Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Jinsi ya kukabili KUJIJUA!

>> Monday, January 03, 2011

Katika safari ya MTU ya kujijua,......
...... mtu anaweza mpaka  kustukia  mengi  DHAIFU yasiyo rahisi kukiri ndiyo sehemu ya  yeye.:-(


Swali:
  • SI kunauwezekano  katika kujijua kwa MHESHIMIWA MWIZI, mwizi  anaweza kupata taabu kukubali  UKWELI  kuwa yeye ni MWIZI na afanyacho ni wizi mtupu hata kama ni wa KALAMU?

Ila,....
.....labda  kwa KUJIJUA kwa mwizi kuwa afanyacho ni WIZI,.....
....kunaweza kuwa ni msaada  kwa MWIZI katika kusaidia mwizi kuridhika na wizi wake  kitu kiwezacho kumsaidia KUIBA kwa starehe,......
....kwa kuwa angalau  wizi utafanywa  wakati roho imetulia.:-(


NI wazo tu hili!
Naendelea kuwaza.....


Kwa kuwa ni JUMATATU hebu tukumbushwe wikiend na Afro 70 Band katika jiwe-Wikiendi




Au tu ngojea TATUNANE waingilie shughuli kwa-Msewe

3 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Ney 11:00 am  

Duh! Bro mawazo yako ni ya ukweli na yanazidi kunifanya nifikirie mambo kwa undani zaidi,unaweza ukawa unajua una udhaifu fulani lakini kukubali kuwa ni udhaifu ikawa ngumu lakini ukiwa unauona kwa mtu mwingine ikawa ni kero kwako.Heri ya mwaka mpya!

emu-three 2:18 pm  

Kweli mkuu hata mlevi hakubali kuitwa mlevi, kama alivyo fisadi asivyokubali kuitwa fisadi. Ni ubinadamu kuwa hakuna anayependa kuitwa `wasivyopenda watu' hata kama ni `sifa', lakini kwa vile jamii haikubali kuwa ni sifa basi waogopa kuitwa hivyo.
Wakumbuka wapigania uhuru walikuwa wakiitwa majina mabaya, ambayo baadaye yaligeuka kuwa sifa! Nimewaza tu mkuu, tupo pamoja

Simon Kitururu 3:47 pm  

@Ney: Heri ya Mwaka mpya Dada yangu!
@M3: Nakubali kabisa ulilosema Mkuu!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP