Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Leo katika KISWANGLISH: You know when I was in MAKERERE ndio pale nili kutana na Miss LAWINO na kujua KURIDHIKA hufanya life cheap aisee!

>> Tuesday, May 03, 2011

You know life BWANA  is very  cantankerous na usipokuwa muangalifu aisee unaweza kujikuta unahangaika maisha yako yote bila kuwa satisfied yani!

Inabidi ujijue wewe na insecurities zako yani kama unataka life isiwe expensive  kwa kuwa unaweza kustukia moja ya kifanyacho maisha ni ghali ni katika tu kulipia insecurities zako ambazo zinaweza kujitokeza kwa nini unanunua cha ghali ili angalau u feel you are somebody -kuanzia nguo, magari, nyumba nakadhalika .

Na nilijifunzia hicho pale MAKERERE aisee  na unajua enzi zile  hasa baada ya kukutana na Miss LAWINO  ambaye  alikuwa msichana very smart kuanzia  kwenye ubongo  mpaka kwenye macho yake ya gololi na mashavu ya kumimina.


Msichana yule iko simple bwana na haina makuu na akili - utafikiri kutumia akili kwenye dictionary wameweka picha yake.

Yani those days wee acha tu! Yani kutokana na yeye ndio nikajua kuwa:

Maishani kitiacho gharama sana ni inferiority complex aisee. Kwa kuwa kama unajiamini unaweza kustukia mpaka kununua mitumba huogopi tena. Hutishiki na mabenzi ya watu. Huogopi kutochangia harusi na kitchen Party za usiowajua .Huogopi kula kwa mama Ntilie. 

Oh Miss Lawino halafu sijui yuko wapi maana mara ya mwisho nilikutana naye London wakati naenda Paris kuchekiwa meno kabla ya kurudi hapa Kigoma kwa ajili ya hii project!Musichana ile inaongea Kiingereza kama vile ni Queen Elizabeth yani!



Nje ya utani:

  • SI umestukia lakini jinsi inferiority complex na insecuritie katika MAISHA vinavyoweza kuwa ndio chanzo cha kuingia gharama zisizo na mpango hasa kwa ajili ya watu katika hii ku overcompansate?


Na ni wazo tu hili MHESHIMIWA ki -UjingaBUSARA!




Tahadhari: Leo katika KISWANGLISH:
...ni kipengele cha  kuwaenzi wasomi wetu TANZANIA  ambao moja ya kukutambulisha wameenda shule ni jinsi wachanganyavyo KISWAHILI na Kiingereza hata kwenye hotuba zao VIJIJINI  wakati wanaomba kura kwa wanakijiji ambao labda hawakwenda shule ukizingatia halihalisi ya uchumi ilivyo Tanzania!:-(


Swali:
  • Na ni  kwanini naandika kipengele hiki kuwaenzi hawa wanaoharibu KISWAHILI?

Jibu:
  • I donti noo!
  • Lakini si ni tabia nzuri labda kuwaenzi Waheshimiwa?

Na kuwaenzi hawa wasomi wetu labda tuwapigie tu wimbo wa kiingereza ..
na nahisi Welcome To My World kutoka kwa - Jim Reeves unaweza kusaidia hilo



Au tu angalau wimbo wa X-mass hata kama ni katika kipindi cha  majira ya PASAKA hasa kama santuri yenyewe iliyopo nyumbani kwenye radio gram ndio hiyohiyo ya X-mass.

White Christmas - Jim Reeves




Au tu The Mighty Sparrow wabadili kidogo na kututoa eneo fulani kiwazo kwa -Good morning Mr. Walker

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP