Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kama DUNIANI kila mtu angekuwa PROFESA!

>> Monday, May 09, 2011

DUNIANI,...

....ingawa inasemekana kuna mpaka WATEMBEAO KAMA BATA kwenye  mwendo wao wa MARINGO,...


SWALI:
  • Hivi kwani ukitafiti si labda  kila MTU kuna kitu anajua zaidi?
  • Na hivi ni kweli PROFESA wa KITU  ndiye mjuaji zaidi KITU?




Na  katika DUNIA ambayo kila mtu ni PROFESA wa kitu fulani,....

  • Si BINADAMU bado wangetafuta jinsi ya kuona wengine ni MAPROFESA zaidi?



Na DUNIANI kama kila mtu angekuwa MJINGA,...
.... labda WAJINGA wangemteua profesa wao wa UJINGA!:-(




Nawaza tu  MKUU!
Jumatatu njema MHESHIMIWA!





Hebu Sam Mangwana arudishe pini- Mokolo Nakokufa / Minha Angola




Au tu tena Jocelyne Labylle alete tamutamu-Laisse parler les gens


6 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Goodman Manyanya Phiri 3:34 am  

Nilikuwa sijui Profesa hasa ni mtu gani mpaka sasa hivi nilipofanya pekua pekua na kamusi ya Kizungu. Kumbe si lazima awe na Phd?

Nami nitaomba mwaka ujao nipigiwe kura kusudi niwe Prof.

Au kama sio kura, wanapatapataje wenzetu uprofesa huo, watupatie siri kidogo nasi!

Simon Kitururu 8:56 am  

@Mkuu Goodman: Nafikiri kuna MAPROFESA kadhaa mtandaoni ambao tuwasubiri watekenye jibu!

Yasinta Ngonyani 3:39 pm  

Hivi kwani si cheo tu prof. kama vile Dr, headmaster nk...ambapo inasemekana pia ni binadamu kama mimi na wewe na yeye? Hakika kila siku watu tunazidi kuelimishana humu kwenye hizi blog...mmmhh najiwazia tu kama ni kweli....

emu-three 4:49 pm  

Ndio kuna uprofesa wa shule, tunaukubali,...wapo kweli sio mchezo, lakini hata akiwa profesa, sio lazima ajue kila kitu katika nyanja hiyo aliyoisomea..! Au nimekosea ?

Yasinta Ngonyani 6:32 pm  

mmm wala hujakosea kabisa mie naungana nawe...kwani katika ubinadamu lazima kuna kukosea...

Goodman Manyanya Phiri 1:09 am  

Basi wasije wakafanya kosa lakunifanya mimi ndie raisi wakwanza duniani kotekote, la sivyo nitalazimisha asiitwe mtu yeyote yule "profesa" ila tu kama anayo shahada ya DOCTORATE kwisha!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP