAYE na PEKOSI  au tu KIFICHA NYETI  anajua NYUPI  au  SURUALI YA KODRAI BWAYA YA MTUMBA  haikuanza kubana makalio wakati huo IKITATUKA na KUNAUWEZEKANO  ni staili tu ya kuinama iliyochana KISUGUA NYETI  muda HUO:-(
NDIO!
...Chupi a.k.a KIFICHA NYETI   au SURUALI AINA YA PEKOSI YA MTU   iliyobana NYUMBA YA MILANGO YA HAJA KUBWA NA NDOGO  itatukayo mtu akibinuka kuokota kidude,....
... mara karibu zote SABABU ZAKE ZA KUTATUKA au kuchanika  KWAKE  ,sio kwa kuwa inabanwa  na tako KIBONGE hasa  tu KAMA UTACHUNGUZA VIKOROMBWEZO VINGINE  vifanikishavyo CHUPI YA HALIMA/Hamisi , ILE  SAFI , mbele ya MNUNIO WA KITU SAFI a.k.a MLANGO WA  KIDONGOLOSO  WA NYETI kama vya umadhubuti wa kitambaa ,NYUZI na kadhalika kadhaa  wakati wa mtatuko HUO:-(
Ngojea nilainishe kachori:
Na maana kuwa  WAKATI unakosea kosa moja, kunamlolongo wa mambo yaliyoko nyuma ya hilo tendo ukosealo NDIO MAA UMEKOSEA HILO NA SASA HIVI.:-(
Kielelezo :
- Kwa mfano kama KOSA LAKO ni kirahisi unafanya UMALAYA.
- labda tokea mtoto ulifunzwa kugawa na haukustuliwa KUWA kuna tofauti kati ya kugawa PEREMENDE au BAZOKA na MWILI, kimaumbile yako au kibaolojia WEWE kila baada ya sekunde kadhaa badala ya kufikiria msosi UKIWA NA NJAA kwa kawaida WEWE unafikiria sehemu za siri kitu kikufanyacho unakuwa MAHARAGE ya MBEYA a.k.a MAJI MARA MOJA, umechacha na akili zako zifanyavyo kazi na mazingira uliyokulia YALIVYOKUFUNZA yamekufanya uamini kujifunza ufundi seremala ili uishi na kulaliwa na kupewa UTUPU uupendao tu halafu unalipwa KATIKA HITIMISHO ukahitimisha ni rahisi kulaliwa au kubinuka kuliko kuchonga vinyago.:-(
- Kwa mfano kama kosa lako katika kuwakilisha RIWAYA lilisababishwa na kukosea UNG'ENG'E' a.k.a KINGEREZA.
Siri ya kwanini UNG'ENG'E KWAKO haupandi linaweza lisisababishwe na kitu kimoja tu kuwa una ulimi mzito hasa ukiangalia mlolongo ulio kukumba wa kuwa MWALIMU wako mwenyewe aliyekufundisha Ung'eng'e kwake mwenyewe UNG'ENG'E ulikuwa haupandi vizuri , hujawahi kukutatana na waongeao Kiingereza kwakuwa hata Padre wa kijijini kwenu na marafiki zake WATASHA walikuwa ni WAITALIANO ambao kwa bahati mbaya ung'eng'e ulikuwa unawatoa jasho na HALAFU wanashuka KILUGURU na KISWAHILI utafikiri ni MKUDE, halafu bila kusahau ukweli wenyewe kuwa WEWE NI MVIVU WA KUJIFUNZA MAMBO yaliyoko nje ya UDAKU ,....nk.
NALIKATIZA WAZO HAPA.:-(
Swali:
- Umejaribu kuninielewa naongelea nini Mwanakwetu?
- Kwa hiyo umenielewa sasa KUWA wakati unaharibu hiki , UHARIBIFU WAKO WA HIKI kunauwezekano umechangiwa na KILE ambacho kinaweza kisihusianishwe kirahisi na HIKI?
- Unakumbuka wakati unazungumzia CHUPI moja , unachogusia pia ni ushirikiano wa kitambaa, nyuzi na labda hata rababendi ishikiliayo chupi yako kiunoni ambayo vyote kwa USHIRIKIANO HUO hufanya CHUPI YAKO iwe CHUPI yenye mauaua?
NIWAZO TU HILI Mheshimiwa  na NIMEACHA!:-(
Ngojea Barrington Levy abadilili kama alivyofanya 1984 katika- Here I come
Nimuache juzijuzi katika-Too Experienced
Au nimrudishe tena enzi katika -Murderer
Au tumalizie kwa kwenda Uingereza mwanzo wa Jungle MYuziki katika kitu cha jungle enzi hizo ambacho katika jango miye nikiwa mpenzi wa staili hiyo najua bado ni kikali. Dr Edo Mtafungwa unakumbuka enzi? -
Au ngojea niache picha na wadau Juzi ya jana nilio kuwa nao wakati Mtaalamu Barrington Levy anatunong'oneza.


















 
 
  
 Posts
Posts
 
 




2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:
Leo sijaona picha ya bilauri. Ama ulibanwa sana na chupi ukashindwa kuinama na kuichukua?
@Askofu Fadhy: :-)
Post a Comment