Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

TEGEMEO la matokeo katika kuharibu KURIDHIKA kwa mtu na MATOKEO!

>> Wednesday, January 19, 2011

Kama MTU  hana aidia ya nini ANATEGEMEA KIWE  ni matokeo ya kitu,....
..... ni rahisi KWAKE  kuridhika na chochote kile kitu  na ndio maa CHAI isiyo na sukari  ni tamu kwa asiyetegemea CHAI inahitaji sukari !:-(

Swali:

  • SI unajua BIA ni tamu tu kwa hata wapendao chai ya SUKARI hasa kwa kuwa hawategemei BIA iwe tamu kama sukari?

Ndio,...
....labda sio unachofanya,...
.... na ni kile tu UNACHOTEGEMEA KWA KUFANYA,....
....ndicho kilichoko nyuma ya FURAHA ZAKO za matokeo.:-(

Swali:
  • Kwani hustukii kuwa kama HUTARIDHIKA na muonekano wa MPENZI baada ya kukutananaye uso kwa uso baadaya kumjua kutoka kwenye picha zake kwenye FACEBOOK wewe kuna kitu ulishategemea ambacho kwa bahati mbaya KILIKUZA matumaini?



Ndio,...
....utegemeacho kutoka kwenye KITU,...
...labda  ndicho chenye misingi ya mauaji ya TAMUTAMU ya kitu!:-(

NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA!

Hebu twende ZIMBABWE tena kukutana na Alexio na Andy Brown warudie- Shaina



ANDY BROWN aendelee na-Mawere kongonya



Au tu ANDY BROWN amalizie tu kwa-DAISY

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP