Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

WAMAREKANI bwana kwa kukasifia kanchi kao bwana- ETI kanchi kao ni ``THE GREATEST PLACE on EARTH!´´

>> Sunday, October 23, 2011

Haki ya nani ukisikiliza WANASIASA wa MAREKANI wakisifia MAREKANI,...
... unaweza kudhani MAREKANI ni nusu MBINGUNI kwa jinsi wanavyopasifia na pia kusifia WAMAREKANI kama wao ni watu bomba sana na SPESHO hapa DUNIANI ,...
....mpaka unaweza kuelewa fununu ZA KITU  hata bila ya  kuhoji WAENDEKEZAO UMAREKANI hata bila kufika MAREKANI kwanini labda kuna  uwezekano WAPO waaminio  WAMAREKANI wakienda haja zitengenezwazo na malighafi CHAKULA,...
... labda watoacho kihaja kubwa ni  karibu na keki au angalau kwa wapenda ubwabwa wanaweza hisi tokeo lao la ya msalani AREKANI AKIENDA KUJISITIRI ni PILAU.

Lakini: 
  • Umestukia ukiongea na MSWISI ,.....au MFINI hata tukiruka nchi nyingine unaweza kukuta na wao wanaamini nchini kwao ndio BOMBA zaidi na wanafundishana hivyo hata katika porojo za hapa na pale na kama kunakasoro wanaamini ni kwa sababu WAGENI nchini kwao ndio wanawaharibia NCHI?
  • Na si unastukia sie kwetu hata kitu kirahisi kujivunia kama Mlima KILIMANJARO tunashindwa kuutetea kuwa uko Tanzania na  nasikia kuna Watanzania kibao kama hailazimiki wanakwepa kujitambulisha kuwa ni Watanzania huko ughaibuni kisa hata waowenyewe wanashindwa kujivunia TANZANIA?



Ndio ,..
... na labda ni JANJA moja wapo,...
..... kujisifia wenyewe hata ki-PROPAGANDA kama wafanyavyo WAMAREKANI,...
...lakini:
  • Ukijivunia TANZANIA ya leo si kunawatakaoamini tu kirahisi UNADANGANYA?
Ndio,...
.... wenzetu hata KIPOROJO za uongo kikuombea KURA ,...
.....wanajivunia sana KWAO na kudai kuwa kwao ni ``THE GREATEST´´!


Ni wazo tu hili kiangalizo MHESHIMIWA!:-(



Hebu Kassav waingilie kati na kubadili mchezo kwa ndude kimchanganyiko yenye -OH, MADIANA



Kassav bado kipaza sauti kikishikiliwa na Jacob Desvarieux wapandishe dozi kwa - Mwen Malad Aw


Hebu ndani ya KASSAV huyu Jean-Claude Naimro ashike kipaza sauti tena katika- Ave'w Doudou



Ndani ya KASSAV mdada Jocelyne Béroard zamu yake ashike kipaza sauti na kurudisha-SIWO




Au tu kundi zima la KASSAV wazime tu manyanga   kwa-Tim Tim Bwa Sek

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP