Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Leo katika UCHOKOZI: Tatizo AFRIKA sio DINI za KIGENI ukizingatia UKRISTO ULAYA ni DINI ya KIGENI ukiachilia mbali kuwa Wazungu walipoletewa UKRISTO walimbadili YESU kuwa MWEUPE PEE na MWENYE MACHO ya BLUU ili awe MZUNGU MWENZAO ,....

>> Friday, May 27, 2011

 .... kitu ambacho ,...

....LABDA NDIO SIRI ya MAFANIKIO ya KUIGA ya WATU kwa mafanikio,....
.... na waliposhindwa kumfanya Mtume MOHAMMED (s.a.w)kuwa MZUNGU kama WAO  wakafukuzilia mbali UISLAMU,....
..... kitu ambacho,...
.....LABDA NDIO SIRI ya MAFANIKIO katika VISIVYOIGIKA kwa mafanikio yabidi VIFUKUZILIWE mbali!:-(


Swali:

  • AU?

Labda ni kweli  kama unaiga  basi fanya UIGAVYO viwe vyako KIVYAKO  kama walivyofanya WAZUNGU kwenye UKRISTO walioutoa MIDO ISTI/Mitaa ya fulu kubwengana WAARABU na WAYAHUDI   kwa waarabu na WAYAHUDI ,...

....au kama WAJAPANI walivyofanya na MATEKINOLOJIA ya WAZUNGU kuanzia kwenye MAGARI  mpaka nanihii ambacho ndicho CHINA ifanyacho sasa hivi,....

.... na vikushindavyo  ACHILIA MBALI kama walivyofanya WAULAYA baada ya UISLAMU kuingia ULAYA hasa nchi kama SPAIN ambako kwa mamiaka walikuwa chini ya utawala wa KIISLAMU,....
... au kama wafanyavyo URUSI baada ya kustukia UKOMONISTI mambo zake valuvalu kitu ambacho NYERERE alistukia mapema na KUNG'ATUKA katika maswala ya KIJAMAA!:-(


Swali:
  •  Hivi unafikiri UBEPARI haujatushinda bado TANZANIA kwenye nchi ambayo hata sheria zetu bado ni za MUINGEREZA na wajanja ni waliosoma vitabu visivyo na asili ya TANZANIA?

  • Kwani hufikiri moja ya sababu AFRIKA dini za watu zinatuzingua  labda ni kwa sababu bado  YESU  wetu aka NABII ISSA bado ni MZUNGU na  Mtume MOHAMEDI (s.a.w) bado ni MUARABU?


Ndio,...
... labda TATIZO la UIGAJI wa KIAFRIKA  bado haujafikia kugeuza tuigavyo viwe vyetu KIVYETU,...
....kuanzia kwenye mambo ya DINI ambazo yanatugombanisha SISI  kwa SISI,...
.... mifumo ya UONGOZI , siasa na UCHUMI ambayo bado  hata kwa lugha za kikwetu bado twashindwa kuielezea  kwa wananchi wetu na  AJUAYE zaidi ni yule aliyesomea NJE na asifiwaye na PROFESA wa nje ambaye hahusiki na  maisha ya KILA SIKU ya MUAFRIKA  hapa AFRIKA,....
..... na yasemekana mpaka  hata katika maswala yale ya  chupi pia bado chupi bora  ni za nje.:-(


Swali:
  • Unabisha?


Ndio,...
....labda  AFRIKA  tatizo sio DINI za KIGENI,...
.....mifumo ya utawala ya kigeni , ....
....mifumo ya uchumi MPAKA hata  demokrasia zenye kifafa za nje ...
...... kama tungekuwa tunamkakati maalumu wa jinsi ya KUIGA na kugeuza tuyaigayo yawe YETU KIVYETU!:-(


NI UCHOKOZI TU huuu na ni WAZO TU HILI MHESHIMIWA,...
... na HAKI YA NANI TENA  wala usibanwe chupi!:-(


Hebu tubadili wazo kwa kumdeku BABA naye akinyonyesha- kwani nanikasema wanaume hawana matiti?:-(






Turudi tu ghafla MADAGASCAR ili DADAH adinye- Madimozely



Au ngojea tubakie kidogo tu zaidi hapa Madagascar ili KIAM'BE adinye pia na - Mavandy


4 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

EDNA 12:51 pm  

Mmmmh

emu-three 2:48 pm  

Tatizo, ni nini, kuiga au `umasikini'
Unajua kuna jamaa kaniambia kuwa uliwa masikini kila cha tajiri utakiona ni kizuri hata `mavi' yake...nilicheka kusikia hivyo...ni kwelii hilo nenokalitamka hivyo, `mavi' lakini lina maana ndefu ukilitafakari...hebu angalia tunayoiga sasa hivi, wenzetu walishayafanya kinyesi,...au tuseme mavi, sisi twayaona bora!
Ni hayo tu mkuu kwa nyongeza TUPO PAMOJA, NA USISAHAU TUMEKARIBISHWA MAKANDE KWA DADA YASINTA!

Simon Kitururu 3:03 pm  

@Edna: Mmmh!
@M3: Mimi nahisi tatizo sio kuiga bali ni``JINSI gani MTU anaiga!´´:-(

Umasikini na UTAJIRI nafikiri siomuhimu sana katika swala la KUIGA,...

....ndio maana utakuta kuna MATAJIRI walifikia kuchana mpaka MA-JEANS yao magotini na mpaka kwenye makalio kwa kuiga MASIKINI halafu ikaitwa kuwa ni FASHENI ambayo matajiri mpaka kama akina MADONA walishavyaa majinsi yenye viraka na kuchanikachanika.

Na nimekaribia MAKANDE kule kwa YASINTA ingawa naona kwao PURE na KIBULU vyote ni MAKANDE!

Yasinta Ngonyani 7:49 pm  

Mweh! :-) MAKANDE, PURE AU KIBULU ni mchanganyo wa mahindi na maharage nk au?

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP