Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Umuhimu wa kuwa wa MWISHO kwa mtu wa MWISHO!

>> Wednesday, May 25, 2011

MTU wa MWISHO,....
....labda ni MUHIMU sana kwa swala zima la kujisikia vizuri kwa ashangiliaye sana kwa kuwa WA KWANZA,....
.....kwa kuwa labda hakuna wa kwanza kama hakutakuwa na wa MWISHO!:-(


Swali:
  • Na si inasemekana ni DALILI ZA UDHAIFU FULANI  hata katika kitengo cha kujiamini  kwa MTU WA KWANZA kama anafarijika sana na kitendo cha kuwa WA KWANZA?


Na kwa kuwa kwa bahati mbaya  JAMII inafunza wanajamii kuthamini zaidi WA KWANZA ,...
..... kuwa WA PILI huanza kufikiriwa kama ni MWANZO wa KUSHINDWA.:-(


Na cha kusikitisha ni kwamba katika jamii huwa kuna baadhi husahau kuwa  katika kitu fulani kwa mfano umalaya - MTU  WA KWANZA,...
....labda ni katika kitu fulani tu NI WA KWANZA  na huyo huyo kwenye kitu kingine kwa mfano katika TAALUMA YA  kupiga chabo -huyo huyo WA KWANZA kwenye ya KEMIA kwenye WASHINDI wa HESABU  anaweza kuwa ndiye anayeSHINDWA.:-(

Swali:
  • Lakini  si labda isisahaulike kuwa- KUWA WA MWISHO kuna umuhimu wake na kama umuhimu huo hauko sana kwa WA MWISHO basi angalau uko kwa wengine hasa katika JINSI WANAVYOJISIKIA  walioko kwenye shindano?
  • Na si inasemekana USHINDI ufanyacho kikubwa ni kufariji tu kwa muda WALIO amini WAMESHINDA hasa kwa kuwa inasemekana wengi watoao zawadi kwa washindi ni wale isemekanao kuna kitu HAWAKUSHINDA?



Ndio,...
.... kwa kuwa  kama kuna WATU WAWILI,...
.... basi wa pili katika kidedeo ndiye WA MWISHO,...
....basi kama kuna mtu mmoja  labda wa kwanza ndiye wa MWISHO!

Ni wazo tu hili na usikonde MHESHIMIWA!:-(

Hebu Ayo aingilie kati kwa - Lonely



Ayo aendeleze kwa - Slow, Slow (Run Run)



Au tu Irma atulize kwa - I know


2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 8:47 am  

Haswa wa kwanza atakuwa wa mwisho na wa mwisho atakuwa wa kwanza:-(

Goodman Manyanya Phiri 5:35 am  

@Yasinta

Msemo wako huo unakujaje sasa katika mandhari hii?

Nitakupa jibu!!

Nikutokana na kwamba yule wa kwanza ni kifutio tu cha machozi ya wale waliojaribu kwa bidii labda kuliko yeye lakini wakashindwa kufanikiwa kuwa wa kwanza.

Watarudia bada ya kushindwa kwao, hakika! Na siku watakaposhinda nao, watafanya siyo tu makubwa kuliko yale yake wakwanza aliyeyafanya, bali wataweza hata kumkosoa kama ni wa kwanza kibandia tu.


Kifupi, usijidai sana kama wewe ni wa kwanza; na nafikiri Dada yangu umenukuu vizuri sana uliposema "wa kwanza atakuwa wa mwisho na wa mwisho atakuwa wa kwanza".

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP