Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

UDHAIFU wa stori ya SIMON KITURURU akiiandika Simon Kitururu!:-(

>> Thursday, January 06, 2011

Husemekana stori ya MTU,....
..... ikiandikwa na MTU mwenyewe,....
....kuna mambo hurukwa kwa makusudi.:-(


Na kwa bahati mbaya stori ya MTU,....
..... ikiandikwa na MTU MWINGINE  hata aliyetafiti vipi mambo  hata kama na kundi na sio pekee mwenyewe,....
.... kuna mambo yatarukwa kwa kuwa  KUNA YA MTU anayeyajua NI HUYO MTU PEKE YAKE na mwingine akiyasimulia kuna kitakachoachwa hata kama sio kwa makusudi.:-(


Swali:
  • Kwa hiyo unafikiri kuna MTANZANIA ajuaye stori  nzima ya NYERERE?
  • Na si unajua anayemchukia Simon Kitururu na anayempenda Simon Kitururu wanaweza kuongea stori mbili tofauti kuhusu Simon Kitururu mpaka ukachanganyikiwa  kuwa inawezekanaje Simon Kitururu ni mtu  YULEYULE mmoja? 
  • SI inasemekana kuna mambo mengine KUHUSU STORI YA MTU ajuaye ni KIMADA na sio yule mke wa mtu?
Ndio,...
.... labda hakuna STORI ya mtu aliyoandika mwenyewe ILIYOKAMILIKA kwa kuwa aandikaye ina maana  bado yuko HAI  a.k.a hajachungulia kaburi,...

....ingawa pia hakuna stori IMHUSUYO MTU   iliyokamilika iliyoandikwa na mtu mwingine kutokana na ukweli  ukichunguza utastukia hata wazazi si yote wayajuayo kuhusu mtoto wao WALIOMZAA WENYEWE kama tu watoto wajuavyo stori nusunusu kuhusu wazazi wao  tukiachilia mbali  tu watu wengine.:-(


Ndio,....
....labda kama WAKRISTO waridhikavyo na stori nusunusu za YESU ambaye mambo yake yaliyoandikwa  hatujui  miaka mingi alikuwa anafanyanini kabla ya kuanza kuhubiri ,....
.....turidhike na yale tu machache  tutakayo kujua kuhusu MTU....
... kwa kuwa  labda si kila kitu kuhusu mtu NI MHUHIMU na åpia labda hakuna uwezekano kwa MTU kujua stori nzima ya mtu mwingine.:-(


Nawaza tu  hivi MHESHIMIWA baada ya kukumbuka ushauri wa Rais KIKWETE wa watu kuandika VITABU kuhusu viongozi wao,....
...na baada ya kupata KITABU cha stori ya IDI AMIN ambacho nawasiwasi na UHAKIKA wa stori yenyewe!:-(


NI HILO TU Mheshimiwa!


Hebu Bembeya Jazz National watubadilishie hali ya hewa kwa - Whisky Soda





King Masco arudie- Mao Mao



Au tu na Prince Nico Mbarga amalizie tu tena na-Sweet Mother

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 11:38 am  

Simon Kitururu:-)

malkiory 2:01 pm  

Binafsi sintakuwa na muda wa kutaka kusoma historia ya Kikwete na Mkapa kwa sura ya ujeuri na ubabe na udikta wao.

Nyerere na Sokoine ni viongozi pekee walioacha historia katika nchi yetu. Hawa wengine ni mafisadi.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP