Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Hongera WANAWAKE wa shoka ELLEN JOHNSON SIRLEAF, Leymah Gbowee na TAWAKKUL KARMAN kwa kutunukiwa tuzo la NOBEL!

>> Friday, October 07, 2011

Ellen Johnson Sirleaf RAIS wa LIBERIA

Mwanaharakati  wa Ki-Liberia  Gbowee

Mwanaharakati, Mwanasiasa na Mwanahabari waki-YEMEN Tawakkul Karman



HONGERA ZENU  akina MAMA!
Habari zaidi kongoli  HAPA




Ngojea nilolome kidogo!

Tukiachana na kuwa hili TUZO  la NOBEL kama tu kwenye sinema lilivyo la OSCAR mie huzinguka nalo  kwa kuwa huwa naamini kuna ajenda za chinichini ZIKIWEMO zile za KISIASA na KIMIKAKATI ZAIDI  ambazo hufanya maamuzi ya nani ashinde na kwa hilo kufanya  kuna mpaka akina Rais OBAMA kutunukiwa NOBEL  kitu ambacho siamini kama walistahili,....
.... bado  labda lina mchango wake kiaina ukizingatia BINADAMU akihusika katika chochote kile labda bado kitakuwa na mapungufu ya KIBINADAMU!

MWISHO wa MLOLOMO!:-(


Hebu  tubadili  mshawasho kwa kumuachia Dama Ludmila aturudishe tena Luanda ,ANGOLA na kuanzisha upya kwa - Acaba de Dar o Toque






Dj Sottão aingilie kati na -Sentido Silencio



Dj Sottão aendeleze mwanzo wa wikiendi hii kidhambidhambi tena kwa-Moço direito




Au tu dhambi ikae njenje tu katika siku hizi ambazo labda nizamwishomwisho,...:-(


6 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 3:32 pm  

HONGERA ZENU AKINA MAMA...SIKU MOJA LABDA ITAKUWA ZAMU YAKO KAKA sIMON AU LABDA YANGU ...ila sijui nifanye nini mpaka nipate hiyo..LOL

Simon Kitururu 4:47 pm  

@Yasinta:Cha muhimu bado ni kuwa TUZO zuri la kutenda wema amablo ni zuri kuliko yote wala halihitaji mtu mwingine akutunukie!

Kama ni mtendaji wema tayari TUZO unalo MOYONI hata kwa ufikiriayo ni MADOGO kiwema!
Matunzo mengine ya kupewa na BINADAMU WENZAKO yana udhaifu wa KIBINADAMU hata kama tuzo lenyewe ni KUPEWA Utakatifu na PAPA wa KANISA!

Yasinta Ngonyani 5:38 pm  

Simon! ni kweli unajua wengi nikiwa mmojawapo tunasahau ulilolisema: Ahsante kwa kunikumbusha.Ungekuwa karibu...basi naacha.

sam mbogo 7:24 pm  

Wanawake wana weza basi tu kulialia kwao ndo tatizo ila wakinyamaza mambo yanakuwa.hongereni sana wanawake,ambao ni mama zetu,dada zetu, wakezetu,wachumba,nk. Lakini sasa hao kwenye kideo hiyo bwana kitururu dah! ! manake huo muziki mpaka unaacha kunoga unabakia kuwa chabo hao ma dada na vinasa upanti/vichupi mweeee sijuwi ni kijiji gani katika moja ya nchizetu katika bara la afrika.nimependa sana uchezaji wao kwenye maji,wameumbika hakika ni warembo.kaka S.

Simon Kitururu 7:40 pm  

@Yasinta: Tuko Pamoja!

@Kaka S: Mdau moja kutoka LUANDA , ANgola aliniambia hapo ni umbali kama kilometa 30 kutoka Luanda mjini ndiko walikorekodia kideo hiki.

Yasinta Ngonyani 9:35 pm  

Simon na kaka Samam:-(

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP