Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Wakati nahisi YA WENGINE ni manono zaidi na NAHISI ukiyabonyezabonyeza ni KITU freshi SANA yani !:-(

>> Tuesday, January 04, 2011

Wakati na WIVU na NATAMANI kuwa kama watu WENGINE,.....

.....ya WENGINE huvutia,....
...... yao yana VYEO, ushujaa na hata NGUO NZURI kuliko mie.:-(


Wakati natamani kuwa kama watu WENGINE,...
....ya WENGINE vitu hupatia,.....
...... yao huonekana YANA MAFANIKIO ZAIDI, nyumba nzuri na hata furaha kuliko mie.:-(


Swali la kujitia moyo:
  • Hivi si labda ni kweli mwenye wivu ni kipofu kwa alionealo wivu?


Wakati natamani ya WENGINE,.....
.... ni ya WENGINE yale yenye kunivutia,......
.... ambayo nabobea katika kuyachungulia  hukutayari AKILINI nimeshajijengea kuwa YAO hayana kasoro kwa kuwa  WENGINE siwachunguzi kasoro katika yao kama nijichunguzavyo mie.:-(



Swali tena:
  • Hivi si kwa ya wengine ni RAHISI kustukia tuyafikiriayo ni MABAYA kuliko YETU au tu yale tudhaniayo ni MAZURI kuliko YETU na kusahau ni jinsi gani hayo yako tu  kama YETU?
  • Na hivi si inasemekana kunauwezekano  ni rahisi  zaidi KUONA ya wengine kuliko yako?


Lakini,.....
.....LABDA,......
..... kwa wengine ,.....
...... yako ni MENGINE,.....
..... na KWAO kwa kuwa hawakujui wanaweza kuwa NAO wanatamani YAKO au tu wawe kama WEWE,....
...hasa kwa kuwa yako yanaonesha kama vile ni BOMBA ZAIDI au angalau tu limpenzi lako ZURI ZAIDI utafikiri halinyi vile.:-(


NAWAZA TU Mheshimiwa!:-(

Hebu tudeku STOMP



Au tu Oliver N'GOMA aingilie tu shughuli kwa - Sal'



Au tu Oliver N'goma aendelee tu pia  na-Julie

5 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 12:55 pm  

nanukuu "Na hivi si inasemekana kunauwezekano ni rahisi zaidi KUONA ya wengine kuliko yako?"mwisho wa kunukuu:- hii nimeipenda kwanikweli kabisa

emu-three 1:34 pm  

Wakati unatamani ya wenzako na wapo wanatamani ya kwako, wakijua wewe yako ni bora kuliko ya kwao. Kuna usemi unasema, ukitaka maendeleo tizama aliye juu na ukitaka ubinadamu tizama aliye chini!

Simon Kitururu 1:40 pm  

@Da Yasinta: Tatizo ni kwamba KWELI ni kitu kigumu kwa kuwa UKWELI saa nyingine ni vile tu vifananavyo na tufikiriavyo ni KWELI.:-(

@M3:Tatizo ni ,....
.... hivi ni nani aliye JUU au CHINI kama tukizingatia utashi wa BINADAMU katika kuamua ni nini kiko katikati ,...
....wakati twajua mpaka kuna aaminiye hapohapo India kuwa MUNGU ni Ng'ombe , mwingine ni ALLAH , BUDHA, Sir GOD au tu ..... kwa mtizamo wa KIBINADAMU wa binadamu aaminiye mzani wake wa kupima mambo uko sahihi?

Yasinta Ngonyani 9:33 pm  

Mmmmhhh au kaaazi kwelikweli!!!

Newton Mudaki 8:28 am  

kweli unawaza. I love this post.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP